TCRA angalieni sms za Biko, Tatu mzuka, Moja bet

Mkuu mm nilishawahi kuwapigia (***) nikawaambia sihitaji kutumiwa jumbe za matangazo ambazo hazihusian na kampun yao.. hadi leo hii sijaziona tena
 
Ningependa kuwakilisha kero inayo nikumba mimi pia hata watu wengi tu.

Haya makampuni ya michezo ya bahati nasibu kutuma SMS kila wakati pasipo option ya Usubscribe.

Mimi nimecheza mara moja tu, sasa kwann kila siku asubuhi, mchana, usiku mnanitumia SMS zenu..... kwani nimeji subsribe for news & updates?????.... hizi message zinaboa kweli kweli pia ni usumbufu kabisa.

Tena sikuhizi hadi wanakutaja jina kabisa.

OMBI KWA TCRA
wekeni mikakati ambayo hawa makampuni waweke namba ya kutuma neno ONDOA ili waweze kujitoa na SMS za kinafiki

Pia kwann wamtumia SMS pasipo makubariano baina ya mteja???

Naimani maofisa wa tcra mmeliona hili... nawatakia utekelezaji mwema.

Nawakilisha tu maoni yangu.
 
Alafu wanakutamanisha kucheza michezo yao kwakukushawishi utashinda mil70, 60,50. Ukicheza unaambulia buku na ndio basi tena mpuno kwa kwenda mbele
 
Binafsi mimi kwa upande wangu naona tatizo maana ile umetulia unasikia SMS imeingia unadhani mtu wa maana kumbe Moja Bet, sijui Mkeka, Sportpesa, Tatu mzuka, Biko Sports, Biko na makampuni mengine hukoo.

Kibaya zaidi wanakutumia SMS kila wakati yaani wananikera kweli!

TCRA pigeni marufuku na hawa wezi waache kututumia miSMS yao ya ushawishi..

Nawasilisha..
 
Mbaya zaidi SMS nyingine ni za michezo ya kamari ambayo ni kharamu kiimani. Yani hawa TCRA sijui hata wanawajibika na vitu gani maana hata kusimamia sheria ya ving'amuzi kuhusu local channels wameshindwa sasa sijui mpaka Magu au Majaliwa waingilie kati? Wakitumbuliwa watalalamika.
 
Hili ni tatizo. Wanatumia information zetu kujipatia kipato. Line hawatupi bure, na huduma zote tunalipia, sasa kwanini watukere na matangazo?
 
Yani mimi wananikera na kunihalibia concentration..
Unakuta mtu unasubiri txt ya muhimu ukisikia text imeingia unaangalia kwa shauku unakuta ni wapuuzi wa biko..

Kwanza wanatulazimisha kutangaza bidhaa zao bila ridhaa yetu...huu ni ujambazi
 
Back
Top Bottom