ASSALAMU ALAIKUM
Nakupongeza kwa utafiti na ubunifu wa tiba yako.
Ndugu Ustadh kuwa na uume mdogo au mkubwa siyo kasoro ni maumbile mtu aliyoumbiwa na MUNGU.
Basi kwa nini kuna watu warefu na wafupi?Wanene na wembamba?
Je unaweza kuongeza kimo cha mtu mfupi? Au kupunguza kimo cha mtu mrefu?
Kwa maumbile hayo tuliyoumbiwa isipokuwa tu kwa wenye matatizo ya afya, yatupasa tuzingatie yafuatayo;
Kwanza, Jikubali na ridhika na jinsi ulivyo.
Pili, jiamini kwamba wewe ni mkamilifu na unaweza.
Tatu, Jitahidi kuwa mbunifu jinsi ulivyo.
Kwa kuzingatia hayo bila kujali maumbile yetu mmoja anaweza kufanya chochote kilicho chema kwa UFANISI ULIO TUKUKA.