Nadhani nina kila sababu ya kuishitaki mitandao ya simu inayonihudumia kwa usumbufu ninao upata kila baada ya dakika kadhaa kwa sms za kamari na matap

Kudo

JF-Expert Member
Nov 2, 2017
1,809
6,081
Mods naomba msiunganishe uzi huu mana na nyie mmekuwa kama mnahusika na mitandao kila tukiweka uzi wa aina hii mnafuta au kaunganisha na nyuzi za miaka sita nyuma.

Kiukweli upande wangu imegeuka kuwa kero kuwa mtumiaji wa mitandao hii ya simu.
Si voda;airtel;Halotel ama Tigo yote hali ni moja.


Kwa usumbufu ninaopata nimelazimika kuweka simu yangu silent ila nikiigusa lazima nikutane na sms zaidi ya kumi kutoka kampuni za kuchezesha kamari.

Yani Boompesa;Instamoja;Biko;Bikosports;Tatumzuka;supatano;sportpesa;Sokabet;Mkekabet;15577(muito);PesaniMpesa; Tigoapp;vodataarifa; Matapeli; mganga kutoka sumbawanga; Polisi(japo hii ni muhimu kwa sasa ila mara mbili au moja kwa mwezi sio kila siku na kila dakika kadhaa);Tigobima.....

Yani imekuwa ni bandika bndua kiasi kwamba naona simu imegeuka kuwa kero kwangu japo ni muhimu katika kizazi cha sasa.

Hebu fikiria unangojea simu ya muhimu mara inakupigia hii namba 2259... Inakutangazia miito ya simu.

Ama unasubiri text ya muhimu (hasa watongozaji) unajua umejibiwa kumbe ni Biko...

Kiukweli naona upande wangu kuna haja ya mimi kufika mbele ya vyombo vya Sharia kuishitaki mitandao hii hasa kwa kugawa namba zangu bila ridhaa yangu kwa kampuni zote hizo na pia inaniondolea usalama wa matumizi ya simu yangu.

Kwa nini nimeandika?

Jana nilisajili laini ya simu yani natoka tu kwa wakala zinaingia sms kama tano hivi, tatu kutoka kwa matapeli na mbili za BIKO.

Nilijiuliza inawezekanaje hii kitu yani hata vocha sijaweka tayar wanaanza kutuma je wahusika ni wafanyakazi ama?
vodacom na mitandao mingine mnakila sababu ya kuwajibishwa hapa
 
Mimi nimeamua ku mute inbox yangu. Na nimeandika kabisa whatsup kama ukinihtaji ni bora unipigie kuliko ku txt sms za kawaida. Maana nazisomaga siku mbili zijazo. Na hapo na kutana na sms zaid ya 12 za dakapesa.


Kama hapa sms 245 zote za dakapesa. Hizo unread 58 ni zakijinga. Nime mute sms zoteeeee atakaenitumia sms namjibu siku mbili baadae au nijikute tu nina muda wakucheki huko kama kuna chochote.
Screenshot_20190126-143720.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie niliacha kusoma Hadithi/ riwaya zitokazo kwenye magazeti kwani kila ifikiapo patamu waambiwa"itaendelea wiki ijayo" Tamthilia kwenye Tv zikanishinda kwa biashara hiyo hiyo ya "don't miss next episode tomorrow" Tigo ilinishinda baada ya ukiweka vocha hongera utafikiri umechangia mchango muhimu Msikitini/ Kanisani. Usiombe bando au vocha ikafikia kikomo! Utandhani umekopa Brac/Tala! Mara piga no hii kusikiliza nyimbo. Kwa ufupi sipendi kitu kinachonigharimu hela yangu kuwa kero. Ila kwenye zama hizi najifunza kuwa na hekima ya uvumilivu kwa haya yaendeleayo kwenye mitandao hii. Darofa,Instamoja,Tatu mzuka/kinyamkera, Biko, spot pesa nahizi za Shemeji yule mganga aliyerekebisha ndoa na kazi yangu zimekuwa zikinifanya nitamani kuzima simu wakati flan! TCRA tafadhal, sio kila mtu ni mlevi wa kamari, kwa nini wasilipie bilboards barabarani watangaze huo upuuzi wao badala ya kututumia direct kwenye sim zetu? Natamani niwatukane ila watoto bado wadogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nimeamua ku mute inbox yangu. Na nimeandika kabisa whatsup kama ukinihtaji ni bora unipigie kuliko ku txt sms za kawaida. Maana nazisomaga siku mbili zijazo. Na hapo na kutana na sms zaid ya 12 za dakapesa.


Kama hapa sms 245 zote za dakapesa. Hizo unread 58 ni zakijinga. Nime mute sms zoteeeee atakaenitumia sms namjibu siku mbili baadae au nijikute tu nina muda wakucheki huko kama kuna chochote.View attachment 1005373

Sent using Jamii Forums mobile app
Kinachokera zaidi yani hata kampuni ikianza leo tayar wananamba yako yani ahsubuh hadi jioni unakuta umepokea zaidi ya sms 50 za kipuuzi tu
 
Back
Top Bottom