Tatizo la umeme nchini linahitaji ufumbuzi wa muda mrefu na sio muda mfupi

Hata hivyo nina kaswali kadogo tu kwa Mheshimiwa - kwa nini aliutafuta ubunge kwa tiketi ya CCM. Nauliza hivi kwa sababu hii post yake yaonyesha wazi kuwa kwa hili la umeme haridhiki na sera zinazotekelezwa na chama chake.

Matatizo ya umeme nchini ni zao la hizo sera na ilani ya uchaguzi za chama tawala na amepiga kura mara ngapi kupinga miswada inayowakilishwa bungeni na serikali. Katika uchaguzi ujao kama atasimama tena kugombea ubunge, je ana mkakati gani kuwa haya mapendekezo yake yatapewa kipaumbele kama chama chake kinashinda ?
Je ni haki kulalamika kuwa miradi kama hii inahitaji hela nyingi wakati rasilimali za taifa zinatapanywa kama vile hazina mwenyewe.

Karibu Mh. Mohamed Dewji, Mbunge wa Singida.

Sidhani kama sera fulani ikikukwaza kwenye chama chako lazima ukimbilie chama kingine, na sidhani Mo amekuja kulalamika kwenye JF. Na at least ame-dare ku-talk openly sijui huko chamani watamuambiaje maana kuna watu hawataki kusikia chochote kuhusu mapungufu yao

Amefanya la maana kuleta hoja kama Mo kutokana na his faith kwamba JF kuna great thinker na sio sinkers

Sometime japo kwa sekunde tujaribu kuweka constructive idea halafu tuone kama ataleta impact yoyote...
 
Sasa wewe hujui hapa kuna kitu kinaitwa profile? click kwenye jina la mtoa mada na utakutana na profile yake. Pili ameweka blog yake chini ya bandiko, fuata hiyo link ili kumjua. Tatu unaweza kumpm na Nne unaweza kumfuta huko Singida(M) kuhakikisha kama ndie ama sie.


...Na hii ina maana gani?

Samahani sana mkuu wangu naona kangara ya ughaibuni imenizidia
 
suala la umeme na maendeleo mengine, naona iko haja ya mikoa, wabunge na wananchi kwa ujumla kuchukua hatua zifaazo badala ya kuiachia serikali ya ccm, aidha wabunge kuwa mobilise watu wao ili wajifanyie kitu cha maana, na hata kwa barabara, ni kuzikaba halamashauri ili mikoa inayo pakana waweze kujiunganisha kwa barabara zilizo bora, kwani ustawi wa maendeleo yao yatatokana na juhudi zao. na kuimarisha miundo mbinu, na nishati
 
.....kwa nini aliutafuta ubunge kwa tiketi ya CCM. Nauliza hivi kwa sababu hii post yake yaonyesha wazi kuwa kwa hili la umeme haridhiki na sera zinazotekelezwa na chama chake. ....


Kimsingi kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake popote pale, cha muhimu asivunje sheria wala kukanyaga haki za wenzake katika kutoa mawazo yao. Kuwa katika CCM hakumnyimi Mo haki yake ya kutoa mawazo yake nje ya chama. Katiba ya nchi inamruhusu!
 
Ninashukuru kwa comments wadau.......ni post yangu ya kwanza lakini ninataka wadau wajue kuwa tatizo la umeme limeshamiri mpaka katika nchi kama Nigeria wakati wamejaliwa utajiri wa mafuta......tukiyaacha hayo I believe constructive discussion should be encouraged...

WanaSingida nimeshirikiana nao katika kuliendeleza jimbo letu kwa kiasi kikubwa miaka minne iliyopita.....sasa ninaamini vijana wa nchi hii tusaidiane kujenga taifa.....and that's my motto KUHAMASISHA VIJANA KUJENGA TAIFA LETU

Mungu Ibariki Tanzania
 
WanaSingida nimeshirikiana nao katika kuliendeleza jimbo letu kwa kiasi kikubwa miaka minne iliyopita.....sasa ninaamini vijana wa nchi hii tusaidiane kujenga taifa.....and that's my motto KUHAMASISHA VIJANA KUJENGA TAIFA LETU

Mungu Ibariki Tanzania

Tafadhari tupe mifano hai ya mambo mliyoshirkiana katika hili la umeme, je ni miradi mingapi ya umeme wa upepo imeanzishwa na kumilikiwa na wanasingida? ni maeneo gani haswa mmefanikiwa na yepi hamkufanikiwa ili na sisi wa jimbo la tabora mjini tujifunze?

