Tanzania tujitoe Jumuiya ya Madola

DENG XIAOPING

JF-Expert Member
Mar 6, 2022
2,398
2,593
- Habari za muda huu wana jamii wenzangu, natumai ni njema.

- Nilikuwa na dukuduku kuhusu uwepo wa taifa letu la Tanzania Jumuiya ya Madola, dukuduku langu limezaa maswali kadhaa yenye kuhitaji majawabu kutoka kwenu wana jamii wenzangu.

1. Kwanini Taifa la Tanzania lipo Jumuiya ya Madola?

2. Ni faida zipi tunapata kuhusu uwepo wetu Jumuiya ya Madola?

3. Ni hasara zipi tutapata endapo hatuta kuwepo kwenye Jumuiya ya Madola?

4. Tukipima katika mizani faida na hasara za Jumuiya ya Madola kwetu, kipi kitakuwa ni bora kwetu? Tanzania kuendelea kuwepo katika jumuiya ya madola au tujitoe na kuendeleza maisha yetu ya kawaida kama Taifa nje ya Jumuiya ya Madola?

5. Kwa nini taifa la USA na Hongkong (China) hayapo Jumuiya ya Madola?

6. Je, inawezekana kwa njia ya amani member wa Jumuiya ya Madola akitaka kutoka naye akaruhusiwa kufanya hivyo?
commonwealth.jpg

N.b: Karibuni wadau mwenye swali pia anaweza kuongeza swali lake.
 
- Habari za muda huu wana jamii wenzangu , natumai ni njema.

- Nilikuwa na dukuduku kuhusu uwepo wa taifa letu la Tanzania jumuiya ya madola , dukuduku langu limezaa maswali kadhaa yenye kuhitaji majawabu kutoka kwenu wana jamii wenzangu.

1. Kwa nini taifa la Tanzania lipo jumuiya ya madola ?

2. Ni faida zipi tunapata kuhusu uwepo wetu jumuiya ya madola ?

3. Ni hasara zipi tutapata endapo hatupo jumuiya ya madola ?

4. Tukipima katika mizania faida na hasara za jumuiya ya madola kwetu kipi kitakuwa ni bora kwetu Tanzania kuendelea kuwepo katika jumuiya ya madola au tujitoe na kuendeleza maisha yetu ya kawaida kama taifa nje ya jumuiya ya madola ?

5. Kwa nini taifa la U.S.A na Hongkong [ China ] hayapo jumuiya ya madola ?

6. Je inawezekana kwa njia ya amani member wa jumuiya ya madola akitaka kutoka naye akaruhusiwa kufanya hivyo ?
View attachment 2353028
N.b: Karibuni wadau mwenye swali pia anaweza kuongeza swali lake.
Pumba tupu
 
Aliyetutoka angejitutumua. Tuliye naye anatokea sehemu wanaoamini kwamba mdhungu na Mwarabu ndo wenye uwezo wa kutumia rasilimali za Mwafrika ila Mwafrika mwenyewe hawezi kujiendeleza kwa kutumia rasilimali zake.
Sawa.
 
Swali zuri lkn majibu ya watu ni takataka, ndiomaana tunasema JF imebadirika sana tofauti na hapo mwanzo, ambapo hakukuwa na wahuni wa kileo ambao hawajui kushusha hoja za mtoa mada zaid ya kutukana, kukashifu, kudharau na kuleta matani ya kijinga ila hao hao wapuuzi utawaona kwenye maswala ya kipumbavu kama mpira na udaku jinsi wanavyoweka attention.

Kuna ulazima wa hawa mods kufunga baadhi ya ID humu ambazo hazina maana
 
♦️ Kuanzia katiba tuliyo nayo nasheia zoye tunazotumia zimetungwa na huyo MADOLA ambaye leo hauoni umuhimu wake

♦️ Ndiye huyo huyo madola alitotoa kwwnye ukoloni na alitulea na kutufunza mpaka tukapata uzoefu akatukabidhi nchi yetu kwa amani
Katiba imetungwa 1977, Harakati za kudai uhuru zilianza toka utawala wa Ujerumani Chifu Abushiri, Mkwawa , Kinjekitile n.k awamu ya pili chini ya mkoloni muingereza baada ya vita vya pili vya dunia 1939-1945 harakati za kudai Uhuru zikarudi tena miaka ya 1950 s. 1953 TAA, 1954 TANU Mwalimu , Bibi Titi Mohammed, Abdulhman sykes n.k wakalianzisha varangati la kumng'ang'niza mkoloni muingereza awape uhuru, Mwalimu akawekwa rumande kwa kosa la kujihusisha na siasa wakati wa ukoloni hasa hasa siasa za harakati za ukombozi wa Tanganyika kitu kilicho kuwa kimepigwa marufuku na mkoloni muingereza . 1961 tukapata Uhuru wa masharti/Uhuru wa bendera. Ningependa ujibu maswali yangu niliyo uliza.

N.b: Uhuru hatukupewa kama mama ampatiavyo mwanaye pipi.
 
Yasome vizuri maswali yangu 6 yameligusia pia hilo swali lako . ambalo natumai majawabu yake tutapata kutoka kwa wadau wa humu Jf.
Hujajibu swali; kumwambia mtu asome tena post yako huku alishaisoma na akakuta pumba tupu ni kutwanga maji ndani ya kinu. Kama unadhani ni vizuri kujitoa kwenye Jumuia ya madola weka sababu za msingi kujadiliwa siyo kuandika vijiswali visivyokuwa na mkia wala miguu.
 
Back
Top Bottom