TCRA Wakomesha wizi wa simu za mkononi

TCRA Wakomesha wizi wa simu za mkononi

nilishafanya nao kazi ila wao hawakujua nilikua nafanyautafiti kile kitengo hakitoi matokeo chanya kama kilivyokusudiwa kuna mapendekezo nilitoa huenda kikafanyiwa reform kiutendaji
 
Mkuu mtu akiiba simu akaenda kuuza mtu akanunua iko locked, wakiendelea hivohivo mara kadhaa itafika muda mtu kabla hajanunua kitu anahakikisha kua haiko blacklisted, mwisho wa siku wezi watakosa soko sababu kila mtu atataka kukagua simu kwanza....

Labda wabadilishe IMEI process nyingine hiyo vibaka wengi bongo hapa hiyo knowledge hawana
Tatizo itaibuka biashara ya screen za simu,housing ,mother bodyand batery Darn!
 
Habari wanabodi,

TCRA imesikia vilio vya wadau wa simu za mkononi,taarifa za ndani zinasema kwamba kuanzia May 2015 simu yako ikiibiwa piga simu haraka sana huduma kwa wateja TCRA kuelezea upotevu wa simu yako,jambo la msingi ni kukumbuka IMEI/ESN ya hiyo simu TCRA kwa kushilikiana na mitandao ya simu wameanzisha CEIR (Bonyeza hapa Kujua maana) ambayo itakayoanza kufanya kazi May 2015.

Sasa mwizi akiiba simu yako haitofanya kazi tena chini tanzania hata wakii-flush kwa matapeli wa k/koo.Safi Sana TCRA

CEIR ni nini? Ni mtambo ambao utakuwa unafanya kazi ya kuzuia simu zilizolipotiwa kama za wizi zisiweze kukamata mtandao wowote nchini tanzania.Hii ina maanisha ukishareport upotevu wa simu na ikishakuwa blocked that means hiyo simu inakuwa Toy la kuchezea watoto.

Kwa upande mwingine inaweza kuwa pigo kwa wafanyabiashara wanaoleta simu zilizoibiwa nje ya tanzania kuja kuuza huku nchini kwetu kama TCRA wakiunganisha na CEIR za nchi nyingine maana hazitofanya kazi pia nchini.

Daaa fursa hii mie nitanunua hizo za wizi kwa elfu 10 na kujua wapi pa kuzipeleka, TCRA si waanze ata kesho huu mpango aisee
 
Ni wazo zuri na nawapongeza TCRA bt am xure halitoleta matokeo mazur.
 
Kama wangeanza na hawa wezi wa vocha zetu i. e mitandao ya simu ningewapongeza sana au wamekuja kuzima fikra zetu za kuibiwa na mitandao
 
Mtandao wa wezi ukishapata hizi taarifa watakaa kikao kujua jinsi gani wataweza kuuiba hiyo CEIR kwanza ili wasife njaa hehehehe :lol:
 
Hawawezi kufanya hilo...

Mim nawaonaga wahuni tu.... mambo mengi ya deal chafu yanafanyika kwa kutumia mitandao ya simu lakini hakuna lolote walilofanya.... vitengo muhimu kama TCRA kwa nchi za wenzetu lazima kiwe chini ya Jeshi au Taasisi ya usalama wa Taifa ili kifanye kazi vizuri.
 
Nilipoteza simu two weeks ago nilipokuwa Tz. Niliporudi niliwataarifu network providers wangu wakaiblock.

Kama ni Iphone unaweza pia kuiblock kwa any other device kama umeiunga na iCloud. Ikiwashwa sehemu yenye wifi, inapiga alarm na kudisplay message yoyote utakayodesign.

simu umeiacha bongo, provider wako wa huko hana mamlaka juu ya provider wa huku, jizi la hiyo simu bado linaitumia kama kawaida.
 
hawawezi kufanya hilo...mm nawaonaga wahuni tu....mambo mengi ya deal chafu yanafanyika kwa kutumia mitandao ya simu lakini hakuna lolote walilofanya....vitengo muhimu kama TCRA kwa nchi za wenzetu lazima kiwe chini ya Jeshi au Taasisi ya usalama wa Taifa ili kifanye kazi vizuri.

Tuwaamini wao waliosema wameshapata huo mtambo na miezi mitatu ijayo utakuwa ushaunganishwa na provider wote, au wewe mjuzi wa kupiga soga JF?
 
nilishafanya nao kazi ila wao hawakujua nilikua nafanyautafiti kile kitengo hakitoi matokeo chanya kama kilivyokusudiwa kuna mapendekezo nilitoa huenda kikafanyiwa reform kiutendaji

Ulitoa mapendekezo kwa nani?
 
simu umeiacha bongo, provider wako wa huko hana mamlaka juu ya provider wa huku, jizi la hiyo simu bado linaitumia kama kawaida.

Imefungiwa simu sio subscription ya network.

Simu imefungiwa kwa:

1. Apple ID through iCloud kwa kupitia my iPhone. Hakuna atakayeweza kuifunga unless ana password
2. Apple wameifunga simu kwa kutumia IME number-haipo kwenye network yao tena
 
Stefano Mtangoo,

Kama ulinunua simu kwa laki 2 tena miaka mitatu nyuma haina haja ya kuifuatilia ila kama umenunua simu milion 1.5 tena ina mwaka lazima uifuatilie hadi uipate.
 
Last edited by a moderator:
Hizi stori za CyberCrime nimezisikia sana tu lakini sijui kama ni kweli. Nimepoteza Simu January mpaka sasa sijaipata!
Wako uchochoro gani? Na kwa nini wamejificha? Mpaka uunganishwe????

Tatizo lingine la Tanzania ndio hili, kuna watu wenye utaalamu lakini hawajitokezi
 
let say nimeiba galaxy s5 yako, then nikachange imei nikaeka nikaeka ya galaxy s5 ya kenya ambazo ni version moja ya africa watajuaje?

Ukumbuke details za simu zinakaa kwenye efs folder hivyo ni rahisi kuudanganya mtambo wowote duniani usijue. nchi kubwa duniani wameshindwa ku implement hiki kitu ndio maana unaona nina doubt.

Hiki kitu kinatakiwa kifanywe na watengeneza simu wenyewe.

Wezi wenye utaalamu kama wako hawapo au wapo wachache sana.
 
Wezi wenye utaalamu kama wako hawapo au wapo wachache sana.

kaka app zipo hapo playstore kuchange imei (simu za mediatek) au ukiikosa playstore zinapatikana kirahisi tu mtandaoni hazihitaji utaalamu wowote.
 
kaka app zipo hapo playstore kuchange imei (simu za mediatek) au ukiikosa playstore zinapatikana kirahisi tu mtandaoni hazihitaji utaalamu wowote.
Ukibadili IMEI na ukagundulika adhabu ni fine ya milioni 30 au miaka mi3 jela au vyote kwa pamoja.

-Kesho ndio utaujua uwezo wa huu mtambo CEIR simu feki zote chali.
 
Back
Top Bottom