kagumyamuheto
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 286
- 3
kibano kinaanza
TBC inazidi kupoteza mwelekeo kwa kurudia rudia hii docomentari yao
ungeangalia ili uwajue wali ua na ndicho nilichofaidi kwamba sasa hivi ni kutanao nitajua nani aliua ndugu zetu.....kwani kabla ya hapo mimi nilikuwa najidanganya eti wale wanafunzi wa ccp kumbe ni hawa tunao ishi nao.....asante tbc1Kama ni hivyo afadhali sikuangalia
Sijaona hata kipigo cha maana, hawa jamaa walikuwa na nafasi ya kuuwa hata mia, natamani IGP angekuwa Omar Mahita saa hizi tungekuwa tunaongelea maiti zaidi ya mia.
Du!Ndugu wana JF, tangu jana kuna tangazo linaoneshwa TBC1 kuhusu vurugu za Arusha lakini linakera kwa sababu linapendelea upande mmoja wa polisi na kufanya Watanzania waamini maandamano ya Chadema yalikuwa na lengo la kwenda kuvamia kituo cha polisi na kupora silaha.
Huo ndio ujumbe nilioupata kutoka kwa ‘commentator' wa tangazo hilo na naona haliwatendei haki Watanzania. Chanzo cha vurugu za Arusha zinafahamika ni uchaguzi tata wa meya Arusha. Kwa nini sasa waliotengeneza tangazo hilo hawaoneshi tangu A hadi Z na wanaonesha Z tu? Wanataka Watanzania waamini nini?
Kama habari za kiintelegensia ni za kweli mbona hatujasikia hao walikuwa wamepanga kufanya uvunjifu wa amani wakati wa maaandamano wamekatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria na badala yake walikamatwa tu viongozi wa maandamo?
Nionanvyo mimi, tangazo hilo, ambalo linaonesha limetoka Idara ya Habari (Maelezo), linahalalisha polisi polisi kupiga waandamanani na kuua baadhi ya wananchi. Ila najiuliza kwa nini baadhi ya matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na polisi haukuoneshwa kama vile kuna watu walidai waliporwa simu na polisi, lakini sehemu hiyo haioneshwa?
Pia, kuna polisi walionekana wakishambulia gari moja jekundu hivi wakitumia virungu vyao kuvunja vioo vya gari hilo na tukio hilo halioneshwi wakati kwenye runinga zingine tuliona polisi wakivunja vioo vya hilo gari na hata pengine kumjeruhi dereva wake. Hilo gari, kwa mfano, lilikosa nini hadi livunjwe vioo? Ndiyo ulinzi wa raia na mali zao?
Hata kama polisi waliona kuna haja ya kutumia silaha ni lazima mpaka waue? Kama nia ni kufikiri Watanzania ni wajinga na wanaweza kurubuniwa, muda huo umekwisha. Watanzania siyo wajinga kiasi hicho (ingawa wengine ni wajinga ndiyo). Wana uwezo wa kusoma kilicho nyuma ya pazia na kujua ukweli na ukweli haugeuki. Mojawapo ya ‘attributes' za ukweli ni ‘immutability'. Hivyo, ni kupoteza muda kuwapotosha Watanzania na kujenga dhana kwamba polisi ndio wanaotoa haki za raia kuandamana na kwamba wakitoa tamko basi ni amri halali hata kama kufanya hivyo wanavunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (kama inavyobadilishwa mara kwa mara) na kubaka demokrasia.
Nimeicheki mwishomwisho,yaani ni full propaganda.Muda wote wanakazania eti viongozi waliwahamasisha wafuasi wao kwenda kuvamia kituo cha polisi.Lengo lao(serikali)kubwa ni kuuchochea umma waichukie CDM....pumbaf kabisa!
Bahati nzuri viongozi wa Chadema pia wamepewa nafasi ya kusikika, sehemu ya hotuba za Ndesambulo, Dr. Slaa na yule mwenzao yamesikika vizuri.
Tanzania hii ya sasa si ya mabwege tena. Watu wanajua kuchambua pumba na mchele. Few stupids will buy the story. Hiki si kipindi cha kueneza propaganda ambazo hazijengi nchi ila zinaendelea kutuletea umaskini kwa kukutetea maslahi ya wachache. Mbaya sana polisi kujiingiza kwenye siasa