Mimi sio mtabili wala sio mchambuzi, ila
Simba atakua bingwa mpya wa kombe ya Shirikisho la Afrika jumapili 25-5- 2025.
Sababu zangu ni hizi:
-Baada ya kuangalia mechi ya kwanza huko Morocco,nimegundua RS Berkane sio wakali sana kuwazidi sana Simba,kama walivyokua wanaogopwa.Simba ameshacheza na timu ngumu zaidi ya RS Berkane,mfano Al Ahly na akazifunga nyumbani na zenyewe zilishinda kwao.
Sababu zangu kwa Nini Simba atabeba kombe ni hizi:
- katika mchezo wa Morocco RS Berkane hawakuweza kupata magoli zaidi ya mawili kwao,magoli waliyopata ni kutokana na
Goli la kwanza mpira
-Mpira uliokufa(Kona)Sikuona goli la ufundi wa kupangua mabeki wa Simba na kutupia mpira golini,
-Goli la pili
(Kagoma) alianguka Kwa bahati mbaya wakati alikua tayari ana mpira na ndipo mchezaji wa Berkane akaunasa na kupelekea kufunga,ukweli kama sio Kagoma kuanguka ulie mpira ungeokolewa na kupelekwa upande wa Berkane.
- RS Berkane walipata magoli Yao wakati Simba wakiwa hawajajipanga vizuri,
ndani ya dk 17 walikua wameshapata goli mbili.
Baada ya hapo, dk 28 za kipindi Cha kwanza na dk 45 za kipindi Cha pili chote RS Berkane hawakuoata goli Tena.
Kwa kipindi chote kilichobaki Cha dk 73 RS Berkane walidhibitiwa na Simba na hawakupata goli lolote,hii inaonesha Simba waliweza kuwadhibiti, tofauti na watu wengi waliodhani kuwa,Simba atafungwa nyingi.
Hii inaonesha kuwa ,Simba waliwamudu, Berkane sema tU, walipata faida ya kucheza kwao.
Hivyo ndivyo nae Simba Sasa atapata faida kama hiyo ya kucheza,na uzuri Simba hua anajua kutumia nafasi hii.
- kama mjuavyo mpira wa Afrika na hususani timu za kiarabu pamoja na kuujua mpira lakini pia huweza sana kucheza mpira nje ya uwanja,
(Fitina za soka),hivyo matokeo makubwa aliyoyapata Berkane dhidi ya Stellenbosch ni kutokana na ugeni na uchanga wa Stellenbosch katika mashindano ya Afrika,maana yangu ni kwamba Kuna namna RS Berkane waliwazidi Stellenbosch nje ya uwanja na hata Kwa sababu ya ugeni wao.
- RS Berkane aliweza kumfunga CS Constantine akiwa Morocco goli nne kwa sababu kama hizo nilizotaja za mpira wa kiafrika za mchezo machafu nje ya uwanja,lakini waliporudiana CS Constantine akiwa kwao, RS Berkane alifungwa goli moja bila,
Hapa utaona RS Berkane alishindwa kuonesha umwamba wake wa kupiga goli nyingi,alidhibitiwa vyema na CS Constantine.
Simba tulimfunga CS Constantine,tukaongoza kundi,kama ingekua ni mtoano tungemtoa.
Simba tulimfunga Constantine goli mbili,
Constantine alifungwa goli nne na Berkane,
Mechi ya pili Constantine akamfunga goli moja Berkane,
Simba tulifungwa goli mbil na Berkane,
Berkane anafungika,
Mechi ya pili Simba atamfunga Berkane.