JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,318
- 5,483
ZAIDI ya laini 21,788 za mawasiliano ya simu zimefungiwa kupokea na kutoa mawasiliano kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo kutumika kufanya uhalifu mtandaoni kwa kipindi cha miezi mitatu iliopita.
Kwa mujibu wa ripoti ya mwenendo wa sekta ya mawasiliano iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jabiri Bakari, idadi ya matukio ya ulaghai imeendelea kupungua kutoka laini za simu 23,328 zilizofungiwa Julai na Septemba 2023 hadi laini za simu 21,788 kwa Oktoba hadi Desemba 2023 ikiwa ni upungufu wa laini za simu 1,540, sawa na asilimia 6.6.
Aliitaja mikoa inayoongoza kwa matukio ya simu za ulaghai hadi kufikia Desemba mwaka 2023 na idadi ya kwenye mabano ni Rukwa (7,666) na Morogoro (7,171), Dar es Salaam (1,717), Mbeya 1,549, Tabora 590 na Songwe 328. Mikoa yenye matukio machache ni Kaskazini Pemba (5), Kusini Pemba (6) na Mtwara (22).
Dkt. Bakari alisema TCRA imeendelea kubaini simu za ulaghai zinazoingia nchini na hatua stahiki zimekuwa zinachukuliwa ambapo idadi ya simu za udanganyifu imeendelea kupunguwa.
Chanzo: Nipashe
Kwa mujibu wa ripoti ya mwenendo wa sekta ya mawasiliano iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jabiri Bakari, idadi ya matukio ya ulaghai imeendelea kupungua kutoka laini za simu 23,328 zilizofungiwa Julai na Septemba 2023 hadi laini za simu 21,788 kwa Oktoba hadi Desemba 2023 ikiwa ni upungufu wa laini za simu 1,540, sawa na asilimia 6.6.
Aliitaja mikoa inayoongoza kwa matukio ya simu za ulaghai hadi kufikia Desemba mwaka 2023 na idadi ya kwenye mabano ni Rukwa (7,666) na Morogoro (7,171), Dar es Salaam (1,717), Mbeya 1,549, Tabora 590 na Songwe 328. Mikoa yenye matukio machache ni Kaskazini Pemba (5), Kusini Pemba (6) na Mtwara (22).
Dkt. Bakari alisema TCRA imeendelea kubaini simu za ulaghai zinazoingia nchini na hatua stahiki zimekuwa zinachukuliwa ambapo idadi ya simu za udanganyifu imeendelea kupunguwa.
Chanzo: Nipashe