MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,564
- 849
- Thread starter
-
- #181
Nina maswali kuhusu Dr.Salim:Hivi amesha deliver nini hasa kwa taifa hili mpaka kuonekana anafaa sana kuwa Rais,mpaka Nyerere kumbembeleza mara kibao as if hakuna wengine capable kumshinda?
Kama Dr.Salim angeukwaa huo Urais tuseme 1985 au 1995 ama 2005,je bongo sasa tungekuwa tunacheza na GDP per capita ya Botswana,Namibia au hata Kenya ama tungekuwa kama Wasomali tu?
Inaelekea Dr.Salim ni arrogant na alijihisi kuwa yuko overqualified kwa nafasi ya Urais wa Tanzania au alikuwa hataki au hana nia hasa ya kuwa Rais wa Tanzania.
Kama alikuwa anajua kuwa Wazanzibari wenzake hawamtaki,iweje akatae Urais wa 'kupewa mezani' na Nyerere,kisha ghafla tu autake Urais huohuo 2005,wakati Nyerere ambaye angeweza kumbeba hakuwepo?
Naweza nikasahihishwa kwenye hili ila kwangu mimi naona CY ya Dr. Salim Ahmed Salim imeng'arishwa zaidi na vyeo alivyo shika badala ya nini alifanya katika hivyo vyeo. Mfano Sokoine anakubwa kwa yale aliyo yafanya akiwa waziri mkuu nk. ila kwa Salim sioni hili. Pia kutokana na uelewa wangu Salim amelaumiwa sana na Watanzania wengi pale OAU kwa kuto kusaidia Watanzania kupata nafasi za kazi mbali mbali. Nikisema kusaidia simaanishi kuwafanyia upendeleo bali inasemekana alikwenda a step ahead na kama kuhakikisha ana wazibia oppportunity Watanzania. Naomba nisahihishwe ikibidi.
Labda alikua na ndoto ya A STAR SHINING ON THE DARK.
Kuna mambo mawili ninayoyafahamu yaliyompelekea Mwalimu kumpenda Salim. Kitu cha kwanza ni uchapa kazi. Salim alikuwa akipewa assignment na Mwalimu, mathalan amekwenda ziara ya nje, akirudi alikuwa anahakikisha siku hiyo hiyo Mwalimu anapata ripoti kamili.Naweza nikasahihishwa kwenye hili ila kwangu mimi naona CY ya Dr. Salim Ahmed Salim imeng'arishwa zaidi na vyeo alivyo shika badala ya nini alifanya katika hivyo vyeo. Mfano Sokoine anakubwa kwa yale aliyo yafanya akiwa waziri mkuu nk. ila kwa Salim sioni hili. Pia kutokana na uelewa wangu Salim amelaumiwa sana na Watanzania wengi pale OAU kwa kuto kusaidia Watanzania kupata nafasi za kazi mbali mbali. Nikisema kusaidia simaanishi kuwafanyia upendeleo bali inasemekana alikwenda a step ahead na kama kuhakikisha ana wazibia oppportunity Watanzania. Naomba nisahihishwe ikibidi.
hata mimi nimeshangaa The boss, da! Ni noma.Kaka umejuaje yote hayo? Au ulishiriki kwenye mchakato mzima?
Labda tuanzie pale Nyerere aliposema kuwa "serikali inanuka." Ilifika wakati wafadhili waligoma kuisaidia Tanzania kwa sababu serikali ya Mwinyi ilikuwa haikusanyi kodi.Kwa hiyo mkuu pamoja na kuwa "second option" Nyerere alimuamini sana Mkapa kwa sababu kwa uelewa wangu (naomba kusahihishwa), Nyerere alikua too involved na serikali ya Mwinyi in terms of kuinfluence baraza na decision making. Je ni kweli hakumuamini Mwinyi (kwenye uwezo wa kuongoza) lakini akamuamini Mkapa? Au aliona alikua too involved na serikali ya Mwinyi akajifunza na kuamua kumuachia Mkapa maamuzi yote?
Ila kuna kingine kina nitatiza mkuu. Wengi wanadai Nyerere kumpenda Mkapa ni kwa sababu ya Ukatoliki wao. Sasa hawa watu wanaelezeaje kuwa first choice ya mzee alikua SALIMA AHMED SALIM?
Jasusi, hivi umewahi kufanya mahojiano na Nyerere?Labda tuanzie pale Nyerere aliposema kuwa "serikali inanuka." Ilifika wakati wafadhili waligoma kuisaidia Tanzania kwa sababu serikali ya Mwinyi ilikuwa haikusanyi kodi.
