Tanzania ya Ujamaa ndani ya Ubepari uchwara(petty bourgeoisie)

Sina hakika kama Tanzania ni nchi ya kijamaa vile lakini ninafikiri udhibiti wa unyonyaji wa makundi yenye nguvu kiuchumi dhidi ya makndi ya wafanya kazi na wachuuzi wadogo ndio tatizo letu. hatujamudu kuweka udhibiti maridhawa, ndio sababu kuna migogoro ya wawekezaji na wananchi. Ndio sababu wakulima na wafugaji hawaishi kugombana: Kumekosekana udhibiti madhubuti katika sekta za uzalishaji mali. Wawekezaji wanaoanekana ni wa maana kliko wananchi.

Wawekezaji wanaonekana wa maana lakini siyo wa maana Sana vile vile haswa ukichukulia Tanzania haina any competitive advantage kiuchumi kwenye sekta yeyote ile (labda madini kwa mbali sana), bila hii competitive advantage mwekezaji anakua hana uhakika wa mtaji wake achilia faida atakayopata-kama hujajua competitive advantage angalia gharama za uzalishaji, kodi,miundombinu mibovu, upatikanaji wa wafanyakazi wenye uzoefu na sekta husika, n.K, kwa haya Mimi Naona serikali ingebidi iweke mazingira mazuri zaidi kwa wawekezaji haswa wale wa ndani kwa zaidi hata ya inavyofanya sasa ambapo mazingira bado hayakidhi haja ya mwekezaji kuwekeza zaidi ya kwenye sekta ya madini peke yake.
 
Mama unaandika vizur, Ungeungana na UKAWA 2015 NINGESOMA HII MAKALA, maake ningejua unaandika uhalisia, zaidi sana naona unaandika stories tu
 
Shuleni masomo uliyosoma yalikuwa na chapter ngapi?

Tukikupeleka ukajadili mkataba wa bomba la gesi au wa Standard Gauge Railway au wa mgodi wa buzwagi,utamaliza hata utangulizi kweli?

Hapo ndipo watanzania tunapopigiwa,baadae tumaanza,oohh,sasa mbona wanapeleka mchanga nje ya nchi.

Kuna msemo kwamba "ukitaka kumficha mwafrika jambo lolote,liweke katika maandishi/kitabu"

Pia kuna utani kwamba kabla ya kubadili na kusaini mikataba mikubwa mkubwa,wachina hutupokea kwa bashasha kubwa sana ya vinywaji,pombe,mpaka usiku mnene,unaingia ukumbini uko hoi,ukumbini vidada virembo kabisa vinahudumia kwa bashasha,

Vinatutoa kwenye mjadala tunabaki kuvitongoza
Kusoma kitabu ama mkataba na kusoma makala kwa kutumia simu ni vitu viwili tofauti.
 
Ziko changamoto nyingi na kubwa pande zote. Hakuna kitu rahisi, ni lazima kuzikabili zote.


Ni kweli kabisa lazima tukubali na tuamue kuanzia sasa kuzikabili changamoto zetu ili tuweze kusonga mbele kwa pamoja kama Taifa. Kitu kikubwa kwetu tuwe na imani na hakika tutafanikiwa katika matarajio yetu.
 
Ziko changamoto nyingi na kubwa pande zote. Hakuna kitu rahisi, ni lazima kuzikabili zote.


Ni kweli kabisa lazima tukubali na tuamue kuanzia sasa kuzikabili changamoto zetu ili tuweze kusonga mbele kwa pamoja kama Taifa. Kitu kikubwa kwetu tuwe na imani na hakika tutafanikiwa katika matarajio yetu.
Nyerere alisema "ujamaa ni imani" mpaka leo huwa sielewi alimaanisha kwamba si mfumo wa kiuchumi?
 
Nyerere alisema "ujamaa ni imani" mpaka leo huwa sielewi alimaanisha kwamba si mfumo wa kiuchumi?
Hapo mimi nadhani imani alimaanisha kuwa Ujamaa una itikadi na misingi yake tofauti na Mfumo uliokuwepo wa Ubepari ambao nao una itikadi na misingi yake vile vile. Sasa anaposema Ujamaa ni imani anakuandaa kisaikolojia ili uweze kubadilika kutoka Ubepari hadi Ujamaa. Ujamaa una vitu kama utaifishaji mali, chama kimoja, vijiji vya ujamaa na kadhalika. Hivo hivo Ubepari una Soko huria, ushindani na kadhalika. Sasa kuwatoa watu wenye uelewa na ufahamu kutoka kwenye Ubepari kwenda kwenye Ujamaa siyo kitu rahisi wapo ambao watapinga, wapo watakaokubali na wengine kwenda kwa kulazimishwa na hapo wanaopinga inabidi wawe na imani na Ujamaa kwamba utawaletea mafanikio. Yani kama waumini waumini wa dhehebu fulani lazima wawe na imani na dhehebu lao katika suala zima la kumuabudu mola. Vilevile lazima uwe na Imani na Ujamaa kama solution ya Kiuchumi. Hapo nazungumzia hilo huku naashumu kuwa Serikali imeshajiandaa kupelekea mfumo husika ili kuwarahisishia wananchi waweze kufanya kazi kwa bidii ili kuujenga uchumi imara. Lakini kama Serikali haijajiandaa yani imevamia tu mfumo basi ni lazima muanze kuathirika na athari za kujiandaa kwenda kwenye mfumo wa Ujamaa au Ubepari.
 
