HPAUL
JF-Expert Member
- Jan 18, 2011
- 410
- 567
Baada ya kuangalia tarifa ya habari Leo saa mbli ya TBC sasa ni dhahiri kabisa inaelekea kule lilipo gazeti la Uhuru, Nina maana ya kutokuwa na wateja kabisa. Najua wote mnaelewa Kuwa gazeti la Uhuru sasa hivi haliuziki kabisa labda chembe ya mauzo wanayopata ni taasisi za serikali. mawakala, wauzaji rejareja na wasafirishaji hawataki hata kuyaona. Reporting ya Leo ya TBC katika taarifa ya habari inayoendelea sasa hivi na hata wakati wanahitimisha live ufunguzi wa bunge maalum la katiba ni dhahiri inaelekea kule kule iliko fia gazeti la Uhuru kwa sababu zilezile za biased reporting. Waliohojiwa kwa comments ya Kikwete speech wote ni wabunge wa CCM. Sio Siri kwamba kwa kizazi cha sasa hivi zaidi ya 80% watazamaji, wasikilizaji na wasomaji ni Watu wanaopenda habari za mageuzi na sio mawazo mgando ya CCM. Kwaheri TBC na sasa mtegemee ruzuku tu.