tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesisitiza umuhimu wa vyombo vya habari, hususan vya mtandaoni, kuzingatia miongozo na kanuni za uandishi wa habari kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Soma pia: Hali ya Vyombo vya Habari kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025: Kuna uhuru wa kutosha katika utekelezaji wa majukumu yao?
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo katika kikao kazi kilichowakutanisha waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali, Meneja wa Kitengo cha Huduma za Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, ameeleza kuwa kwa kuwa dunia ya sasa inaendeshwa na teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), ni muhimu maudhui ya mtandaoni yazingatie maadili na weledi, hususan katika matangazo ya moja kwa moja (live broadcasts).
"Vyombo vya habari vya mtandaoni vinapaswa kuwa na rasilimali watu muhimu kama mhariri na mhariri mkuu, badala ya kuwa kazi ya mtu mmoja anayefanya kila kitu – kuandika, kuhariri na kupandisha maudhui mtandaoni," amesema Kisaka.
"Hatutavumilia ‘one-man show’ inayokosa uhariri wa kitaalamu."
Aidha, amebainisha kuwa matangazo ya moja kwa moja yanaweza kuwa chanzo cha uchochezi, kwa kuwa huonesha moja kwa moja maeneo ya tukio, muda, na hata mahali walipo askari wa usalama – jambo ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa taifa.
“Matangazo ya moja kwa moja yanahitaji kuchujwa kwa umakini. Kama kuna machafuko, je ni sahihi kuonesha kila kitu bila kujali athari zake kwa jamii?” amehoji Kisaka.
Akiwaasa waandishi wa habari, Kisaka amesisitiza umuhimu wa kujiepusha na vichwa vya habari vyenye lugha ya uchochezi au vinavyolenga upande mmoja wa kisiasa. Alisema ni wajibu wa waandishi kuhakikisha wanatoa taarifa sahihi, zisizoegemea upande wowote, na zinazosaidia kudumisha amani.
Chanzo: nipashe digital
Soma pia: Hali ya Vyombo vya Habari kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025: Kuna uhuru wa kutosha katika utekelezaji wa majukumu yao?
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo katika kikao kazi kilichowakutanisha waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali, Meneja wa Kitengo cha Huduma za Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, ameeleza kuwa kwa kuwa dunia ya sasa inaendeshwa na teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), ni muhimu maudhui ya mtandaoni yazingatie maadili na weledi, hususan katika matangazo ya moja kwa moja (live broadcasts).
"Vyombo vya habari vya mtandaoni vinapaswa kuwa na rasilimali watu muhimu kama mhariri na mhariri mkuu, badala ya kuwa kazi ya mtu mmoja anayefanya kila kitu – kuandika, kuhariri na kupandisha maudhui mtandaoni," amesema Kisaka.
"Hatutavumilia ‘one-man show’ inayokosa uhariri wa kitaalamu."
Aidha, amebainisha kuwa matangazo ya moja kwa moja yanaweza kuwa chanzo cha uchochezi, kwa kuwa huonesha moja kwa moja maeneo ya tukio, muda, na hata mahali walipo askari wa usalama – jambo ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa taifa.
“Matangazo ya moja kwa moja yanahitaji kuchujwa kwa umakini. Kama kuna machafuko, je ni sahihi kuonesha kila kitu bila kujali athari zake kwa jamii?” amehoji Kisaka.
Akiwaasa waandishi wa habari, Kisaka amesisitiza umuhimu wa kujiepusha na vichwa vya habari vyenye lugha ya uchochezi au vinavyolenga upande mmoja wa kisiasa. Alisema ni wajibu wa waandishi kuhakikisha wanatoa taarifa sahihi, zisizoegemea upande wowote, na zinazosaidia kudumisha amani.
Chanzo: nipashe digital