Tb Joshua alivyonipa utajiri

Tb Joshua alivyonipa utajiri

milion 2 ndani ya miezi 3 ni milioni 180 (2 mara 90 = 180)! Inawezekana vipi kwa milion 180 uweze kununua fuso 2, coasta 3 pia ujenge nyumba 2, restraurant 3? Innocent chacha hebu fafanua vizuri.

Mkuu kweli unatisha ushakokotoa hesabu hadi umemtoa nockout au pengeni amenunua vizuzuki carry,akadhani ni fuso.Hiyo hadith apelekee watoto wa chekechea


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Hata kwa chembe hunidanganyi...wizi mtupu. Naigeria wasinge imba hata huo mziki kama kina davido Maana maji ya utajiri yapo. Zama hizi ni za mwisho kabisa.
 
kuwa mfuasi mzuri wa Yesu haimaanishi kuwa mambo yako yatakuwa mazuri

Ni kweli, lakini hiyo spidi aliyopanda nayo inatisha kama ni kweli maelezo yake. Itabidi watu tusitoke jasho sana maana utajiri wa Yesu wa miezi minne tu, mtu wa kawaida anaweza asiupate kwa umri wake wote, wa labda miaka hata themanini hivi!
 
Ni kweli, lakini hiyo spidi aliyopanda nayo inatisha kama ni kweli maelezo yake. Itabidi watu tusitoke jasho sana maana utajiri wa Yesu wa miezi minne tu, mtu wa kawaida anaweza asiupate kwa umri wake wote, wa labda miaka hata themanini hivi!

ndiyo maana tunasisitiza watu wampokee Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yao
 
Hata kwa chembe hunidanganyi...wizi mtupu. Naigeria wasinge imba hata huo mziki kama kina davido Maana maji ya utajiri yapo. Zama hizi ni za mwisho kabisa.

Davido hajaokoka, mimi nimeokoka. Maji ya upako huwa hayatumiwi na kila mtu. ni lazima huyo mtu awe na neno la Mungu kwanza
 
Nilichosema ni uhakika mtupu. Sijapunguza wala kuongeza neno. Mambo ya rohoni hayapaswi kuaminiwa na watu wa mwilini. Kwahiyo sipati shida ninapoona kuna idadi kubwa ya watu wanabishia ushuhuda wangu.

Ushahidi wako ujakamilika mr chacha.hebu tueleze hiyo restaurant ako inaitwaje??kwa faida hiyo hata serena hotel hawana hiyo faida..mimi ni tomaso nahitaji uthibiti....sho wa macho.
 
Kama utakumbuka, miezi miwili iliyopita nilikuja na post juu ya kutoa shukrani kwa Yesu kwa kumtumia mtumishi wa Mungu TB Joshua kuniponya tatizo langu la uvimbe sehemu za siri ambalo lilikuwa likinifanya kushindwa kusimamisha uume wangu kwa miaka zaidi ya 4. Uponyaji wa tatizo langu ulifanyika kupitia maji maarufu ya ANOINTING WATER yanayoandaliwa na kutolewa na TB JOSHUA MINISTRIES.

Leo nataka nikushirikishe juu ya jinsi maji hayo yalivyonipa FUSSO 2, COASTER 3, NYUMBA 2, na RESTAURANT 3.

Nilianza biashara yangu miezi 4 iliyopita. Kalikuwa ni kamgahawa kadogo tu lakini kwasababu niliamini kwenye nguvu iliyomo ndani ya Yesu, sikuwa na hofu yoyote kuwa mafanikio yanakuja.

Kabla ya hapo, nilisikia shuhuda za watu mbaimbali ambao walitajirika baada yakutumia ANOINTING WATER kwa imani. Nikaamua kuyatumia haya maji kwenye biashara yangu kwa imani kubwa. Nilichokifanya ni kupuliza haya maji kwenye milango na makabati ya chakula huku nikiamrisha wateja wafurike kwenye biashara yangu kwa jina la Yesu.

Huwezi kuamini, mauzo yalibadilika kutoka shs laki 2 kwa siku hadi milioni 2. Watu wanajaa kwenye restaurant hadi nikaamua kuweka viti na meza eneo la jikoni na bafuni. Wateja wako radhi hata kula huku wamesimama au wamechuchumaa. Inapofika muda wakufunga huwa inabidi niwafukuze wateja vinginevyo tunaweza kukesha.

Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2.

ASANTE YESU. ASANTE TB JOSHUA

1. Kuuza milioni 2 kwa siku kwa bei ya chakula cha mgahawani ina maana umeuza pieces 1000 kwa wastani. Mgahawa kuhudumia watu 1000 kwa siku ni "miujiza"

2. Kuuza milioni 2 kwa siku, kwa biashara ya chakula faida haitazidi milioni moja ukiondoa gharama zote. Kwa miezi mitatu ina maana ulipata faida ya milioni 90. Coaster 1 ni sh milioni 40, so coaster 3 ni milioni 120. Fuso moja ni milioni 40 so fuso 3 ni miloni 90. Jumla ni milioni 210. Nyumba moja ya wastani ni milioni 30, so nyumba 2 ni milioni 60. Jumla yote ni milioni 270.

Kapange uongo wako vizuri...
 
Ndio keshasema, ni kwa muujiza wa maji ya annointing!

dah, na tofali ukinyunyiza maji zikiwa kumi tu nyumba inapanda hadi kwenye lenta. Bado bati hapo, ba mbao moja tu inatosha kupaua. Miezi 3 ya muujiza!
milion 2 ndani ya miezi 3 ni milioni 180 (2 mara 90 = 180)! Inawezekana vipi kwa milion 180 uweze kununua fuso 2, coasta 3 pia ujenge nyumba 2, restraurant 3? Innocent chacha hebu fafanua vizuri.
 
Last edited by a moderator:
Heading yako iko vizuri kuwa TB Joshua amekupa utajiri. Umekosea hapo mwishoni ulipomtaja Yesu kwani hakuna uhusiano wa anointing water na Neema ya Bure iliyotolewa na Yesu Kristo wala haiuzwi kwa bei yeyote. Hiyo anointing water ni ibada ya sanamu na ushirikina ambayo chanzo chake ni shetani. Shetani anasema ukinisusujudia na kunitumikia nitakupa milki yote ya dunia. Yesu anasema tafuteni kwanza ufalme wa mbinguni na haki yake na hayo yote mtazidishiwa...hapo usimmsingizie Yesu.

AMEN Mtu wa Mungu. Hawa watu wa ibada za mashetani hawawezi kukulewa. nilishasema ulokole ni janga la Dunia kamasiyo Urimwengu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom