Majala Kimolo
JF-Expert Member
- Aug 3, 2007
- 342
- 39
Kuna ukweli ndani yake. Sitarajii makubwa kutoka kwao hasa ukizingatia kuwa watangazaji na waandaa habari wameshatiiza malengo yao (kuwajiriwa na TBC) Nafikiri kuna haja ya kubadili mfumo. Nakumbuka zamani watangazaji walikuwa makini licha ya teknolojia duni, sijui wakati huu kuna nini? Kuna haja basi ya kuwawajibisha wahariri ili kuboresha matangazo yao.Tatizo hilo la kweli, makosa huanzia kwa waandishi na kama wahariri hawakupitia vizuri taarifa hiyo basi ndo hayo uliyoyaona yanajitokeza.
Tatizo la taarifa ya Rais wa Brazil kuwasili nchini na wakati huohuo kuwa atapokelewa na Rais Kibaki ni la Mpangilio ambayo wa kulaumiwa ni mhariri aliyepanga na si mtangazaji kwasababu yeye analetewa labda alichopaswa kufanya ni kurekebishia hewana kama naye alipitia kabla ya kuingia studio.
Jambo la Msingi hapa kinachoonekana pale waandishi wa TBC wanajiona wako juu ya wenzao wa vyombo vingine kwahiyo wanasahau mambo ya msingi kikazi hadi taarifa ya habari wanasoma kama vile Clause FM wanavyofanya, hawajui kuwa ile ni chombo cha Taifa. Zamani RTD ilikuwa inaajiri waliofunzwa pale lakini siku hizi kujuana bwana, mtu analeta kijana wake aajiriwe, wanasiasa nao wasumbufu nasikia ikitanagzwa ajira wanapeleka watoto na vimemo hata wasipokuwa na uwezo wataajiriwa.
Naomba kuwasilisha wana jamii.
jambo jingine linalonikera ni upendeleo wa wazi wa baadhi ya watangazaji kama huyu Mr Upara katika kipindi cha asubuhi akiwa na wawakilishi wa vyama vya siasa, kwake sisiem ndo kama mungu wake au mbwa mbele ya chatu kazi yake ni kusaidia kujenga hoja na kuponda maelezo ya wanasiasa wa vyama vingine. TBC lazima irejeshe heshima yake la sivyo itakuwa sawa na gazeti la uhuru
Nawasilisha