Mungu ibariki Tanzani..Amina
 
Hivi Maximum demand wakati wa peak hours, 20:00-23:00 kwa sasa ni megawatt ngapi kwa nchi nzima?. Nina maana kwa mikoa yote ambayo imeunganishwa na grid ya taifa?. Nadhani jamaa zangu wa pale National Grid Center watatusaidia kutupa jibu.
 
Wabunge ndio hupitisha mipango ya muda mfupi na ya muda mrefu ya serikali na ni wao huitengenea fedha. Na pale ambapo hakuna sheria ya kusababisha jambo fulani kufanyika wabunge wana uwezo (kama kundi -chama, au kama mtu mmoja mmoja) kuleta mswada wa sheria wa kusababisha jambo hilo kutendeka au kutotendeka.

Suala la tatizo la nishati siyo geni kwa TAnzania na kwa eneo letu la Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara. Kwa upande wetu Tanzania tatizo hili ni dalili tu ya tatizo lenyewe tulilonalo ambalo ni mipango mibovu ya wanasiasa wetu. Tanzania haina sababu hata chembe ya kuwa upungufu wa nishati ya umeme.

Leo hii kuweza kuyarejesha mabwawa yetu yote ya kuzalishia umeme kwenye full capacity inakadiriwa kutumia karibu dola bilioni 2! Lakini tukifanya hivyo zaidi tutakachopata ni kama Megawatts 1000 hivi (kama sikosei). Lakini wakati huo huo tukitamua kujenga bwawa moja kubwa la Stielger's Gorge itatugharimu karibu dola bilioni 2 vile vile lakini tunaweza kupata Megawatts zaidi 2900!

Wanasiasa wetu hawajui wachague nini! suluhisho lao ni kuingiza majenereta ya umeme na kutoa tenda zaidi ya majenereta. Wako tayari shilingi milioni nyingi kila siku na ukiwauliza hadi leo (kuanzia 1995) serikali imetumia kiasi gani katika kulipia mafuta na IPPs, jibu lake litawafanya muinamishe kichwa kwa aibu!

Sasa, Mhe. Dewji,

a. una mpango gani wa kuleta mswada Bungeni wa kusababisha ujenzi wa Stielger's gorge au kutengea fedha mradi huo mkubwa ilii hatimaye tuondokane na tatizo la umeme?

b. Una msimamo gani kuhusu kampuni ya Dowans ambayo iliingia nchini kitapeli na hadi leo tunahangaika na majenereta yao. Je, kwa maoni yako serikali itaifishe mitambo hiyo na kuwachukulia hatua wahusika wote?

c. Unafikiri Kamati yenu Teule ya Bunge ilifanya kazi yake vizuri katika suala la Richmond na hivyo kazi yake iheshimiwe na wabunge wote au unaamini ilikuwa imewaonea watu mbalimbali?
 
Leo hii kuweza kuyarejesha mabwawa yetu yote ya kuzalishia umeme kwenye full capacity inakadiriwa kutumia karibu dola bilioni 2! Lakini tukifanya hivyo zaidi tutakachopata ni kama Megawatts 1000 hivi (kama sikosei). Lakini wakati huo huo tukitamua kujenga bwawa moja kubwa la Stielger's Gorge itatugharimu karibu dola bilioni 2 vile vile lakini tunaweza kupata Megawatts zaidi 2900!
Mzee Mwanakijiji.

Mradi huo wa Stiegler Gorge ni bomu. Gharama yake kimazingira itazidi faida ya huo umeme. Athari yake kwenye Ruaha basin na Rufiji delta ni kubwa mno. Kibaya kingine ni kuwekeza kwenye source moja kubwa ambapo kama ikija pata matatizo tutaumbuka.

Matatizo yetu kwenye vyanzo vya sasa si kukesekana kwa mvua tu bali ni uchakavu wa mitambo na hali mbaya ya distribution system. Mimi ningewashauri hao wakubwa waachane na mawazo ya kwamba kuna jawabu rahisi. Tuboreshe usambazaji wa umeme na kuhakikisha kuwa ni kiasi kidogo tu kinachopotea njiani kuelekea kwa mtumiaji.

Tuangalia vyanzo vidogo vidogo. Ukiangalia mahityaji yetu ya umeme kwenye miji mingi ni madogo na si ya kutisha. Tuangalia solution zinazoendana na sehemu hizo. K.m. Singida wawekeze kwenye upepo na jua, sehemu za milima kwenye maporomoko madogo nako wanaweza kujenga vi micro power station (maporomoko ya mita moja yanaweza kuzalisha umeme wa kutosha kijiji), sehemu zenye wafugaji waangalie bio-gas, sehemu zenye wakazi wengi, taka taka zao zitumike kuzalisha umeme, kodi kwenye vifaa vya kuzalisha umeme endelevu (sio jenereta) ipunguzwe ili wananchi waweze kuzalisha umeme kwenye majumba yao na kwenye maofis, wenye viwanda kama vya sukari wahamasishwe kuzalisha umeme kutokana na masalio ya miwa, vile vile wenye viwanda vinginei n.k.

Vyote hivi vikiunganishwa, hili tatizo tutalitatua kwa kiasi kikubwa na zaidi ya yote kuweka umeme karibu na wananchi wa kawaida ambao sehemu kubwa hadi leo wanaosikia kwenye redio zao za betri!

Tuachane na hii miradi mikubwa ambayo sana sana inawafaidisha wachache sana.

Amandla........
 
Mo,

Ni maoni mazuri na sio kusema Dr Idriss hafai au anafaa. Kwa kuongezea ni kwamba Tanzania tusifikirie one energy source tunaweza kufocus katika Nuclear Energy. Sababu kuu ni tatu kwanza hii energy ni renewable energy therefore inaweza kuwa environmental friendly. Pili Tanzania ina reserve kubwa ya uranium madini ambayo ni haba duniani na malighafi kuu katika uzalishaji wa umeme. Tatu, maji or hydro-electical na windpower energy ni seasonal hivyo basi panaweza kutokea shortage ya umeme kipindi fulani but Nuclear energy inatwanga throughout the year.

Disadvantage zake ni kwamba ni expensive na sometimes can be dangerous kwasababu technologia yake huweza kubadilishwa kuwa silaha but to me those are trivial issues. Kuhusu gharama tunaweza kuspread costs tukashirikiana na wenzetu uganda na Kenya (even though kenya wenzetu wameshatenga budget ya hiyo kitu). But tunaweza kushirikiana na wenzetu. Pia tunaweza kuomba funding from world bank tukawalipa kidogo kidogo kwani tukishaanza kuzalisha umeme tunaweza kuuza nchi za jirani tukapa pesa za kulipa deni na shirika likajiendesha kibiashara. Kuhusu silaha nadhani Atomic Agency ya Professor Mohammed Elbaradei. Hii inasimamia na hivyo basi watatoa misimamo yao. Tuna mtaalamu mkali anayetambuliwa duniani Dr Shein (Vice president wa Tanzania tumtumie kwa faida ya Tanzania).
 
Ni maoni mazuri kusema Dr Idriss hafai au anafaa.
Hawezi kuepuka responsibility hata umtetee vipi. It was under his watch hali ya sasa ndiyo imetokea. Obama analaumiwa kuhusu kukesekana kwa kazi marekani ingawa wote wanajua matatizo yalianza na George W. Yeye ndiye yuko kwenye madaraka na hawezi kukwepa responsibilty. Ndivyo ilivyo kwa Idriss. Hawezi kuepuka kwa kuwasingizia waliomtangulia au wanasiasa. Yeye angeona yote haya kama ni obstacle basi angeachia ngazi.

Hapana, Mkuu. Dr. Rashidi hafai kuendelea na uongozi wa Tanesco. Awapishe wengine wajaribu. Sababu nyingine ziko hapa http://allafrica.com/stories/200907280404.html



Amandla.....
 
Hawezi kuepuka responsibility hata umtetee vipi. It was under his watch hali ya sasa ndiyo imetokea. Obama analaumiwa kuhusu kukesekana kwa kazi marekani ingawa wote wanajua matatizo yalianza na George W. Yeye ndiye yuko kwenye madaraka na hawezi kukwepa responsibilty. Ndivyo ilivyo kwa Idriss. Hawezi kuepuka kwa kuwasingizia waliomtangulia au wanasiasa. Yeye angeona yote haya kama ni obstacle basi angeachia ngazi.

Hapana, Mkuu. Dr. Rashidi hafai kuendelea na uongozi wa Tanesco. Awapishe wengine wajaribu. Sababu nyingine ziko hapa http://allafrica.com/stories/200907280404.html



Amandla.....

Mie nina swali moja tu kwako na link uliyotupa kuhusu matengenezo ya nyumba. Je makisio ya shirika yanasemaje? Kama Board iliyapitisha, basi Idrissa hata mumseme vp kama yamo ndai ya budget tatizo lipo wapi mkuu??? na Mohammed Dewji kazungumzia opinion yake kuhusu umeme inahusiana vp na Dr Idrissa hiyo hoja ipeleke kwenye Thread ya Dr. Idrissa mie nimeitoa kama rhetoric statement ya kwamba tuzungumze cha maana kuhusu Tanesco kwani hapa JF na hakika hata Rais akipata muda huwa anaisoma aone maoni ya wananchi sasa tuzungumze constructive criticism na sio destructive ili nchi iendelee na sio kurudi nyuma
 
Tumewekesha nguvu za Umeme ktk Hdro power miaka 30 iliyopita na nguvu zake zinatuwezesha kila kata nchini kupata umeme.. Swala kubwa ni UKARABATI, utamaduni ambao sisi MIAFRIKA hatuna..

Inashangaza na kusikitisha sana naposoma makala ikisema tuna Hdropower yenye uwezo wa kuzalisha Mw 4,700 lakini ni only asilimia 12 ya uwezo huo ndio inatumiwa..

Na ukirudi ktk matumizi tunaambia only asilimia 12 ya wananchi ndio wanapata Umeme kitu ambacho kinanipa imani kwamba kama Mw zote 4,700 za hdropower zikifanya kazi tutakuwa na uwezo wa kuwapa wananchi kwa asilimia 100..Hapo bado hatujahesabu nguvu nyinginezo..

Ni uzembe mtupu unatumika kwetu sijui hizo nchi nyinginezo lakini binafsi sioni sababu nje ya kutokuwa na VIONGOZI BORA..
Hili nimewahi kulizungumzia hata wakati tunauza viwanda vyetu...Matatizo yalikuwa tulishindwa kuzalisha kulingana na kiwango cha viwanda vyenyewe, haya soko lilikuwepo iweje tunauza viwanda wakati tatizo sii viwanda ila ni uongozi mbaya wa viwanda hivyo?..

Haya sii ndio ya mwanamme kumtalakia mke kwa sababu hapati mtoto hali ukweli ni kwamba bwana ndiye mwenye matatizo ya uzazi?..

Inawezekana design ilikuwa hiyo MW 4,700 kama unavyosema lakini baada ya matumizi ya miaka mingi hicho kiasi hupungua tokana na kupungua kwa kina cha maji baada ya ukame ama mkusanyiko wa matope chini ya bwawa. Tope huletwa na mto. Kuondoa matope ni ghali sawa na kujenga hydro nyingine ama zaidi.

Kama turbines zipo zenye uwezo zaidi (yaani zina mizunguko zaidi kwa kiasi kilekile cha maji), basi dawa ni kubadilisha. Lakini kuna uwezekano zilizopo TZ ni zile bora hivyo jibu ni kuendelea kujenga hydro zingine. Kama hatuna sehemu za kujenga hydro moja kubwa basi inabidi tuangalie sana uzalishaji kwa solar ama thermal power. Nuclear ni jibu zuri lakini je tunaiweza? Nchi nyingi, hata China walianza kwa kujengewa nuclear power, nasi tunaweza fanya hivyo.

Lakini je CCM inaweza SIMAMIA maana badala ya nafuu itakuwa ghali na hapo ndio naungana nawe kua HATUNA UONGOZI BORA kutuletea mbadala wa vihydro.
 
Kwa nini Afrika tu? They are still with us. Kumbuka wale jamaa waliotaka kuhujumu mitambo ya Msumbiji akiwemo mjerumani nadhani ili wapate dili la biashara za majenereta. Wafanyabiashara nanyi mmo kwa kutengeneza matatizo!! Hata tatizo letu ni artficial, kuna watu wanafanya biashara zao, na ndivyo zilivyo nchi nyingine za Afrika.
 
Mie nina swali moja tu kwako na link uliyotupa kuhusu matengenezo ya nyumba. Je makisio ya shirika yanasemaje? Kama Board iliyapitisha, basi Idrissa hata mumseme vp kama yamo ndai ya budget tatizo lipo wapi mkuu??? na Mohammed Dewji kazungumzia opinion yake kuhusu umeme inahusiana vp na Dr Idrissa hiyo hoja ipeleke kwenye Thread ya Dr. Idrissa mie nimeitoa kama rhetoric statement ya kwamba tuzungumze cha maana kuhusu Tanesco kwani hapa JF na hakika hata Rais akipata muda huwa anaisoma aone maoni ya wananchi sasa tuzungumze constructive criticism na sio destructive ili nchi iendelee na sio kurudi nyuma

Mkuu, wewe ndiye uliyemuingiza Idriss humu. Hamna cha rhetoric whatever. Usitake kukwepa responsibility kama anavyotaka kufanya huyo unayemtetea.

Tatizo sio kuwa matengenezo yalikuwemo kwenye bajeti au la. Tatizo ni item kama ya maua ya plastiki iliingiaje kwenye hiyo bajeti. Tatizo ni kuwa katika wakati huu mgumu, kiongozi makini anaweza kupeleka maombi kama hayo kwa bodi yake? Kupitishwa na bodi si hoja. Bodi zetu mara nyingi zinategemea fadhila za menejimenti au unadhani vibahasha vinatoka wizarani au bungeni?

Wakati mwingine tunahitaji kubomoa kabla ya kujenga. Hapa hakuna anayemchukia Dr. Idriss kama mtu bali tuna kila haki ya kupinga kuwa anastahili kuendelea kama ilivyo kwako kumtetea kuwa anafaa.

Amandla.......
 
Pengine TANESCO wamewahi kuwa na mpango kabambe kama huo. Hebu watwambie kama wamehi kuwa nayo ili tujue ni kwa kiasi gani siasa zetu chafu na mipango mibovu imekwamisha juhudi za wataalamu! Tatizo kubwa ni uongozi usio na uwezo, nia, dira wala uzalendo!
 
Wabunge ndio hupitisha mipango ya muda mfupi na ya muda mrefu ya serikali na ni wao huitengenea fedha. Na pale ambapo hakuna sheria ya kusababisha jambo fulani kufanyika wabunge wana uwezo (kama kundi -chama, au kama mtu mmoja mmoja) kuleta mswada wa sheria wa kusababisha jambo hilo kutendeka au kutotendeka.

Suala la tatizo la nishati siyo geni kwa TAnzania na kwa eneo letu la Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara. Kwa upande wetu Tanzania tatizo hili ni dalili tu ya tatizo lenyewe tulilonalo ambalo ni mipango mibovu ya wanasiasa wetu. Tanzania haina sababu hata chembe ya kuwa upungufu wa nishati ya umeme.

Leo hii kuweza kuyarejesha mabwawa yetu yote ya kuzalishia umeme kwenye full capacity inakadiriwa kutumia karibu dola bilioni 2! Lakini tukifanya hivyo zaidi tutakachopata ni kama Megawatts 1000 hivi (kama sikosei). Lakini wakati huo huo tukitamua kujenga bwawa moja kubwa la Stielger's Gorge itatugharimu karibu dola bilioni 2 vile vile lakini tunaweza kupata Megawatts zaidi 2900!

Wanasiasa wetu hawajui wachague nini! suluhisho lao ni kuingiza majenereta ya umeme na kutoa tenda zaidi ya majenereta. Wako tayari shilingi milioni nyingi kila siku na ukiwauliza hadi leo (kuanzia 1995) serikali imetumia kiasi gani katika kulipia mafuta na IPPs, jibu lake litawafanya muinamishe kichwa kwa aibu!

Sasa, Mhe. Dewji,

a. una mpango gani wa kuleta mswada Bungeni wa kusababisha ujenzi wa Stielger's gorge au kutengea fedha mradi huo mkubwa ilii hatimaye tuondokane na tatizo la umeme?

b. Una msimamo gani kuhusu kampuni ya Dowans ambayo iliingia nchini kitapeli na hadi leo tunahangaika na majenereta yao. Je, kwa maoni yako serikali itaifishe mitambo hiyo na kuwachukulia hatua wahusika wote?

c. Unafikiri Kamati yenu Teule ya Bunge ilifanya kazi yake vizuri katika suala la Richmond na hivyo kazi yake iheshimiwe na wabunge wote au unaamini ilikuwa imewaonea watu mbalimbali?

d. Na wewe mtoa mada una mpango gani wa kusababisha ujenzi wa Stielger's gorge kwa kusudi la kusaidia tuondokane na tatizo la umeme?
 
Leo hii kuweza kuyarejesha mabwawa yetu yote ya kuzalishia umeme kwenye full capacity inakadiriwa kutumia karibu dola bilioni 2! Lakini tukifanya hivyo zaidi tutakachopata ni kama Megawatts 1000 hivi (kama sikosei). Lakini wakati huo huo tukitamua kujenga bwawa moja kubwa la Stielger's Gorge itatugharimu karibu dola bilioni 2 vile vile lakini tunaweza kupata Megawatts zaidi 2900!

Nadhani tatizo ni kukosa utashi. TRA wanakusanya close to US$ 2 billion kwa mwaka. Kama kungekuwa na utashi hata kwa makusanyo yetu ya ndani tungeweza kukamilisha miradi kama hii kwa miaka 5-10.
 
Back
Top Bottom