Tatizo la kula/kutafuna kucha

Tatizo la kula/kutafuna kucha

Mimi hata sijui nisemeje maana najua matatizo kibao yananikabiri na nature ya kazi yangu ndo hatari ila Mara nyingi ni psychosocial behavior kindly like ukichaa flani kuna mdau hapo huu ameelezea vizuri sana bila tatizo linakuja pale kwenye kupata hizo nails paint maana zina kagharama kidogo na kosa ukizitoa utatafuna mpaka utajuta
 
Unaweza ukaacha kutafuna kucha "kama utataka". Hakuna aliezaliwa akitafuna kucha isipokuwa hayo ni matokeo ya kimazingira.

Tatizo la kutafuna kucha tena "mpaka kuitwa tatizo" si kidogo. Kwa wenzetu wanasaikolojia wanaliita "tatizo la kitabia" na kwa watafunaji wengi, huwa kuna mazingira linatokea; mfn. Unapokuwa na stress, huna kazi ya kufanya, una matatizo ya ulaji n.k.

Katika umri mkubwa hali hii huwa ni mbaya sana kwa muathirika kwani unakuta mtu hawezi kupitisha dk 5 bila kuweka kidole aama vidole mdomoni na kuanza kung'ata kucha hata kaama ni fupi mno.

Ni kweli hali hii huleta fedhesha kwa mtafunaji hasa pale anapokuwa mbele za watu wa kuheshimika ama anapofanya presentation ya kitu fulani.
UNAWEZAJE KUACHA.
Kuacha si rahisi kama "hutatia nia ya kufanya hivyo". Utafunaji wa kucha ni tabia na mtu hujifunza tabia fulani na huamua kuiacha pia (a behavior can be learnt or unlearnt).

Kama alivyosema msemaji mmoja hapo juu njia moja wapo ni KUPAKA VITU VICHUNGU KWENYE KUCHA ZAKO ambavyo vitakufanya ushinde kuzitafuna kucha zako

Pili, kuviwekea "nail clip" vidole vyako.

Kuweka kitu kwenye meno ya upande wa juu mbele ambavyo vitasaidia kuzuia ukataji wa kucha.

Tatu, kujitahidi kujiepusha na vitu vinavyoweza pelekea kutafuna kucha (najua utakuwa unajua ni mazingira gani huwa unatafuna kucha zako)

Kutafuta kitu mbadala ambacho kitakufanya uwe bize nacho (kama gums) hivyo kutojishughulisha na kucha zako, ingawa nazo si nzuri.

Jitahidi kujizuia hata kwa kuvifunika vidole vyako kwa vitambaa ama gause kwani ukiweze kufanya moja ya mambo hayo kwa muda wa miezi miwili ama zaidi, hakika utaondokana na tatizo la kutaka kutafuna kucha'zo.

Dawa ya kuondoa tatizo linalokusumbua kwanza ni kama ulivyofanya "kuliona tatizo na kulikubali" na pili "kuchukua hatua" kwa kudhamiria kufaaanya hivyo.

All the best dear!
Ushauri mzur asnte.
 
sio rahisi kuacha ila jitahidi kuiweka busy mikono yako utaacha taratibu kula kucha.
 
mimi ndo huwa natenga kabisa kwamba kidole hiki ni cha jumatatu, hiki cha jumanne hiki jumatano mpaka jumapili ili kuhakikisha kuwa nikiwa nang'ta hizi basi nyingine zinaota na kuwa na mzunguko mzuri ila sku izi najitahidi naanza kuacha acha
 
Kama kichwa kinavyojitaja,

Nina swali juu ya hili swala kwa sababu cjui sababu ya kupelekea mtu kutafuna kucha na pia ningependa kujua tiba yake kwe sababu ni jambo ambalo limenikumba na nahitaji kuacha.

Naomba msaada wenu!!
Hizo ni stress mwone dr wa saikologi akusaidie
Same applies to me, nahitaji sana huo msaada jaman nishakuwa muathirika kabisaa
 
Tumia bablishi zisizo na Sukari badala ya vizipo
Mimi tatizo langu ni kula kizibo cha kalam(pen)yaani siwezi kukaa na pen bila kuitafuna kizibo,kiasi kwamba ofisi nzima wanajua pen zangu.nimejizuia nimeshindwa.mradi hainidhuru nimeona niache hali kama ilivyo.
 
vipi wale tnaotafuna lips kwa ndani?
hii ni nini au ni mastress pomoni....
 
Kitaalam walaji wa kucha huwa wana lack madini chuma. Hivyo basi ili kuacha hii tabia ya kula kucha ni vema mtu akafanya mpango wa kula dagaa za kutosha kwa mfululizo kwa.mda wa mwezi mmoja. Hii imemsaidia sana jamaa yangu alikuwa anakula.kucha hadi zinavuja damu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom