TCRA: Kutoa taarifa za siri za mawasiliano ni kosa la jinai

Wanataka kufungiwa gazeti la mwanahalisi isihojiwe kwa sababu kesi iko mahakamani
 
Safi sana Mwanahalisi mshitakiwa wa kwanza ataieleza mahakama alipataje siri za wateja wa TiG0.
 
Likes Received 860Likes Given 860

what a coincidence


mkuu itabidi kila ukipewa like na wewe unagonga ili ziende sambamba, teh teh!
:focus: kama wataweza kufunga na mitandao ya kijamii basi hapo ndo watakuwa wame'win kutufunga mdomo na kutuweka gizani./
 
kha.. Juzi hapa taarifa ya mkulu imesema gazeti la Mwanahalisi linaandika uvumi na uchochezi na uongo mtupi, hii leo wengine hawa wanakiri kwamba kuna taarifa zimevujishwa .. sasa mbona double std..

Mgonjwa akiwa kwenye nukta, anapumulia mashine, basi kila tabibu atajichomea misindano yake LIWALO NA LIWE, POTELEA MBALI, labda dozi hii au ile itamtoa mautini maskini mgonjwa wetu.. POLENI VIPOFU WA KUONGOZA ..
 
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAI

Hivi karibuni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imegundua kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunzaji wa siri za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa huduma za mawasiliano ya simu za mkononi. Mawasiliano hayo yamefikia hatua ya kuchapishwa katika vyombo vya habari.

Mamlaka ya Mawasiliano inapenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wenye makampuni ya Simu na wananchi kwa ujumla kuwa, kutoa taarifa za mawasiliano binafsi ya simu bainA ya watumiaji wa huduma hiyo, ni uvunjaji wa Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta Na. 3 ya mwaka 2010 na Kanuni za Mawasiliano (Kulinda Wateja) za mwaka 2005.

Kifungu cha 98 ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kinasema;

(1) “Mtu yeyote ambaye ni mfanyakazi wa kampuni yenye leseni ya kutoa huduma za mawasiliano, au mwakilishi wake, ana wajibu wa kutunza siri za mawasiliano binafsi na taarifa zozote za siri za wateja kwa mujibu wa sheria hii”

(2) “Mtu yeyote haruhusiwi kutoa taarifa binafsi za mteja yeyote alizopokea au kusikia kwa mujibu wa sheria hii isipokuwa tu mtu huyo ameruhusiwa kwa mujibu wa sheria”

Kifungu cha 123 (1) kinasema:-
Mtu yeyote ambae bila sababu za msingi atasababisha kuingilia au kuzuia kupokewa kwa mawasiliano yeyote ya kielektroniki anafanya kosa and akipatikana na makosa atatakiwa kulipa faini ya shilingi za kitanzania zisizopungua milioni tano au kwenda jela kwa muda wa usiopungua miaka miwili au adhabu zote kwa pamoja”

Kanuni ya 12 ya Kanuni za Mawasiliano za mwaka 2005 za Tanzania (Kulinda Wateja) inasema:-
“Mtoa huduma za Mawasiliano haruhusiwa kuingilia kati, kusikiliza au kutoa taarifa zozote za mazungumzo ya mteja yeyote yaliyopitia kwenye mtandao wa mtoa huduma, isipokuwa kwa ruhusa kulingana na mahitaji maalumu kwa mujibu wa sheria zilizopo”

Kutolewa kwa taarifa za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa simu za mkononi ni lazima kunafanywa na mtu mwenye ujuzi na uelewa wa jinsi ya kupata taarifa hizo na wenye ruhusa ya kufanya hivyo katika mtandao wa Kampuni husika ya kutoa huduma ya mawasiliano; ama peke yake au kwa kushirikiana na wenzake kwa kuingia kwenye mtandao kwa makusudi kwa lengo la kuingilia mawasiliano binafsi ya watu, ambayo ni uvunjaji na kinyume na matakwa ya kifungu cha 123 cha Sheria Na. 3 ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta.

Mamlaka ya Mawasiliano inayakumbusha Makampuni ya simu kuweka uzuizi na kuhakikisha siri za mazungumzo binafsi ya wateja zinahifadhiwa na hazitolewi kwa yeyote isipokuwa kwa mujibu wa sheria na; kuhakikisha yanafanya uchunguzi kugundua walioiningilia mazungumzo binafsi ya wateja.