Sina hakika kama Tanzania ni nchi ya kijamaa vile lakini ninafikiri udhibiti wa unyonyaji wa makundi yenye nguvu kiuchumi dhidi ya makndi ya wafanya kazi na wachuuzi wadogo ndio tatizo letu. hatujamudu kuweka udhibiti maridhawa, ndio sababu kuna migogoro ya wawekezaji na wananchi. Ndio sababu wakulima na wafugaji hawaishi kugombana: Kumekosekana udhibiti madhubuti katika sekta za uzalishaji mali. Wawekezaji wanaoanekana ni wa maana kliko wananchi.
Kwangu kuwapo kwa hiyo migogoro ya ardhi ni ushahidi tosha kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa. Ardhi ni mali ya umma na rais ni mlinzi wa mali hiyo kwa niaba ya wananchi. Pia wananchi wanatambua hivyo kupitia katiba yao ya kijamaa kuwa yeyote aliyepewa ardhi huwa amekodishwa tu. Iwapo kutakuwa kunahaja ya kubadilisha matumizi ya ardhi husika Mh Rais anaweza kubadili matumizi. Kwa kujua hili wananchi wamekuwa wakitumia fursa hiyo. Laiti tusingekuwa na ujamaa hakuna ambaye angethubutu kudai mali ya mtu au taasisi. Hata hao wanaharakati wasingethubutu kufanya hivyo. Chukua mfano Kenya wao wamezoea kuwa wapangaji kwenye ardhi za watu. Husikii kelele kama huku kwetu.
Pia uhusiano wa uzalishaji katika nchi ya Tanzania umekuwa ukitathiminiwa kijamaa kwa kuangalia kuwapo kwa usawa wa kipato miongoni mwa wanajamii ili kusiwepo na pengo kubwa kati ya walionacho na wasionacho. Mataifa ya kibepari huwa hayaangalii hiki kitu survival for the fittest was and still is the rule of the days. Kila mtu atajijua.
Migogoro ya ardhi itamalizwa pale serikali itakapoamua kufifisha ufugaji wa kienyeji kwa njia yoyote itakayotafitiwa na kufaa. Pia kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kuishi makazi yaliyopangwa. Zaidi ya hayo serikali ihuishe sera ya makazi na ihakikishe kunakuwa na makazi ya kutosha kwa kizazi kinachoingia kazini. Kufificha makazi msambao na kuhimiza makazi shadidi.
 
unachosema mama ni sahihi, niliwahi kusema kuwa watanzania tuliacha ujamaa kwa kuonjeshwa mshikaki kutoka kwenye mdenge mmoja, tukadhani tungeshiba kwa kula mshikaki mmoja, sio hilo tukaacha na kuchangia michango yetu kule Socialist International (SI). Niliwakumbusha vyama vyote vilivyoacha ujamaa na kufuata ubepari ziliondoka madarakani kwa aibu kubwa. walinielewa na mara ya kwanza ccm walituma wajumbe kwenye mkutano wa SI ujumbe ule uliongozwa na mama Anna Makinda.

Unajua siasa ni kama meli ukitaka kuikata kona lazima iyumbe na nahodha asipokuwa makini basi inaweza piga mweleka na kuzama kama MV Bukoba. Yanayoendelea sasa ya kufufua TRL ATCL na kupiga vita shule na vyuo binafsi ni dalili za kurudi kwenye ujamaa. Nahodha keshaona hawezi kupiga kona kaamua kufuata upepo unakoelekea, sasa hatujui kama anayo dira sahihi ya kutupeleka tunakotaka kwenda.

