Kontena lililosheheni kondomu za kiume aina ya Melt Me zenye thamani ya sh222.1 kutoka nchini India zimekamatwa na kuzuiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam, baada ya kubainika kuwa hazifai kwa matumizi ya binadamu.
Maofisa wa TBS wamelazimika kufanya msako mkali kwenye baadhi ya maduka ya dawa jijini Dar es Salaam baada ya kubainika kwamba tayari kondomu hizo zipo sokoni.
"Imebainika kwamba tayari nyingine ziko madukani, mbali na zile zilizokamatwa' kumbe kuna shehena nyingine imeingizwa nchini kwa njia ya panya. Kaimu Mkurugezi wa Mkuu wa TBS Leandri Kinabo amewataka wananchi kuwa makini, kwani kondomu hizo ni mbovu, zimebainika kuwa na vitundu, pia zinapasuka haraka. TBS bado wanaendelea kufanya mawasiliano na kampuni iliyotengeneza kondomu hizo. Lakini kwenye kasha lake inaonyesha kuwa inaingizwa nchini na kampuni ya Fair Deal Exim ya Dar es Salaam.
Chanzo cha Habari: Gazeti la Mwananchi Jumamosi 22, Desemba 2012.