Hawa wabunge nao wamezidi sasa taarifa ya ugunduzi umetoka kwa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali wao wanasema wamegundua
Deo Filikunjombe Haule, Makamu Mwenyekiti
Hesabu za Mashrika ya Umma
Madudu ndani ya mashirika ya umma yamezidi kuibuka ambapo jana Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (POC), ilibaini kuwa Shirika la Viwango nchini (TBS), limedanganya taifa kwa kutumia makampuni hewa ya kukagua magari nje nchi.Utapeli huo ulibainika baada ya timu ya wabunge kufanya ziara katika nchi za Singapore, China na Japan kwa ajili ya kutembelea makampuni yanayoelezwa na TBS kwamba yanahusika na ukaguzi wa magari kabla ya hayajaingia hapa nchini. Hata hivyo, wabunge hao walijionea vituko baada ya kufika huko nje ya nchi ambapo walibaini hapakuwa na kampuni wala ofisi yoyote inayofanya kazi hiyo ya ukaguzi wa magari.
Mmoja wa wabunge hao, Deo Filikunjombe, alisema jana kuwa baada ya kufika walipata aibu mpaka wakafikia hatua ya kukimbilia ofisi za Ubalozi a Tanzania zilizopo katika nchi hizo kwa ajili ya kujihifadhi. "Huko nje, hakuna ofisi, makampuni wala ofisi ambazo zimekuwa zikidaiwa na TBS zipo huko kwa ajili ya kukagua magari kabla hayajaingia nchini ili kujua ubora wake," alisema Filkunjombe.
Kutokana na utapeli huo kuwa mkubwa, Kamati imemuandikia barua Spika wa Bunge, Anne Makinda, kutaka suala hilo litinge bungeni likajadiliwe na wabunge wote. Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa POC, John Cheyo, alisema licha ya wabunge kukosa ofisi za makampuni hayo huko nje ya nchi, lakini pia hakuna mchanganuo wa fedha zilizopatikana kutokana na ukaguzi huo wa magari nje ya nchi.
Alisema TBS kwa miaka 10 mfululizo imekuwa ikifanya vibaya katika mahesabu yake na kueleza kuwa hakuna shirika bovu la serikali kama hilo hapa nchini.
Imedaiwa kuwa baadhi ya wabunge waliokwenda nje ya nchi kuangalia makampuni hayo walitaka kumpiga ngumi, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Charles Ekelege, ambaye aliwaongoza baada ya kubaini kwamba walikuwa wanatapeliwa. Kamati za Bunge za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na ile ya Hesabu za Serikali (POC), jana zilisema ukaguzi wa magari unaingiza fedha nyingi lakini TBS imeshindwa kueleza mahali zilipo wala mchanganuo wake.
"Huko nje ya nchi hatukukuta ofisi wala wakala wa ukaguzi wa magari baada ya kufanya ziara nje ya nchi, alisisitiza Makamu Mwenyekiti wa POAC, Filikunjombe. Wabunge hao ambao ni wajumbe wa Kamati hizo, walisema kutokana na utendaji mbovu wa TBS, kwa sasa haijulikani magari mangapi yanayokaguliwa ubora wake kabla ya kuingia nchini na ukaguzi huo unaingiza kiasi gani cha fedha. Kutokana na utata huo, kamati hizo zimeitaka Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na TBS wiki ijayo kufika mjini Dodoma ili kutoa maelezo ya kina.
Hawa wabunge nao wamezidi sasa taarifa ya ugunduzi umetoka kwa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali wao wanasema wamegundua
Mwisho wa haya madudu kwa taifa letu ni lini?
Mkombozi wa watanzania hajazaliwa?
Yaani jitihada zote hizo zinazofanywa na waheshimiwa wabunge kuthibiti matumizi mabovu ya pesa za walipa kodi hawa watumishi wa umma ndio wanaspeed up? Inatisha@
Huyo mkurugenzi alipohojiwa na waandishi wa habari jana TBC1 alogoma kutoa majibu hadi jumatatu. Swali la msingi mpaka yote haya yanafanyika miaka kwa miaka watu wa TISS wako wapi jamani. Bila ya shaka hii ni dili ya mafisadi. Kweli watanzania ni watu wajinga sana duniani na kwa mtindo huu katu hatutapata heshima duniani zaidi ya ujinga.
Huyo mkurugenzi alipohojiwa na waandishi wa habari jana TBC1 alogoma kutoa majibu hadi jumatatu. Swali la msingi mpaka yote haya yanafanyika miaka kwa miaka watu wa TISS wako wapi jamani. Bila ya shaka hii ni dili ya mafisadi. Kweli watanzania ni watu wajinga sana duniani na kwa mtindo huu katu hatutapata heshima duniani zaidi ya ujinga.
Ngoja nipate supu, halafu nitarudi hapa. TBS ni kero kero kerooooo.... kero.