Chikaka Sumuni
JF-Expert Member
- May 16, 2013
- 1,337
- 773
TBCCM ni janga la Taifa, Mwakani CCM ikibwagwa wafanyakazi wote wafungashe virago tu. Ifungwe kwa muda wakati watawala wapya wanapanga safu zao. Halafu ndipo wakabidhi mitambo na ofisi na baadaye watafutwe wafanyakazi wapya wa kuendeleza gurudumu la maendeleo.
Inasikitisha sana !!!
Jana niliangalia habari na mwishoni wakasema nje ya bunge wabunge pia walipata nafasi ya kuelezea maoni yao lakini wakachukua maoni ya wajumbe wa ccm tu»»» jambo la ajabu
Wao ni kuegemea upande moja tu wala hawajui kubalance habari huku wanajiita "ukweli na uhakika"
samahani kwani ukawa hawana tv station???!.
hawana!
Mimi huwa najiuliza laini nashindwa kupata jibu: hivi watangazaji wote wa TBCCM ni makada wa CCM au wanajilazimisha tu kutekeleza matakwa ya CCM ili mradi mkono uende kinywani?
Basi wafungue tv station mbona gazeti wameanzisha? Hata radio basi mbona ladyjaydee amefungua? Chadema watashindwa vipi? Japo gazeti lao news zao ni negative tu hakuna postive kama wenyekiti wamejihuzuru nk.
mimimsiangaliagi ,imetokea wiki hii nipo safarini nikajikuta nilipo ni TBCMM pekee ndo ipo hewani ,aisee nimeogopa jamaa wamefungwa gavan ,sijui kama mtu mwenye akili kubwa kama anaweza kuvummila ujinga ule ....mh! siku ya ukombozi lazima watu wengine tuwan'oe hata nywele tuMkuu, Laiti tu wangekusikiliza. Lakini wanasema; Sikio la kufa halisikii dawa. Hao wabunge wawili ni mwiba kwa ccm
Jaman hivi hakuna sheria au NGO au watetezi wahaki za raia ambao wanaweza kufungua kesi ya wananchi dhidi ya TBC kuwaomba. mahakama iwalazimishe TBC kubalance taarifa zao?Katika kipindi cha redio cha Leo Katika Bunge ambacho katika bunge hili maalumu la katiba kinaitwa Katiba Tuitakayo, kinachorekodiwa na kurushwa na TBCCM kuanzia saa 3:00 hadi saa 4:00 usiku, mtangazaji wa TBCCM anayerekodi kipindi hiki kutoka bungeni Dodoma ameacha kwa makusudi kabisa kurekodi michango iliyotolewa na Juma Duni Haji, pamoja na Eng. Habibu Mnyaa waliotoa maoni ya kundi la watu wachache! Lakini maoni yote yaliyotolewa na wabunge wa CCM, hata kama ya kipuuzi, yamepewa airtime ya kutosha.
Haya ni makusudi kabisa yanayofanywa na chombo hiki kilichopo chini ya CCM ambacho huendeshwa kwa kodi za wananchi. Wanalenga kuwanyima wananchi habari sahihi juu ya watetezi wa maoni yao waliyoyatoa kwenye rasimu ya katiba hii inayojadiliwa. Inaonekana ripota wa kipindi hiki amepewa maelekezo maalumu na CCM kuhusu michango ya wabunge anyopaswa kuirekodi na kuirusha hewani, lengo likiwa kuwapumbaza na kuwahadaa wananchi juu ya usaliti unaofanywa na wabunge wa CCM katika kusigina maoni ya wananchi yaliyomo kwenye rasimu ya katiba.
Haiingii akilini kuona kwamba CCM wanafanya makusudi kuwanyima wananchi habari na kuwaacha wabakie mbumbumbu ili waendelee kuwatawala, kuwakandamiza, kuwanyonya na kuwamasikinisha. Raia wanakosa huduma muhimu za kijamii kama vile huduma za afya, shule, maji, barabara, nk kwa kisingizio kwamba hakuna fedha, kumbe fedha zinatumika kuendesha kituo cha redio ambacho hakina manufaa yoyote kwa wananchi. Ni bora vituo vya redio na tv vya TBCCM Taifa na TBCCM1 vifungwe kwani havina faida yoyote kwa wananchi.
:yield:
View attachment 150744 View attachment 150745 View attachment 150746
View attachment 150747 View attachment 150748 View attachment 150749
View attachment 150750 View attachment 150751 View attachment 150752
Mimi huwa najiuliza laini nashindwa kupata jibu: hivi watangazaji wote wa TBCCM ni makada wa CCM au wanajilazimisha tu kutekeleza matakwa ya CCM ili mradi mkono uende kinywani?[/QUOTE
Wameolewa mkuu kama wabunge wa ccm walivyo olewa!
Nadhani unajua wabunge wa ccm wameolewa ndio maana wamezuiwa kupiga kura za siri wanafuata mashariti ya bwana zao kwa maana nyingene sheria ya ushoga ccm hawawezi kuipinga coz.........
Jaman hivi hakuna sheria au NGO au watetezi wahaki za raia ambao wanaweza kufungua kesi ya wananchi dhidi ya TBC kuwaomba. mahakama iwalazimishe TBC kubalance taarifa zao?
Mnajidai haimtazami TBC lakini utafiti unaonyesha nyie ndio watazamaji wakuu, kila mara mnakuja na malalamiko yasiyo na kichwa wa mguu humu!