TCRA: Watumiaji wa Huduma ya Intaneti wameongezeka kutoka Milioni 54.1 (Juni 2025) hadi Milioni 56.3 (Septemba 2025) sawa na 4.1%

TCRA: Watumiaji wa Huduma ya Intaneti wameongezeka kutoka Milioni 54.1 (Juni 2025) hadi Milioni 56.3 (Septemba 2025) sawa na 4.1%

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472
SnapInsta.to_565862164_18171129301365536_8806349910858270622_n.jpg
Huduma ya intaneti inaonesha kuongezeka utumiaji kutoka milioni 54.1 mwezi Juni 2025 hadi kufikia milioni 56.3 mwezi Septemba 2025 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 4.1.

Kwa mujibu wa ripoti ya takwimu ya sekta ya Mawasiliano ya robo mwaka inayoishia Septemba 2025 inaonesha idadi ya utumiaji wa intaneti inatokana na laini/waya ambazo zimetumia huduma ya Intaneti angalau mara moja katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita, bila kujali teknolojia iliyotumika (FTTX, 2G - GPRS na EDGE, 3G, 4G, au 5G).

Ripoti hiyo imefafanua kuwa huduma ya intaneti kwa njia ya simu ya mkononi inapendelewa zaidi (99%) ikilinganishwa na huduma ya intaneti isiyohashimishika.

Kuongezeka kwa utumiaji wa intaneti unatokana na ubora wa huduma na miundombinu inayowezesha upatikanaji wa mawasiliano kwa wananchi.

Tembelea tovuti ya TCRA (www.tcra.go.tz) kwenye kipengel cha Machapisho, kisha bofya Takwimu, au bofya kiunganishi https://bit.ly/48CADOW ili kusoma ripoti nzima ya Sekta ya Mawasiliano (Julai – Septemba 2025).
 
Wastani wa kasi ya internet Tanzania ni Mbps 30, CCM lazima itoke
 
Sasa kama kuna mitandao imefungiwa, TCRA haioni kuwa hiyo hesabu imepungua?
 
Back
Top Bottom