Mabibi na mabwana kutokea taarifa za habari jana na pia baada ya kujiridhisha:
He! Kumbe yule mgeni wetu mpendwa kabisa, mwalikwa tokea pande za pale Burundi aliingizana nchini kwa kutumia moja ya madege yetu yale mapya mapya ya ATCL chapa ya twiga?
Ikizingatiwa uwanja wa ndege Bujumbura ungali umefungwa kutokana na yale mambo yetu ya kujicoronize, yaonyesha dege letu lile lilifanya safari mahsusi kwa ajili ya kutuletea ugeni ule ugeni wetu.
Kweli mgeni njoo, wenyeji tupone. Tunasubiri.
Ama kwa hakika tunayo sababu ya kutembea kifua mbele kwa kuwa na uwezo wa kuwazukia wageni wetu huko huko waliko na kuanza kuwakaribu tokea makwao.
Hatuko vibaya. Mambo yetu kama uraya uraya vile!
Nani kama sisi?
Naamini yule amekuja kwa hisani yetu.
Hakulipa hata ndururu!
He! Kumbe yule mgeni wetu mpendwa kabisa, mwalikwa tokea pande za pale Burundi aliingizana nchini kwa kutumia moja ya madege yetu yale mapya mapya ya ATCL chapa ya twiga?
Ikizingatiwa uwanja wa ndege Bujumbura ungali umefungwa kutokana na yale mambo yetu ya kujicoronize, yaonyesha dege letu lile lilifanya safari mahsusi kwa ajili ya kutuletea ugeni ule ugeni wetu.
Kweli mgeni njoo, wenyeji tupone. Tunasubiri.
Ama kwa hakika tunayo sababu ya kutembea kifua mbele kwa kuwa na uwezo wa kuwazukia wageni wetu huko huko waliko na kuanza kuwakaribu tokea makwao.
Hatuko vibaya. Mambo yetu kama uraya uraya vile!
Nani kama sisi?
Naamini yule amekuja kwa hisani yetu.
Hakulipa hata ndururu!