Mama Anna bado sera yetu ni nchi ya kijamaa (Socialist) Nahodha kapoteza dira tu baada ya meli kuyumba ila anahitaji umakini mkubwa kukata kona na kuchukua usawa stahiki, tunapoona hatuna uelekeo siyo kweli, ni mawimbi tu yamekipiga chombo ubavuni. Ila tukumbuke watu wameshaonja ubepari tayari, wameshaona raha ya kuwa na mali, wameshaona raha ya kunyonya wenzao, wameshaona unaweza iba fedha za dawa mishahara ada za shule ukajengea bar guest house au night club.
Na hapo ndio tatizo lilipo: Kuwa iwe ubepari ama ujamaa, unyonyaji ndio jadi
 
Kwangu kuwapo kwa hiyo migogoro ya ardhi ni ushahidi tosha kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa. Ardhi ni mali ya umma na rais ni mlinzi wa mali hiyo kwa niaba ya wananchi. Pia wananchi wanatambua hivyo kupitia katiba yao ya kijamaa kuwa yeyote aliyepewa ardhi huwa amekodishwa tu. Iwapo kutakuwa kunahaja ya kubadilisha matumizi ya ardhi husika Mh Rais anaweza kubadili matumizi. Kwa kujua hili wananchi wamekuwa wakitumia fursa hiyo. Laiti tusingekuwa na ujamaa hakuna ambaye angethubutu kudai mali ya mtu au taasisi. Hata hao wanaharakati wasingethubutu kufanya hivyo. Chukua mfano Kenya wao wamezoea kuwa wapangaji kwenye ardhi za watu. Husikii kelele kama huku kwetu.
Pia uhusiano wa uzalishaji katika nchi ya Tanzania umekuwa ukitathiminiwa kijamaa kwa kuangalia kuwapo kwa usawa wa kipato miongoni mwa wanajamii ili kusiwepo na pengo kubwa kati ya walionacho na wasionacho. Mataifa ya kibepari huwa hayaangalii hiki kitu survival for the fittest was and still is the rule of the days. Kila mtu atajijua.
Migogoro ya ardhi itamalizwa pale serikali itakapoamua kufifisha ufugaji wa kienyeji kwa njia yoyote itakayotafitiwa na kufaa. Pia kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kuishi makazi yaliyopangwa. Zaidi ya hayo serikali ihuishe sera ya makazi na ihakikishe kunakuwa na makazi ya kutosha kwa kizazi kinachoingia kazini. Kufificha makazi msambao na kuhimiza makazi shadidi.
Ujamaa ulifanikiwa katika nchi gani? Kote ulijojaribiwa ulishindwa kwa kishindo kikuu,ni mfumo wa kufikirika,good only for academics,

Ukitaka nchi hii irudi nyuma miaka 50,leta ujamaa leo, kumiliki mali si kosa,kinachotakiwa ni serikali kukusanya kodi kutoka kwa wenye mali na kuzigawanya kwa kwa kufanya shughuli za maendeleo ambazo zitawanyanyua wasio nacho,mfano elimu,vyuo,n.k

Pia sioni mantiki ya kumfanya mtanzania awe mpangaji kwenye ardhi yake na kupangiwa muda wa umiliki,Leasehold ni mfumo unaopendwa na nchi za kijamaa kwa kuwa zinaruhusu serikali kumiliki kwa niaba ya umma,serikali ndio tajiri,hii wanautumia kwenye ardhi kwa kuita ardhi ni mali ya umma,mfumo wa kijamaa unaamini katika umiliki wa serikali,mfumo wa kijamaa hauamini katika private ownership,lengo lake ni kumfanya mtanzania asiwe na mali, asiwe na kitu,kapuku

Umetoa mfano wa Kenya,kenya katika mradi wa standard gauge,miradi ya barabara,na mingine ya umma,serikali hulipa fidia inapohitaji kuchukua ardhi ya mtu, hivyo hata kwenye Freehold,bado serikali unaweza kuweka kipengele cha kufidia na kuchukua ardhi

Private ownership ya ardhi ni jambo muhimu,hatuwezi kuishi maisha ya kupangishwa katika nchi yetu,ni jambo la aibu kumpa mtanzania hati miliki ya miaka 33 au hata 99
 
Ujamaa ulifanikiwa katika nchi gani? Kote ulijojaribiwa ulishindwa kwa kishindo kikuu,ni mfumo wa kufikirika,good only for academics,

Ukitaka nchi hii irudi nyuma miaka 50,leta ujamaa leo, kumiliki mali si kosa,kinachotakiwa ni serikali kukusanya kodi kutoka kwa wenye mali na kuzigawanya kwa kwa kufanya shughuli za maendeleo ambazo zitawanyanyua wasio nacho,mfano elimu,vyuo,n.k

