Shirika la viwango Tanzania TBS limetahadharisha Watanzania kuhusu uwepo wa Condom bandia zilizozagaa kwenye maduka ya dawa ziitwazo MELT ME zilizotengenezwa India. Mara ya kwanza zilikamatwa bandarini Dar es salaam kwa kosa la kutokaguliwa katika nchi zilizotoka mapema August ambapo mamlaka hiyo iliagiza zirudishwe India. Kaimu Mkurugenzi wa TBS Leandri Kinabo amesema bidhaa hizo zimepimwa na kufeli vipimo vitatu vya kuthibitisha ubora wa bidhaa hapa Tanzania ambapo TBS imeanza mipango ya kuzisaka hizo Condom kwenye maduka mbalimbali ya dawa.
source ni millard ayo.
maoni yangu,je ni watu wangap washazitumia izo condom feki,je maisha ya raia si yako hatiani kutokana na uzembe au rushwa unaofanywa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.