Taratibu za kufunga ndoa ya Serikali (Bomani)

Taratibu za kufunga ndoa ya Serikali (Bomani)

kwa ukristo nadhani kuna dhehebu wanaikubali hiyo ndoa japo inabidi muende kuibaliki hiyo ndoa ila kwa imani ya kiislam hiyo ndoa haitambuliki ni sawa tu kama mnavyoishi sasa hivi
Mke ana imani Kali ya kikristo ,na kuja kwenye uislam anakuwa mgumu,siwezi kumlazimisha cha muhimu upendo masuala ya dini kila mmoja abaki na yake
 
Salaam kwenu wakulungwa

Baada ya kuishi kwenye mahusiano na mama watoto wangu kwa miaka 8 bila ndoa nimefikiria kufunga ndoa ya kiserikali. Nimeamua hivi ili kila mtu anendelee na imani yake kwa Amani na upendo, yeye mkristo na Mimi muislam

Sasa wajuvi wa mambo naomba mnijuze taratibu zote za kufunga hii ndoa zinavyokuwa ,Lengo niwe na ufahamu mapema kabla sijaanza kufuatilia mchakato mzima

Jumapili njema.
Romani Katoliki kuna ndoa mseto nenda mkafunge ndoa romani na bado kila mtu atabaki na dini yake
 
Kwa nini umefikilia kufunga ndoa ya kiserikali na si ya dini? Dini zenu tofauti sawa, kwanini mmoja wenu asibadili, miaka 8 ni mingi umezini imetosha sasa au unataka kuendelea kuwa mzinifu?
Hiyo kwa kuwashauri kubadili dini sio jambo dogo kama kuandika msg, wape ushauri utakao wajenga lakini usiharibu imani zao, wewe unajua athari za kubadili dini wewee
 
Mke ana imani Kali ya kikristo ,na kuja kwenye uislam anakuwa mgumu,siwezi kumlazimisha cha muhimu upendo masuala ya dini kila mmoja abaki na yake
Vp kuhusu watoto (kama wapo) watalelewa katika imani ipi?
 
Utaratibu unaanzia kwa AFISA Mtendaji wa Kata ya Wilaya unayoishi, Kwa ajili ya kupata barua ya utambulisho wa makazi yako.

Halafu unaipeleka hiyo barua kwa Mkuu wa wilaya kwa ajili ya kuandikisha ndoa, Baada ya hapo Tangazo litabandikwa hapo wilayani kwenye ubao wa matangazo, Utalipia 40,000/=Tsh.

Ndoa itafugwa siku ya Jumanne au Ijumaa Asubuhi (Kulingana na Ratiba ya Ofisi). Atakayefungisha Ni Mkuu wa wilaya au katibu tawala. Ufike na mashahidi wawili kwa kila mmoja wenu Mkiwa mmeva mavazi ya heshima. Baada ya hapo mtapokea Vyeti vya ndoa ambayo inatambulika kisheria.

My take. Nibora Ndoa ya Bomani kuliko kuishi kienyeji hasa Kama una Mali na watoto ili kuwalinda kisheria Pindi ikitokea umewahi kutangulia mbele ya haki.
Nawasilisha.
images (32).jpeg
 
Katika uislamu 'ndoa' ni ibada na ina taratibu zake, moja ni kuwa wanandoa wote lazima wawe waislamu. Ndoa yyte na mtu wa dini tofauti haipo na inahesbika kama uzinifu tu. Kwa better future ya kizazi chenu na ihesabike ndoa kama wew ni muislamu bas hakikisha shemeji anabadili dini, otherwise hamna ndoa kwa mtazamo wa kiislamu abadani!

Sent from my SM-N910U using JamiiForums mobile app
 
Katika uislamu 'ndoa' ni ibada na ina taratibu zake, moja ni kuwa waandoa wote wawe waislamu. Ndoa yyte na mtu wa dini tofauti haipo na inahesbika kama uzinifu tu. Kwa better future future ya kizazi chenu na ihesabike ndoa kama wew ni muislamu bas hakikisha shemeji anabadili dini, otherwise hamna ndoa kwa mtazamo wa kiislamu abadani!

Sent from my SM-N910U using JamiiForums mobile app

Muislamu Mwanaume anaweza kumoa Mwanamke wa Kikrosto/Kiyaudi pale vigezo na masharti vitakapokuwa vimezingatiwa na kutimia. Lakini Mwanamke Muislamu hawezi kuolewa na Mwanaume Mkristo/Myaudi.
 
Sheria ya ndoa ya JMT kuna ndoa za aina 3 zinazotambulika,nazo ni za Kidini,Serikali na kimila,masuala ya kuonekana nadhini sijui nini kwangu hayana nafasi,nataka kila mmoja aendelee na ustaarabu wa imani yake

Cheti ni kile kile kaka wee kanyaga twende.
Umuhimu wa ndoa ni kutokuchepuka sio cheti au dini gani
 
Watoto wapo ,wakikua watachagua imani itayowafaa kati ya uislam au ukristo,siwezi kuwalazimisha ,wao ni nafsi huru wataamua wenyewe,cha msingi wanatambua Mimi ni baba yao,so nawapa Uhuru wa kuchagua imani ya kufuata

Una miakili weye acha tuu...tungekuwa na watu kama weye wengi zaidi duniani tungefurahi sana.
 
Nimeipenda hii comment
Unapenda wakati mwenzako amejichanganya!!

Hivi nikuulizeni- baba na mama tofauti dini zao watoto watawalea vipi mpaka wafikie kuchagua dini waitakayo? Nitakupa mifano kadhaa

1.baba anataka atangulize kulia katika mambo yake (mfano kunawa) huku mama anatanguliza kushoto mtoto akiuliza yeye atangulize kipi mtamjibu nini

2.baba anasema bismillah anagonga msosi mama anapiga ishara ya msalaba akiwa amefunga macho anaomba kwanza ndo aanze kula je mtoto ataambatana na nani kati yao

3.baba anatoka anaenda msikitini mama anatoka anaenda kanisani je mtoto ataambatana na yupi au ndo utamwambia atulie nyumbani asubiri awe mkubwa achague kwa kwenda

Na kadhalika!

4.
 
Unapenda wakati mwenzako amejichanganya!!

Hivi nikuulizeni- baba na mama tofauti dini zao watoto watawalea vipi mpaka wafikie kuchagua dini waitakayo? Nitakupa mifano kadhaa

1.baba anataka atangulize kulia katika mambo yake (mfano kunawa) huku mama anatanguliza kushoto mtoto akiuliza yeye atangulize kipi mtamjibu nini

2.baba anasema bismillah anagonga msosi mama anapiga ishara ya msalaba akiwa amefunga macho anaomba kwanza ndo aanze kula je mtoto ataambatana na nani kati yao

3.baba anatoka anaenda msikitini mama anatoka anaenda kanisani je mtoto ataambatana na yupi au ndo utamwambia atulie nyumbani asubiri awe mkubwa achague kwa kwenda

Na kadhalika!

4.
Mungu ni mmoja Hakuna shida. Watoto wakienda dini ya mama sawa , wakienda dini ya baba sawa.
 
Back
Top Bottom