Pia sioni mantiki ya kumfanya mtanzania awe mpangaji kwenye ardhi yake na kupangiwa muda wa umiliki,Leasehold ni mfumo unaopendwa na nchi za kijamaa kwa kuwa zinaruhusu serikali kumiliki kwa niaba ya umma,serikali ndio tajiri,hii wanautumia kwenye ardhi kwa kuita ardhi ni mali ya umma,mfumo wa kijamaa unaamini katika umiliki wa serikali,mfumo wa kijamaa hauamini katika private ownership,lengo lake ni kumfanya mtanzania asiwe na mali, asiwe na kitu,kapuku

Umetoa mfano wa Kenya,kenya katika mradi wa standard gauge,miradi ya barabara,na mingine ya umma,serikali hulipa fidia inapohitaji kuchukua ardhi ya mtu, hivyo hata kwenye Freehold,bado serikali unaweza kuweka kipengele cha kufidia na kuchukua ardhi

Private ownership ya ardhi ni jambo muhimu,hatuwezi kuishi maisha ya kupangishwa katika nchi yetu,ni jambo la aibu kumpa mtanzania hati miliki ya miaka 33 au hata 99
Tanzania ni moja ya nchi zinazoendelea kwa kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea. nyingine ni China.
Hujawahi kutafakari tabu wanazopata watu wa kawaida kwenye ardhi zimilikiwazo au zaweza milikiwa na watu binafsi. Kupata picha hiyo kidogo soma riwaya ya Nyota ya Rehema utaona adha ya kuwa na ardhi za watu binafsi.
Ardhi kumilikiwa na umma ni uthbitisho tosha kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa ambapo wananchi toka familia za wasio na ardhi wanayomatumaini ya kupata ardhi kisheria. Kwa kenya asiye na ardhi atakuwa mpangaji yeye na kizazi chake kwenye ardhi ya mtu.
Eneo alilokodishwa mwananchi na kuliendeleza likitakiwa kwa matumizi ya umma serikali au taasisi husika hulipa fidia kwa wenye ardhi inayohitajika kwa mujibu wa sheria. Nakushangaa umejua fidia ya kenya na si ya Tanzania.
Tunakwenda vizuri kama nchi katika kuujenga ujamaa. Waliokaririshwa ujamaa ndio wanapata tabu kutafasiri ujamaa wetu. Wengi wanaamini ujamaa ni wa serikali kumiliki njia kuu za uzalishaji mali. Kweli hiyo ni moja ya njia au nmna mojawapo ilitumiwa na nchi za kijamaa kuhakikisha kunakuwa na usawa miongoni mwa wanajamii na hilo ndilo lengo kuu la ujamaa. Baada ya kubainika bila shaka sekta binafsi inaweza kuwa injini ya kuendeleza uchumi,serikali imeweka mazingira mazuri kwa sekta hii kukuwa na kutoa manufaa na usawa kwa umma. Mamlaka za udhibiti wa huduma zimeundwa ili kudhibiti unyonyaji na kuhimiza usawa.
 
Hakyamungu,maandiko mazuri lakini huko Moshi ukiishi kistaarabu kama Meki sadick utatolewa tu Mamangu,wewe muige Bashite na Gambo,imarisha chuki na utengano hapo utaonekana wa maana sana@Anna Mghwira
 
Hakyamungu,maandiko mazuri lakini huko Moshi ukiishi kistaarabu kama Meki sadick utatolewa tu Mamangu,wewe muige Bashite na Gambo,imarisha chuki na utengano hapo utaonekana wa maana sana@Anna Mghwira
Hahahahaaa! Dah! Umeamua kumpa za mbavu mama yetu?
 
Hongera Mama Anna,nakutakia safari njema huko Kilimanjaro.Moja kubwa Uongozi wako utakuwa wakutukuka kama pale utakapotumia UTU wako,Imani yako kwa Mungu na kwako mwenyewe,Upendo kwa jamii unayoenda kuiongoza,ukatende HAKI maana imeandikwa AMANI ni tunda la HAKI,ukiwa na AMANI wewe mwenyewe ndani ya moyo wako basi utaufanya mkoa wa Kilimanjaro zaidi ya Meck Sadick,waweza kuwa mfano kwa wale wanaofikiria Chuki miongoni mwa watanzani ndiyo italeta maendeleo.

Wakristu tunasema UPENDO hauoni maovu,haubagui hausengenyi.Karibu Kilimanjaro
 
Pongeza kwa andiko lako la kina. Ckujua kama upo jamii forum. Kwa umahiri wako upiganie maendeleo ya Mkoa wa Kilimanjaro, ili siku nyingine ukiwa nje ya wadhifa huo uweze kuweka historia. Usilete msuguano, wala kulazimisha uwepo wa chama chako cha ACT na cha ILANI, huku kuna wenyewe.
 
Bourgeoisie hili neno lilikuwa linamsumbua sana mh! Ndugai wakat tunasoma nae A-LEVEL
 
Back
Top Bottom