Tatizo langu ni nini?

Tatizo langu ni nini?

Najua humu ndani kuna watu wa aina nyingi sana.wapo wanaoweza kunisaidia tatizo langu.na wapo wanaptweza kudharau na kunikebeh
Umri wangu ni miaka 29 sasa.kila nikipata mwanamke nikikaa naye sana ni miezi miwili.naanza kumwona hanifai.na sio kwamba nado nao hapana.tukiwa tu ktk mahusiano.
JE TATIZO LANGU NO NINI HAPO?
Na nikueleze uelewe, hao unawaona hawakufai baada ya muda mfupi, ni kwa sababu hawana vigezo unavyovitaka, kwa asilimia mia. Inawezekana wanafikia 90%. Kwa taarifa yako mwenye 100% ya vigezo uvitakavyo ni wewe na Mungu pekee.. Hivyo labda ujioe mwenyewe au ukamuowe Mungu....

 
Haujatulia, ukitulia utaona anakufaa
 
Kabla sijajibu swali lako, naomba nijibu maswali yangu haya ya kipuuzi labda yanaweza kunipa mwanga kuhisi tatizo ulilonalo
  • Unamaanisha nini unaposema "unawaona hawafai"? Ni kivipi? Kitabia, kimuonekano? au kwa namna ipi?
  • Hao wasichana unao wapata huwa unawapata kwa kutumia vigezo vyako mwenyewe? na je huwa wanavifikia hivyo vigezo?
  • Umeshawahi kuota ndoto za ajabu ajabu usiku?

1-Mara nyingi ni kitabia
2-Wrngine wanafokia vigezo
3-cjawai ota kwakweli
 
Auntie Bilal ndoa yake lini? Nilikusoma kule celebrity nikawa na hamu sana ya details za umbea ule. LOL

Ndoa yake na Sauda ni October 25, hapa nilipo mwili wote unaniwasha kwa hiyo siku.
Unajua nini Kaunga, Bilali tumecheza nae tangu ana miaka 2 mpaka huku ukubwani namjua A to Z kuwa ni Mchicha-Pori, sasa hilo la kutaka kuoa ndo kidogo silielewi, japo kwenye hyo sherehe ya kumvisha pete Sauda nilienda, si unajua tena Wa Kinondoni hatunaga hiyana.
Nitakupa umbea mamie,we subiri tu.

babukijana u wapi?
 
Last edited by a moderator:
1-Mara nyingi ni kitabia
2-Wrngine wanafokia vigezo
3-cjawai ota kwakweli
1. Huwa unawaacha bila kuwaambia tabia zisizokupendeza..?? Na je huwa unawaambia mapema kuwa vitu gani huvipendi na vipi unavipenda..?? Je na wewe tabia yako ikoje..??? Yaani wao wanaiona kuwa ni nzuri au mbaya..???

2. Sasa kama wengi wanafikia vigezo, kwanini hao ''wengi'' tena unawaona hawafai,,??
 
Ndoa yake na Sauda ni October 25, hapa nilipo mwili wote unaniwasha kwa hiyo siku.
Unajua nini Kaunga, Bilali tumecheza nae tangu ana miaka 2 mpaka huku ukubwani namjua A to Z kuwa ni Mchicha-Pori, sasa hilo la kutaka kuoa ndo kidogo silielewi, japo kwenye hyo sherehe ya kumvisha pete Sauda nilienda, si unajua tena Wa Kinondoni hatunaga hiyana.
Nitakupa umbea mamie,we subiri tu.

babukijana u wapi?
Aiseee, ninaifuatilia kwa karibu hiyo story shosti, na huyo Sauda is she okay upstairs au wameamua kutengeneza show tu.
 
Na nikueleze uelewe, hao unawaona hawakufai baada ya muda mfupi, ni kwa sababu hawana vigezo unavyovitaka, kwa asilimia mia. Inawezekana wanafikia 90%. Kwa taarifa yako mwenye 100% ya vigezo uvitakavyo ni wewe na Mungu pekee.. Hivyo labda ujioe mwenyewe au ukamuowe Mungu....


Jamani haya maneno mengine wengine mbona mwakosa hekima? kwani hakuna neno lingine la kusema mpaka umwambie ....AKAMUOE MUNGU?
 
Jamani haya maneno mengine wengine mbona mwakosa hekima? kwani hakuna neno lingine la kusema mpaka umwambie ....AKAMUOE MUNGU?[/B][/FONT]
Mungu pekee ndo kakamilika... kwa hiyo sikuwa na mwingine aliyekamilika wa kumwelezea.... wewe na yeye mtakuwa mmepata ujumbe.

 
1. Huwa unawaacha bila kuwaambia tabia zisizokupendeza..?? Na je huwa unawaambia mapema kuwa vitu gani huvipendi na vipi unavipenda..?? Je na wewe tabia yako ikoje..??? Yaani wao wanaiona kuwa ni nzuri au mbaya..???

2. Sasa kama wengi wanafikia vigezo, kwanini hao ''wengi'' tena unawaona hawafai,,??

anatakiwa kujua kuwa hakuna mkamilifu chini ya jua!
 
1-Mara nyingi ni kitabia
2-Wrngine wanafokia vigezo
3-cjawai ota kwakweli

Kama hawafai kitabia, hilo ni jambo jema, maana hakuna maana yoyote ya kumpata mtu mwenye tabia mbovu au isiyokuvutia na kisha mkaendeleza uhusiano wako just tu kuwaambia watu au kuifurahisha akili kuwa nimempata mtu ambaye nimedumu naye kwa muda mrefu, ni upuuzi. Kwa ishu ya kitabia, endelea tu kutafuta ukiwa na subira, yumkini utampata yule ambaye tabia zake utaziona zinafaa.

Na cha kuongezea hapo, nafikiri pia bado haujampata yule ambaye unampenda kweli kweli, maana ukimpenda mtu, mara nyingine kwa baadhi ya watu, hata hizo tabia zisizofaa huwa hawazioni.
Kila la kheri kaka.
 
tatizo lako hujatoa vigezo vya unaowataka na pia wewe mwenyewe ukoje! isije watu wanaongea wee kumbe wewe ndio tatizo.... na inawezekana wewe tatizo
 
Aiseee, ninaifuatilia kwa karibu hiyo story shosti, na huyo Sauda is she okay upstairs au wameamua kutengeneza show tu.

Sauda yuko poa kbs.
Ila ni zile dizaini za akina Kajalla Masanja, sasa hapo ndo hatujui kama ni maigizo au ni kweli Bilali anakula vyombo pale.
Mamie usijali, utapata data zote.
 
kwa hicho ulichoandika, napenda kujua kuna uhusiano gani kati ya kuwa too close na dada au mama
na kumuona mupenzi hafai.....

inawezekana kabisa, wavulana walio karibu zaidi na mama zao au sistas, mama zao wanaweza wakawainfluence hata katika love relationship kwa kuwachagulia wapenzi. kila unayekuwa naye mama au dada anakwambia hakufai. Na wewe mvulana kwa kuwa akili zako zinakuwa kwenye vyupi za dada zako unakubaliana na upuuzi wa dada zako na hasa ikiwa dada zako/mama have had failed relationships/marriages wanakuwa na fikra kuwa mpenzi wako atafaidi/atakufaida na kwa kuwa wanakuown psychologically wanahisi kuwa watakupoteza ukiwa na mpenzi wako.
 
Tatizo lako ni expectation.Una matarajio ambayo sio sahihi juu ya huyo unayekuwa naye.Kwa jinsi ilivyokwisha tokea badilisha mtazamo wako juu ya utakayekuwa naye.
 
inawezekana kabisa, wavulana walio karibu zaidi na mama zao au sistas, mama zao wanaweza wakawainfluence hata katika love relationship kwa kuwachagulia wapenzi. kila unayekuwa naye mama au dada anakwambia hakufai. Na wewe mvulana kwa kuwa akili zako zinakuwa kwenye vyupi za dada zako unakubaliana na upuuzi wa dada zako na hasa ikiwa dada zako/mama have had failed relationships/marriages.

Nimekupata...
ahsante.
 
Back
Top Bottom