TCRA Wakomesha wizi wa simu za mkononi

TCRA Wakomesha wizi wa simu za mkononi

Amalinze

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2012
Posts
6,780
Reaction score
5,322
Habari wanabodi,

TCRA imesikia vilio vya wadau wa simu za mkononi,taarifa za ndani zinasema kwamba kuanzia May 2015 simu yako ikiibiwa piga simu haraka sana huduma kwa wateja TCRA kuelezea upotevu wa simu yako,jambo la msingi ni kukumbuka IMEI/ESN ya hiyo simu TCRA kwa kushirikiana na mitandao ya simu wameanzisha CEIR (Bonyeza hapa Kujua maana) ambayo itakayoanza kufanya kazi May 2015.

Sasa mwizi akiiba simu yako haitofanya kazi tena chini tanzania hata wakii-flush kwa matapeli wa k/koo.Safi Sana TCRA

CEIR ni nini? Ni mtambo ambao utakuwa unafanya kazi ya kuzuia simu zilizoripotiwa kama za wizi zisiweze kukamata mtandao wowote nchini Tanzania.BHii ina maanisha ukishareport upotevu wa simu na ikishakuwa blocked that means hiyo simu inakuwa Toy la kuchezea watoto.

Kwa upande mwingine inaweza kuwa pigo kwa wafanyabiashara wanaoleta simu zilizoibiwa nje ya Tanzania kuja kuuza huku nchini kwetu kama TCRA wakiunganisha na CEIR za nchi nyingine maana hazitofanya kazi pia nchini.
 
Bado hujawajua wezi vizuri.
Mkuu mtu akiiba simu akaenda kuuza mtu akanunua iko locked, wakiendelea hivohivo mara kadhaa itafika muda mtu kabla hajanunua kitu anahakikisha kua haiko blacklisted, mwisho wa siku wezi watakosa soko sababu kila mtu atataka kukagua simu kwanza....

Labda wabadilishe IMEI process nyingine hiyo vibaka wengi bongo hapa hiyo knowledge hawana
 
Nilipoteza simu two weeks ago nilipokuwa Tz. Niliporudi niliwataarifu network providers wangu wakaiblock.

Kama ni Iphone unaweza pia kuiblock kwa any other device kama umeiunga na iCloud. Ikiwashwa sehemu yenye wifi, inapiga alarm na kudisplay message yoyote utakayodesign.
 
Mkuu mtu akiiba simu akaenda kuuza mtu akanunua iko locked, wakiendelea hivohivo mara kadhaa itafika muda mtu kabla hajanunua kitu anahakikisha kua haiko blacklisted, mwisho wa siku wezi watakosa soko sababu kila mtu atataka kukagua simu kwanza....

Labda wabadilishe IMEI process nyingine hiyo vibaka wengi bongo hapa hiyo knowledge hawana

hawa naona wanawetengenezea watu diri! Hapa kuna mtu atakuwa billionea teba kutoka hapo TCRA kama wanawafanya kazi majinias atahachofanya ni kutengeneza progran ya ku unlock simu kwisha habari yake!
 
Mkuu mtu akiiba simu akaenda kuuza mtu akanunua iko locked, wakiendelea hivohivo mara kadhaa itafika muda mtu kabla hajanunua kitu anahakikisha kua haiko blacklisted, mwisho wa siku wezi watakosa soko sababu kila mtu atataka kukagua simu kwanza....

Labda wabadilishe IMEI process nyingine hiyo vibaka wengi bongo hapa hiyo knowledge hawana

mkuuu zitaibiwa sana tuu nakuuzwa kama scrapper na zitakuwa maalum kwaajili ya spea tuuu.
 
TCRA niwapongeze kwa hili ila mimi nina mawazo tofauti. Badala ya kuiblock, TRA wawe na ACCESS na HRL/VLR za makampuni yote Tanzania ili waweze kujua anayetumia hiyo simu yuko na namba gani kwa ajili ya kumkamata. Hiyo itasaidi
  1. Mpoteza Simu apate mali yake
  2. Mwizi au angalau mpenda vya dezo akamatwe (Itazuia watu kupenda vya kunyonga)

Ni hatua nzuri lakini si wengi wataripoti ili tu simu ifungiwe, wengi watatamani wawajue wezi wao na kupata vifaa vyao!
 
Last edited by a moderator:
TCRA niwapongeze kwa hili ila mimi nina mawazo tofauti. Badala ya kuiblock, TRA wawe na ACCESS na HRL/VLR za makampuni yote Tanzania ili waweze kujua anayetumia hiyo simu yuko na namba gani kwa ajili ya kumkamata. Hiyo itasaidi
  1. Mpoteza Simu apate mali yake
  2. Mwizi au angalau mpenda vya dezo akamatwe (Itazuia watu kupenda vya kunyonga)

Ni hatua nzuri lakini si wengi wataripoti ili tu simu ifungiwe, wengi watatamani wawajue wezi wao na kupata vifaa vyao!

Mkuu hili la kujua mtumiaji linafanyika, polisi wetu wanavyo vifaa vya kujua hili. Pia polisi wana uwezo wa kuwataka makampuni ya simu kutoa taarifa za simu hiyo. Mimi ni mfaidika wa hili suala baada ya co-worker mwenzangu kunizunguka na kuniingiza mkenge wa utapeli wa mzigo wa milioni 20. Ni bahati nzuri nilikuwa na polisi rafiki yangu ambaye aliniunganisha na watu wa cybercrimes na tukafanikiwa kugundua kuwa aliyekuwa nyuma ya tukio ni mfanyakazi mwenzangu. Mara ya pili niliibiwa simu, nikamtafuta huyu polisi akaniunganisha tena na watu wa cybercrimes, tulimkamata mwizi kama vile kifaranga kimenyeshewa na mvua.