Wananchi wanapewa tahadhari kuhusu kutafuta au kutaka kupata taarifa za mawasiliano ya siri kutoka kwa watoa huduma na kuzitumia taarifa hizo binafsi za mawasiliano pasipo kufuata utaratibu ulioruhusiwa kisheria.

Kwa taarifa ambazo zimechapishwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari hivi karibuni, Mamlaka ya Mawasiliano inafanya uchunguzi wa uvunjwaji huo wa sheria kwa kutoa taarifa binafsi za wateja kinyume na sheria. Baada ya kuwabaini wahusika, Mamlaka itachukua hatua za sheria kwa yeyote atakayebainika kuvunja sheria hiyo.


Imetolewa na

Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
22 Desemba 2010



mbn mmechelewa sana ngoja niwakumbushe kidogoView attachment POLE DK-ULIMBOKA.doc
 
Du hii kali naamini Mwanahalisi kweli ana ushahidi maridhawa, alikopatia habari za simu za kina Ulimboka lakini kwa kifupi si ametusaidia kumjua aliyemteka, na waliohusika. Isipokuwa safari hii anaweza okoka km ana vyeti vya MIREMBE km asemavyo Burn Karudi au aione nimtafutie maana Kesi imekaa vibaya na hile Kampuni la Simu
 
Duh..kama ni hivi mamlaka inakataza siri ya makubwa na ujambazi kuwa nje nje..sheria mbofu.ingeruhusu kampuni kutoa siri hizo uharamia ungepungua.
 
bila kuitaja chadema hulali wabunge 6 wa ccm wanahusishawa na hongo ya tanesco na yule aliyeshikwa na hongo ya milion moja chadema kama ni zito wanauwezo wa kumfukuza ccm mnaogopa sababu hakuna mbunge aliyeshinda bila rushwa watawawasha chama chote ubavu hamna haa haa haa
Kukusanya taarifa kupitia makampuni ya simu wala sio kazi ngumu ni rahisi sana ni kuwahonga tu watu wa IT hata Chadema wakati wa uchaguzi wa Bavicha walitumia hii mbinu kutoa taarifa za kina Habib kutumiana fedha kwa M-Pesa.
 
​ha ha ha mwigulu alipodanganya ulifurahi sana ccm ni chuo cha mafisadi na wazandiki wa nchi hii
Smile,
Sheria inakataza kuingilia privacy huwezi kunianika kwenye gazeti lako mfano Ritz mwenye namba za simu 0244 888777 ni mtuhumiwa wa pili alihishiwa salio saa 9 usiku.
 
na bado mambo mengi yatafichuka uchu wa madaraka ndani ccm utasaidia sana chadema hamkai kama kitu kimija kila mtu na lake tutaona mengi b4 2014 tutavuna majimbo mengi mungu wetu yuko upande wetu
Mkuu kwa hiyo wewe ndio msemaji wa Mwanahalisi...nadhani hujui kwa nini Mwanahalisi limefungia na serikali...pitia upya taarifa ya serikali utakutana na kifungu cha 30 cha katiba, kinachoweka ukomo wa uhuru wa habari.
 
​ccm mtaumbuka sana mkianza hilo mtasema mlivyomtuma shibuda na akakwaa kisiki chadema kuna vichwa sio nyio hamna sera ni vitisho na matusi lusinde type mtafika wapi na watu hao ndio mnayoita ccm kwi kwi kwi
Safi sana Mwanahalisi mshitakiwa wa kwanza ataieleza mahakama alipataje siri za wateja wa TiG0.
 
Mkuu nimekusoam Uzuri hata hivyo siku hizi umekuwa adimu sana, hambu mghoshi msimu wa mapeasi bado!!! Mitandao itawatesa sana
mkuu itabidi kila ukipewa like na wewe unagonga ili ziende sambamba, teh teh!
:focus: kama wataweza kufunga na mitandao ya kijamii basi hapo ndo watakuwa wame'win kutufunga mdomo na kutuweka gizani./
 
Mkuu nimekusoam Uzuri hata hivyo siku hizi umekuwa adimu sana, hambu mghoshi msimu wa mapeasi bado!!! Mitandao itawatesa sana
hehhehehe, ekadu mghoshi, ntazenga, du ukiona mntu mweonda fundi ya kuzenga nionda mghoshi, imi mfundi yedi sana ya kuzenga.
 

KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAI
Hivi karibuni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imegundua kuzuka kwa tabiaya uvunjaji wa kanuni ya utunzaji wa siri za mawasiliano binafsi ya watumiajiwa huduma za mawasiliano ya simu za mkononi. Mawasiliano hayo yamefikia hatuaya kuchapishwa katika vyombo vya habari.

Mamlaka ya Mawasiliano inapenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wenye makampuniya Simu na wananchi kwa ujumla kuwa, kutoa taarifa za mawasiliano binafsi yasimu bainA ya watumiaji wa huduma hiyo, ni uvunjaji wa Sheria ya Mawasiliano yaKielektroniki na Posta Na. 3 ya mwaka 2010 na Kanuni za Mawasiliano (KulindaWateja) za mwaka 2005.

Kifungu cha 98 ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kinasema;

(1) “Mtu yeyote ambaye ni mfanyakazi wa kampuni yenye leseni ya kutoa huduma zamawasiliano, au mwakilishi wake, ana wajibu wa kutunza siri za mawasilianobinafsi na taarifa zozote za siri za wateja kwa mujibu wa sheria hii”

(2) “Mtu yeyote haruhusiwi kutoa taarifa binafsi za mteja yeyote alizopokea aukusikia kwa mujibu wa sheria hii isipokuwa tu mtu huyo ameruhusiwa kwa mujibu washeria”

Kifungu cha 123 (1) kinasema:-

Mtu yeyote ambae bila sababu za msingi atasababisha kuingilia au kuzuiakupokewa kwa mawasiliano yeyote ya kielektroniki anafanya kosa and akipatikanana makosa atatakiwa kulipa faini ya shilingi za kitanzania zisizopungua milionitano au kwenda jela kwa muda wa usiopungua miaka miwili au adhabu zote kwapamoja”

Kanuni ya 12 ya Kanuni za Mawasiliano za mwaka 2005 za Tanzania (KulindaWateja) inasema:-

“Mtoa huduma za Mawasiliano haruhusiwa kuingilia kati, kusikiliza au kutoataarifa zozote za mazungumzo ya mteja yeyote yaliyopitia kwenye mtandao wa mtoahuduma, isipokuwa kwa ruhusa kulingana na mahitaji maalumu kwa mujibu wa sheriazilizopo”

Kutolewa kwa taarifa za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa simu za mkononi nilazima kunafanywa na mtu mwenye ujuzi na uelewa wa jinsi ya kupata taarifa hizona wenye ruhusa ya kufanya hivyo katika mtandao wa Kampuni husika ya kutoahuduma ya mawasiliano; ama peke yake au kwa kushirikiana na wenzake kwa kuingiakwenye mtandao kwa makusudi kwa lengo la kuingilia mawasiliano binafsi ya watu,ambayo ni uvunjaji na kinyume na matakwa ya kifungu cha 123 cha Sheria Na. 3 yaMawasiliano ya Kielektroniki na Posta.

Mamlaka ya Mawasiliano inayakumbusha Makampuni ya simu kuweka uzuizi nakuhakikisha siri za mazungumzo binafsi ya wateja zinahifadhiwa na hazitolewikwa yeyote isipokuwa kwa mujibu wa sheria na; kuhakikisha yanafanya uchunguzikugundua walioiningilia mazungumzo binafsi ya wateja.

Wananchi wanapewa tahadhari kuhusu kutafuta au kutaka kupata taarifa zamawasiliano ya siri kutoka kwa watoa huduma na kuzitumia taarifa hizo binafsiza mawasiliano pasipo kufuata utaratibu ulioruhusiwa kisheria.

Kwa taarifa ambazo zimechapishwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari hivikaribuni, Mamlaka ya Mawasiliano inafanya uchunguzi wa uvunjwaji huo wa sheriakwa kutoa taarifa binafsi za wateja kinyume na sheria. Baada ya kuwabainiwahusika, Mamlaka itachukua hatua za sheria kwa yeyote atakayebainika kuvunjasheria hiyo.



 
Back
Top Bottom