Tunataka Kipimo gani kingine cha Kututhibitishia kuwa hii Kero ya Kukatika hovyo Umeme nchini ni Hujuma ya Kimakusudi na ya Kimkakati kwa Rais Samia?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,646
109,031
Wiki Mbili tu zilizopita Mmoja wa Maafisa wa Juu wa TANESCO akizungumza na Waandishi wa Habari wa U-FM ( Uhai FM ) alisema kuwa Mabwawa yote ya Kufua Umeme ya Mtera, Kidatu na Kihansi yamejaa kutokana na Mvua nyingi Kunyesha katika Mikoa Minne ya Mbeya, Iringa, Tabora na Singida inayojaza Mabwawa haya tajwa.

Katika hali ya Kushangaza kabisa na iliyonisikitisha GENTAMYCINE leo Asubuhi katika Kipindi cha Nipashe cha Radio One Mtendaji wa TANESCO Feleschi Mramba bila hata Aibu au kujua kuwa anadanganya na kutudhihirishia ni kwanini ni wa hovyo hovyo Kiutendaji na kwamba hata Kuhamishwahamishwa Kwake katika Nyadhifa kunamaanisha si Mweledi na Mahiri alisema kuwa pamoja na Mvua Kunyesha nyingi nchini Tanzania, ila bado hazijaweza Kujaza Mabwawa muhimu tajwa hapo juu ya Kufua Umeme ya Mtera, Kidatu na Kihansi.

Rais Samia endelea tu kuwa Mpole ila nikuhakikishie kuwa kwa 99.9% UNAHUJUMIWA na Watendaji wako unaowaamini na nisikufiche huku Mitaani ambako ndiko Maisha yangu ya Kiuwajibikaji na Kimajukumu yako Wananchi HAWAKUPENDI, WANAKUCHUKIA na wanauliza 2025 kwanini inachelewa kufika ili UONDOKE na UWAACHIE wale wenye Uwezo wa Kutuongoza Watanzania na Kuiongoza vyema Tanzania yetu.
 
Wiki Mbili tu zilizopita Mmoja wa Maafisa wa Juu wa TANESCO akizungumza na Waandishi wa Habari wa U-FM ( Uhai FM ) alisema kuwa Mabwawa yote ya Kufua Umeme ya Mtera, Kidatu na Kihansi yamejaa kutokana na Mvua nyingi Kunyesha katika Mikoa Minne ya Mbeya, Iringa, Tabora na Singida inayojaza Mabwawa haya tajwa.

Katika hali ya Kushangaza kabisa na iliyonisikitisha GENTAMYCINE leo Asubuhi katika Kipindi cha Nipashe cha Radio One Mtendaji wa TANESCO Feleschi Mramba bila hata Aibu au kujua kuwa anadanganya na kutudhihirishia ni kwanini ni wa hovyo hovyo Kiutendaji na kwamba hata Kuhamishwahamishwa Kwake katika Nyadhifa kunamaanisha si Mweledi na Mahiri alisema kuwa pamoja na Mvua Kunyesha nyingi nchini Tanzania, ila bado hazijaweza Kujaza Mabwawa muhimu tajwa hapo juu ya Kufua Umeme ya Mtera, Kidatu na Kihansi.

Rais Samia endelea tu kuwa Mpole ila nikuhakikishie kuwa kwa 99.9% UNAHUJUMIWA na Watendaji wako unaowaamini na nisikufiche huku Mitaani ambako ndiko Maisha yangu ya Kiuwajibikaji na Kimajukumu yako Wananchi HAWAKUPENDI, WANAKUCHUKIA na wanauliza 2025 kwanini inachelewa kufika ili UONDOKE na UWAACHIE wale wenye Uwezo wa Kutuongoza Watanzania na Kuiongoza vyema Tanzania yetu.
Mama ndiye aliyetuhujumu watanzania kwa kuwatoa welevu waliofanikisha kutibu tatizo la umeme na kuwaleta wapigaji.
Mama asitetewe kwa hili.
Lengo lake limetimia
 
Watanzania tujitahidi tuchague mtu yeyote yule awe Rais isipokuwa hawa watu, January Makamba, Ridhiwani Kikwete, Mwigulu Nchemba na Nape Nnauye ambao najua mwaka 2025 lazima mmoja wao hapo atagombea hiko kiti, mipango yote ya kumhujumu mama ni ili kumsafishia njia mmoja kati ya hao niliowataja na endapo tutamchagua basi tutakuwa wapumbavu wa mwisho
 
Mama ndiye aliyetuhujumu watanzania kwa kuwatoa welevu waliofanikisha kutibu tatizo la umeme na kuwaleta wapigaji.
Mama asitetewe kwa hili.
Lengo lake limetimia
Absolutely I agree with you 100% Chief.
 
Umeme unaozalishwa bongo ni mdogo wakati mahitaji yanazidi kuongezeka hili ndo tatizo. Hata waziri awe nani au bodi ngapi zivunjwe bila vyanzo vipya vya kufufua umeme changamoto ipo pale pale ndo maana Jiwe aliwekeza sana kujenga JNHPP, kama angekuwepo labda ingekua imekamilika. Wanazunguka tu mbuyu hao wanasiHasa
 
Back
Top Bottom