Tatizo ninaloliona ni mazingira ya ufanyaji kazi kwa upande wa polisi ambapo yamekaa kwa kujuana sana au kirushwa rushwa ndio maana huu wizi haukomi pamoja na kwamba vifaa wanavyo. Mimi binafsi baada ya hayo matukio mawili nilijifunza kitu kuwa kamwe usinunue simu mikononi wa mtu tena usiyemjua, hakika utatwisha kesi bila kutarajia. Hata ukibadili laini mara mia, ilimradi hiyo simu inaconnect kwenye network lazima iache footprints na utakamatwa.
 
Mkuu hili la kujua mtumiaji linafanyika, polisi wetu wanavyo vifaa vya kujua hili. Pia polisi wana uwezo wa kuwataka makampuni ya simu kutoa taarifa za simu hiyo. Mimi ni mfaidika wa hili suala baada ya co-worker mwenzangu kunizunguka na kuniingiza mkenge wa utapeli wa mzigo wa milioni 20. Ni bahati nzuri nilikuwa na polisi rafiki yangu ambaye aliniunganisha na watu wa cybercrimes na tukafanikiwa kugundua kuwa aliyekuwa nyuma ya tukio ni mfanyakazi mwenzangu. Mara ya pili niliibiwa simu, nikamtafuta huyu polisi akaniunganisha tena na watu wa cybercrimes, tulimkamata mwizi kama vile kifaranga kimenyeshewa na mvua.

Tatizo ninaloliona ni mazingira ya ufanyaji kazi kwa upande wa polisi ambapo yamekaa kwa kujuana sana au kirushwa rushwa ndio maana huu wizi haukomi pamoja na kwamba vifaa wanavyo. Mimi binafsi baada ya hayo matukio mawili nilijifunza kitu kuwa kamwe usinunue simu mikononi wa mtu tena usiyemjua, hakika utatwisha kesi bila kutarajia. Hata ukibadili laini mara mia, ilimradi hiyo simu inaconnect kwenye network lazima iache footprints na utakamatwa.
Hizi stori za CyberCrime nimezisikia sana tu lakini sijui kama ni kweli. Nimepoteza Simu January mpaka sasa sijaipata!
Wako uchochoro gani? Na kwa nini wamejificha? Mpaka uunganishwe????
 
Hizi stori za CyberCrime nimezisikia sana tu lakini sijui kama ni kweli. Nimepoteza Simu January mpaka sasa sijaipata!
Wako uchochoro gani? Na kwa nini wamejificha? Mpaka uunganishwe????

Kitengo cha cybercrimes kipo makao makuu ya polisi, Dar. Kiutaratibu, mhanga wa huo wizi anapaswa tu kutoa taarifa kituo chochote cha polisi kuhusu upotevu huo wa simu, kisha wao kama polisi ndio wanajua kitengo kipi kinaweza kushughulikia tatizo hilo. Mhanga wa tukio hapaswi kujua internal operations za polisi. Ila kwa sababu ya rushwa, uvivu, kujuana, kutowajibika na mapungufu mengi yanayowaandama polisi, hiki kitengo hakiwi full utilized kama inavyopaswa, ni wachache tu ndio wanafaidika na huduma ya hiki kitengo.
 
Sidhani kama kuna international database ya blacklisted IMEIs, nadhani watatengeneza database yao wenyewe ambayo ita-run hapahapa Tanzania..

Its a good move though! Itapunguza wizi, sema on the other hand nawaonea huruma wasio na pesa, wananunua vya wizi ka bei nafuu afu walioibiwa wananunua nyingine, sema sasa hawapati nafasi hiyo tena..
Sio wasio na pesa tu, sema wasiochukua hatua ya kununua vyao maana hata wasio na pesa wengi hujichanga na kununua vya halali na wengine na hela zao huvizia vya kunyonga
 
mkuuu zitaibiwa sana tuu nakuuzwa kama scrapper na zitakuwa maalum kwaajili ya spea tuuu.
Hii nayo itakuwa CREATIVITY ila kwa njia haramu, hawa jamaa ni noma hawshindwi, wengine wanaweza wakawa wanaiba kukomeshea tu
 
Kitengo cha cybercrimes kipo makao makuu ya polisi, Dar. Kiutaratibu, mhanga wa huo wizi anapaswa tu kutoa taarifa kituo chochote cha polisi kuhusu upotevu huo wa simu, kisha wao kama polisi ndio wanajua kitengo kipi kinaweza kushughulikia tatizo hilo. Mhanga wa tukio hapaswi kujua internal operations za polisi. Ila kwa sababu ya rushwa, uvivu, kujuana, kutowajibika na mapungufu mengi yanayowaandama polisi, hiki kitengo hakiwi full utilized kama inavyopaswa, ni wachache tu ndio wanafaidika na huduma ya hiki kitengo.

Le Mutuz anashirikiana na CYBERCRIME ya sentelo kuwashikisha adabu wanaomtukana.
 
labda waziban simu za android ndo hilo zoezi litafanikiwa. maana kuchange imei nirahisi kuna app hadi playstore zipo

Heshima kwako mkuu Chief-Mkwawa,
TCRA wapo smart sana walijua zipo software za kufanya alteration of IMEI ndio maana huo mtambo una-detect hata simu zilizokuwa na Fake/Forged IMEI na kuzifungia na hata wakiiga imei ya simu nyingine ina detect phones with duplicate IMEI na kuifungia ya pili iliyo-copy hiyo IMEI,kwa kifupi hakuna ujanja watakaoufanya hao wezi.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom