Tanzania & Romania Zatia Saini Mikataba ya Ushirikiano

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944

Tanzania & Romania Zatia Saini Mikataba ya Ushirikiano

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Romania Mhe. Klaus Iohannis wakati wakishuhudia utiaji saini wa Mikataba mbalimbali ya ushirikiano baina ya nchi hizo iliyotiwa saini na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama, na Waziri wa nchi wa masuala ya Dunia na Mikakati ya Kidiplomasia wa Romania Mhe. Traian - Laurentiu Hristea kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, 17 Novemba, 2023.

"Uhusiano wa Romania na Tanzania ulianza May 1964 yaani mwezi mmoja tu baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Romania imekuwa Mbia wetu kama Nchi na kama Nchi Mwanachama wa Umoja wa Ulaya hivyo ni dhamira yetu kuendelea kudumisha umoja huu" - Rais Samia Suluhu Hassan

"Tumezungumzia wigo wa kuongeza ufadhili wa masomo hususani kwenye fani za Udaktari na Ufamasia, pia katika kudumisha uhusiano Romania imekubali kwa mwaka huu kutoa nafasi 10 za masomo kwa Watanzania katika maeneo tutakayoyachagua" - Rais Samia Suluhu Hassan
 

Attachments

  • F_IdQBvXEAAkUiV.jpg
    F_IdQBvXEAAkUiV.jpg
    348.5 KB · Views: 3
  • F_Ie8_FXsAEFYAQ.jpg
    F_Ie8_FXsAEFYAQ.jpg
    341.4 KB · Views: 4
  • F_Icb9vX0AAmMzA.jpg
    F_Icb9vX0AAmMzA.jpg
    412.5 KB · Views: 2
  • F_IF2m8XYAAo9AP.jpg
    F_IF2m8XYAAo9AP.jpg
    230 KB · Views: 2
  • F_Ifp8KXwAAoI6k.jpg
    F_Ifp8KXwAAoI6k.jpg
    71.4 KB · Views: 3
Hii mikataba inasainiwa tangu nikiwa mdogo mpaka nakua mzee sijawahi nufaika na hata mmoja.

Hivi wakuu kuna ambaye yeye kanufaika na mkataba hata mmoja.

Halafu nasikia tu kuna keki ya Taifa na watu wanaila jamani hiyo keki iko wapi na mimi nileee?
 
Hii mikataba inasainiwa tangu nikiwa mdogo mpaka nakua mzee sijawahi nufaika na hata mmoja.

Hivi wakuu kuna ambaye yeye kanufaika na mkataba hata mmoja.

Halafu nasikia tu kuna keki ya Taifa na watu wanaila jamani hiyo keki iko wapi na mimi nileee?
Tumuite Saint Anne ye ndio mtaalamu haswaa wa keki, huenda alipata oda ya keki ya taifa akaipika, atakuwa anawajua waliomuagiza.
 
Hii mikataba inasainiwa tangu nikiwa mdogo mpaka nakua mzee sijawahi nufaika na hata mmoja.

Hivi wakuu kuna ambaye yeye kanufaika na mkataba hata mmoja.

Halafu nasikia tu kuna keki ya Taifa na watu wanaila jamani hiyo keki iko wapi na mimi nileee?
Mikataba ni ya nchi sio wewe na nyumba yako Mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom