Tatizo la kula/kutafuna kucha

Tatizo la kula/kutafuna kucha

hiyo ni kama tabia ya kuku kula mayai hivyo jitahidi ule vyakula vyenye kalsium kwa wingi pamoja na kula vyakula vyenye madini ya chuma sana,
 
1472149964843.jpg


Hiki kitu kina waathirika wengi sana wake kwa waume wakubwa kwa wadogo. Tunaweza kudhani tu kuwa ni tabia mbaya au mazoea! La hasha kutafuna kucha za vidole vya mikononi ni tatizo la kisaikolojia linalomla mtu ndani kwa ndani kwenye ufahamu wake ambapo hupelekea viashiria hivi:-

-woga
-mawazo/msongo wa mawazo
-kutojiamini
-fadhaa/sononi
-kukosa la kufanya
-taharuki
-mapepe/restless mind
-hulka ya kuiga

Hivyo ni viashiria vikuu vya mtafuna kucha na hili jambo hufanya bila kupenda ni involuntary action. Kuna baadhi hufanya wakiwa pekeyao kwenye upweke na wengine hufanya pindi anapokutana na mtu kwa mara ya kwanza ama hadhira.

1472150495442.jpg


Kwakuwa hili ni tatizo la kisaikolojia zaidi basi hata tiba yake ni ya kisaikolojia, hasa hasa

-councelling/ushauri nasaha
-kumjengea uwezo wa kujiamini mwathirika
-kutafiti kupitia yeye mwenyewe chanzo cha tatizo lake hilo na muda

Wengine hukutana na hii hali katika hatua fulani ya makuzi na ikipita tatizo hujitibu lenyewe!

Je una tatizo kama hili ama ndugu yako? Ama rafiki? Usikimbilie kwa mganga wa kienyeji utaambiwa una jini njaa..! Tiba unayo mwenye
 
Asante wenye tatizo nadhani wamekuelewa, lkn hivi wapo na wanaotafuna za miguuni..?
 
m n mwathrika kabsa wa hilo tatzo naliepukaje jaman
 
Nimekuelewaaa sana mkuu na uzi wako!n'a imani utakuwa umepigaa ikuluuu humu

Ova
 
Tuko weng aisee nataman niache naweza jizuia kwa muda ila naenda narudia tena
 
Mamaaaa me ndo addicted miakA mi nne sasa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom