TCRA wawataka Watangazaji wa Redio na Runinga nchini kutumia Lugha ya Kiswahili tu na siyo Kuchanganya na Kiingereza wakiwa Hewani

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,638
109,006
"Tumevitaka Vyombo vyote vya Habari nchini hasa kwa Watangazaji wa Redio na Runinga kutumia tu Lugha ya Kiswahili wawapo Hewani na siyo Kuchanganya Kiswahili na Kiingereza. Na kibaya zaidi unamsikia Mtangazaji anachanganya hizo Lugha halafu hata hilo neno lenyewe la Kiingereza hajui kulitamka au analikosea ila ilimradi tu nae ajitutumue kwa Wasikilizaji ili wajue kuwa Wanakijua" amesema Afisa Mwandamizi wa TCRA jana ( Alhamisi ) alipokuwa katika Studio za EFM Radio.

Haya TCRA nami GENTAMYCINE nawashauri ili hili Tamko lenu ( Mkwara Mbuzi wenu huu ) ukubalike kwa Wadau wenu ( Watangazaji ) mngeweka Sheria itakayoambatana na Faini Kubwa kwa Mtangazaji na Chombo husika ili Lifanikiwe vinginevyo naona ni kama vile mnapaka tu Rangi Upepo.

Ninakipenda mno Kiswahili changu.
 
Hilo ni tatizo la kijamii.

Kuna baadhi ya watu huona kuchanganya lugha kwa kuchomekea maneno ya Kiingereza kuwa ndo usasa.

Hata humu kuna watu nawajua kabisa kuwa Kiingereza hakipandi lakini hawaishi kuchomekea hiyo lugha katika matundiko yao.

Inachekesha.
 
"Tumevitaka Vyombo vyote vya Habari nchini hasa kwa Watangazaji wa Redio na Runinga kutumia tu Lugha ya Kiswahili wawapo Hewani na siyo Kuchanganya Kiswahili na Kiingereza. Na kibaya zaidi unamsikia Mtangazaji anachanganya hizo Lugha halafu hata hilo neno lenyewe la Kiingereza hajui kulitamka au analikosea ila ilimradi tu nae ajitutumue kwa Wasikilizaji ili wajue kuwa Wanakijua" amesema Afisa Mwandamizi wa TCRA jana ( Alhamisi ) alipokuwa katika Studio za EFM Radio.

Haya TCRA nami GENTAMYCINE nawashauri ili hili Tamko lenu ( Mkwara Mbuzi wenu huu ) ukubalike kwa Wadau wenu ( Watangazaji ) mngeweka Sheria itakayoambatana na Faini Kubwa kwa Mtangazaji na Chombo husika ili Lifanikiwe vinginevyo naona ni kama vile mnapaka tu Rangi Upepo.

Ninakipenda mno Kiswahili changu.
Huko FM studios wanejaa kina Shilole type kwa wingi.
Hii kitu inakera kwa sababu vituo vyao vimeomba leseni za kurusha matangazo kwa lugha ya kiswahili.
Sasa hawa watangazaji uchwara wao wanageuza kuwa sehemu za kuuzia sura binafsi.
 
Haya wachambuzi wa mchongo wamefikiwa wazee wa one v one,diagonal pass(hili neno diagonal niamini mimi wachambuzi wengi hawajaui kuliandika),on target shot,technically kama yule George Job ndio anapoga kiswanglish ambacho ni kuunga sana.
 
Safi sana TCRA, hiki kitu Mimi mwenyewe kinaniudhi.

Lakini na ninyi TCRA mbona ni kifupi Cha neno la kiingereza tumieni kiswahili pia.
 
"Tumevitaka Vyombo vyote vya Habari nchini hasa kwa Watangazaji wa Redio na Runinga kutumia tu Lugha ya Kiswahili wawapo Hewani na siyo Kuchanganya Kiswahili na Kiingereza. Na kibaya zaidi unamsikia Mtangazaji anachanganya hizo Lugha halafu hata hilo neno lenyewe la Kiingereza hajui kulitamka au analikosea ila ilimradi tu nae ajitutumue kwa Wasikilizaji ili wajue kuwa Wanakijua" amesema Afisa Mwandamizi wa TCRA jana ( Alhamisi ) alipokuwa katika Studio za EFM Radio.

Haya TCRA nami GENTAMYCINE nawashauri ili hili Tamko lenu ( Mkwara Mbuzi wenu huu ) ukubalike kwa Wadau wenu ( Watangazaji ) mngeweka Sheria itakayoambatana na Faini Kubwa kwa Mtangazaji na Chombo husika ili Lifanikiwe vinginevyo naona ni kama vile mnapaka tu Rangi Upepo.

Ninakipenda mno Kiswahili changu.
Namkubali Sana Samson Charles wa EATV jamaa anajitahidi Sana ajishaui kama wengine Kwa viingereza vya off course na you know
 
Wachambuzi wa mpira hapa tayali wame banwa kwenye Kona hawatoboi,

wengine wa kupigwa marufuku kuchafua lugha ni wabunge, yani wako pale kwa ajili ya waswahili lakini cha ajabu mtu hawezi kuongea maneno 10 hadi 15 bila kuchomekea kakingereza na sababu kubwa hua ni utumwa wa akili kudhania kwamba wakiongea kingereza basi wataonekana wasomi, hadi msukuma na yeye unakuta anajitutumua kuongea asivyo vielewa
Lakini na nyie TCRA mbona ni kifupi cha maneno ya kingereza na wakati ni shirika kwa ajili ya waswahili 🤔🤔
 
Watangazaji wa michezo wanapenda kuweka kingereza kutupia wakiwa wanachambua habari, waonekane wamesoma au wanajua kingereza.
 
Back
Top Bottom