Hii hoja ya kwamba kukatwa kwa Membe imewapooza mashabiki wa Lowasa ni hoja hafifu sana, Malengo yalikuwa EL agombee uraisi kupitia CCM hivyo kimkakati Membe hakuwa threat kabisa, kifupi ni umafia tu umetendeka kukata jina lake tokea kamati ya usalama na Maadili....
Kwa umri wa Lowasa hana cha kupoteza endapo atajitoa ndani ya CCM na kwenda kupitishwa na chama kingine kuwa mgombea uraisi kutimiza ndoto yake hiyo.... Ukweli ni kuwa kokote atakapoenda kwa upepo ulivyo sasa EL atakuwa ni zaidi ya threat kwa CCM.
kwa historia ya ukanda wetu huu wa Africa mashariki vyama tawala vilivyowapa Uhuru nchi nyingi vilianguka pale tu ambapo mtu aliyekubalika ndani kukatwa na kuamua kwenda kujiunga na vyama pinzani e.g Kenya & Zambia
Hivyo kwa kufuata historia hiyo EL bado ana fursa kubwa sana ya kufanya maajabu kwa kipindi hiki kifupi kilichobaki kuelekea uchaguzi mkuu akiwa njee ya CCM.
Regards
Cosmas
Mchambuzi Huru.
Lowasa hajatumia pesa zake toka mfukoni pesa nyingi alichangiwa na marafiki isitoshe Lowasa ni tajiri ana Mali nyingi hawezi kuchoka ataishi maisha ya kushiba bila njaa Kama Raila Odinga , wafuasi wa Lowasa wengi sasa wamehamia kwa magufuli kwani Adui wa Lowasa alikuwa Membe na sasa Membe kakatwa wameamua kumuunga mkono magufuli hawaendi kokote.
Litakuwa ni jambo la ajabu kabisa kama Team Lowassa hawakuwa na Plan B, hata mimi nitashangaa sana.
Kwani timu ya Membe ndiyo ilikuwa imemtuma ama kumshauri team Lowassa kufanya mbwembwe zilizozidi kimpimo hadi kuwafanya wananchi kuanza kujisikia kichefuchefu? Mimi ninafikiri mzee wa maamuzi magumu na timu yake kwa kiasi kikubwa walijichafua wenyewe. Walijitia upofu na ukiziwi wakalewa ukwasi ambao hapana shaka ulisababisha mafuriko ambayo hata hivyo yameweza kuzuiwa kwa vidole viwili tu! Tunamshukuru Muumba kwa hilo. Ninakubaliana na mJF mmoja ambaye amesema zuio hilo limetupunguzia mafisadi kadhaa.Timu Membe si watulivu bali walikuwa wachache sana na wengi walikuwa waganga wa kienyeji na vijana wa kushinda kwenye mitandao kupika uongo, uzushi na kila mbinu za kumchafua Lowasa , Membe yeye aliwatumia Nape, jack Gotham na Timu za kimafia ambazo sasa zimejikausha tayari na hawana kazi wameludi mitaani .
Subiri uone tofauti ya CDM na ZZK na CCM na Lowasa...mimi nitamuongelea km ccm walivyomuongelea ZZK,Lowasa anaongelewa na wana CCM na wasio CCM kwa malengo tofauti kwa sasa NChi nzima.Ina maana kama lowasa alikuwa chaguo la wengi,mbona haongelewi popote?
usichojua ni kwamba hiyo disorgazation dio shida kubwa kwa ccm..akiwa ndani ya ccm.Msizo usiofungwa au kuweka ktk mpangilio ktk ndege huangusha ndegeNi wazi hii ndio team pekee iliyokuwa na rasilimali fedha na watu lakini ilikosa uongozi au weledi.Tazama siku ya uzinduzi wa safari ya matumaini ilikuwa ni vurugu tupu.Hilo linaonekana mpaka sasa kwa kuwa baada ya kukatwa team hii imepagawa na kuchanganyiwa kabisa.1-Kuna kundi limechana kadi za ccm.2-Kuna kundi limetangulia ACT3-Kuna kundi limebaki kimya ndani ya ccm4-Kuna kundi limemsapoti magufuli5-Kuna kundi linatishia kwenda CDM6-Kuna kundi halijulikani linafanya nini Bashe yuko kimyaa!Kingunge yuko kimyaa!Nchimbi,Simba na Kimbisa hatukusikia kama waliwasilisha ile rufaa yao au la.Yale mabasi ya Team lowassa hayajulikani yalipo yaani ni full chaos.Hii ni ishara tosha ya kutokujipanga kwa Team hii.kwa upande wa Team membe bado ni watulivu
ha ha ha ha, mungu anaangalia mwisho na sio mwanzo. Kwisheny, Lowasa hakuwa na ma strategist bali aliwa confuse washikaji na watekaji. Hiyo safi sana International school ya Wakina Lau, kinje Joseph kusaga karudi toka Dubai akijua ushindi ni wao, ephramim kibonde, Bashe, Kingunge, nchimbi sofia simba ndio vichwa cha Mamvi, pole sana hata, ile nyomi ya mafisadi Arusha ndio aliona imemtoa, pale pale wakali tulichua kachemsha, kweli sayansi haina siasa, kila tulichoon kimetokea hakuhitaji expatriate kujua kama hamnazo, kweli akili ni nywele
Lowasa alizungukwa na money mongers na si wafuasi
Hawa team ya Lowasa watakiwa wameenda kujitumbikiza baharini kuogopa aibu
Ina maana kama lowasa alikuwa chaguo la wengi,mbona haongelewi popote?
Aibu ipi ? Kwenye kutafuta na kupata na kukosa , Lowasa alijua njama za kumwengua mapema hivyo alijiandaa Kwa lolote lile.