Nimesoma mawazo ya watu tofauti kuhusu ubaguzi wa TBC anaouzungumzia Markach japo naye hakuweka wazi habari ipi haikutangazwa. Unajua siku zote ukikaa kulalamika kama mtoto yatima utaendelea hivyo kulalamika kuwa unaonewa hata kama hubaguliwi, tuzungumze kwa tawimu jamani, Wakati Chadema wanafanya maandamano nchi nzima kuzungumzia kupanda kwa gharama ya maisha kuna habari iliachwa? ilitangazwa kila siku na waandishi wengine wanatumwa kubalance kwa serika ijibu tuhuma zile kwasababu ilikuwa maslahi ya umma na watanzania wote tunaumia kwa bei ya vyakula kuwa juu, sasa habari ipi haikutangazwa hadi useme kuna ubaguzi? Sisi wa vijini tunasikiliza sana TBC Taifa na habari zote za Chadema tunapata kila siku, hatulalamiki, TBC1 hal kadhalika sasa wewe tuatkuelewaje?
Jana Mbowe akizungumzia bajeti ijayo nilisikia kwenye taarifa ya habari ubande wa TBC Taifa (redio) ambayo wote mliotoa mawao hapa hamsikilizi kwasababu mpo mjini mnajua TV tu nilisikia habari ya mbowe kwenye taarifa ya habari na pia kwenye kipindi cha Jungu kuu(matukio saa nzima saa 3 hadi saa 4 usiku) upande wa Tv yaani TBC1 mnayozungumzia nimeisikia asubuhi kwenye taarifa ya habari sasa with good coverage sasa mnalalamika nini jamani watanzania? najua wengine mmechangia tu hamjaangalia hiyo taarifa, msiwe na tabia ya kufuata mkumbo jamnai mjivunie shirika lenu la umma, tumeni maoni yenu na ushauri kwa TBC mkiwa nayo siyo malalamiko kwenye jamvi hapa bila takwimu. Sasa wengine wamesema wakati wa Tido mabo yalikuwa mazuri alitangaza vizuri chadema ndiyo maana kafukuzwa, jamani binadamu hawana wema na ni wanafiki kweli, si mlisema Jangwani kakata matangazo wakati wa kampeni kwasababu hapendi CDM? leo tena mnasema hivyo?
Haya mwingine umesema Mshana kepewa maagizo kufanya kazi ya CCM ana kadi ya chama, sasa imekuwaje jana habari ya mbowe imetangazwa vizuri japo hamkuona ndiyo maana mnalalamika hapa, fikirieni kitaifa na kwa maslahi ya umma wetu, msipandikize mawazo maovu kwa watu kuhusu shirika lenu la uuma.
Kwa jinsi nilivyosoma mawazo ya mliochangia hapa ni kwamba mnataka kutukuza vyombo binafsi ambayo hata ukiulizwa wanafanya nini kwa maslahi ya taifa utasema wanaaandika au kutangaza vizuri chama chako, sasa hapo ndo ugonjwa wako, chombo cha umma kinatangaza maswala ya uuma, kama CDM itasema jambo la kitaifa kama kupanda bei hiyo ikiachwa lalamika, lakini cDM wakimtukana Rais nayo iandikwe? hiyo ni habari? ukigombana na mkeo ukiwa kiongozi nayo ni habari? mfano wanasema Slaa na mbowe wanaweza timuliwa Chadema, TBC nayo iingie kwenye uchochezi huo? tafakarimara mbili vaa uzalendo tofautisha chombo cha umma na chombo binafsi.
Naomba kwasilisha mawazo yangu binafsi kama raia mwema huku kijijini.