Na mara kwa mara Nyerere alipokuwa anasafiri nje alikuwa anasikia malalamiko mengi kuhusu utendaji wa serikali yetu. Nakumbuka ilipotokea scandal ya Mbilinyi. Nyerere alikuwa New York wakati huo. Nikapata nafasi ya kuonana naye. Alisema kuwa hata kama si kweli kwamba Mbilinyi amechukua hela za kampuni ya samaki, ni lazima ajiuzulu kwa sababu ya kuonyesha kuwa serikali mpya haitavumilia tena mambo ya rushwa.
So he was very proud of Mkapa's performance, pale alipoanza kukusanya kodi na hela mitaani zikaisha, Waswahili wakakiita kipindi chake kipindi cha ukapa. Mwalimu aliamini kabisa kuwa sifa za Tanzania katika nchi za nje zitarejeshwa na utendaji wa Mkapa.
Yes, on Burundi, wakati huo akiwa mpatanishi. Alipokuwa rais alikuwa mgumu sana kutoa interviews.Jasusi, hivi umewahi kufanya mahojiano na Nyerere?
Jasusi,Mwanafalsafa1,
..kwa upande mwingine ni vigumu kwa Mtanzania wa kawaida ku-appreciate mchango waziri wa Mambo ya Nje.
..inawezekana kabisa Salim Salim angetumikia ktk wizara kama ya Ujenzi au Kilimo basi tungeweza kuwa jambo la kusema kuhusu mchango wake kwa wa-Tanzania wa kawaida.
..binafsi I did not support his candidacy kwasababu nilikuwa naona ni mtu ambaye hakuwa seasoned enough ktk kushughulikia matatizo ya ndani, kama ya nchi hii.
The Boss said:wewe jifunze historia vizuri
salim aliwahi kuwa waziri wa ulinzi
na aliheshimika mno na jeshi
sio kila waziri hasa kutoka zanzibar anae weza kukubalika na kuheshimi na jeshi
na alipokuwa waziri mkuu,akapendwa mno na watu
na uliza waziri ganimkuu alie pendwa na watu zaoidi ya salim na sokoine????
The Boss,
..kama una taarifa zinazohusu rekodi na utendaji wa Salim Salim akiwa Waziri Mkuu, au alipokuwa Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Ulinzi na JKT, unaweza kuziweka hapa.
..habari za mitaani ni kwamba wanajeshi walimpenda sana Salim Salim kwasababu walikuwa na shida ya usafiri na yeye akaweza kwenda Uarabuni na kuleta magari ya msaada. wengine wanakwenda mbali na kumsifia kwa kudai kwamba magari hayo alipewa binafsi lakini kutokana na roho ya upendo aliyokuwa nayo akawagawia yote wanajeshi.
..pia kuna habari nyingine kwamba Salim Salim alikwenda mikoa ya kusini na kukuta wananchi wanashida kubwa ya chakula na mavazi. inasemekana alikuta wananchi wanakula mizizi na kuvaa kaniki. sasa ili kutatua tatizo hilo Salim Salim akaagiza wapewe nguo za mitumba.
..pamoja na kwamba maamuzi hayo yalikuwa ni mazuri na yenye msaada kwa wananchi, lakini sidhani kama yanatosha kumfanya mhusika afikiriwe kwa madaraka makubwa zaidi kama Raisi.
NB:
..binafsi ningemkubali Salim Salim kama angeweza kuja na program ya kilimo mikoa ya kusini ili wananchi wasikumbwe tena na tatizo la njaa. inaelekea baada ya kuwapa chakula cha msaada na nguo za mitumba na yeye kusifiwa magazetini basi wananchi wale wa kusini wamesahauliwa.
Joka Kuu,The Boss,
..kama una taarifa zinazohusu rekodi na utendaji wa Salim Salim akiwa Waziri Mkuu, au alipokuwa Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Ulinzi na JKT, unaweza kuziweka hapa.
..habari za mitaani ni kwamba wanajeshi walimpenda sana Salim Salim kwasababu walikuwa na shida ya usafiri na yeye akaweza kwenda Uarabuni na kuleta magari ya msaada. wengine wanakwenda mbali na kumsifia kwa kudai kwamba magari hayo alipewa binafsi lakini kutokana na roho ya upendo aliyokuwa nayo akawagawia yote wanajeshi.
..pia kuna habari nyingine kwamba Salim Salim alikwenda mikoa ya kusini na kukuta wananchi wanashida kubwa ya chakula na mavazi. inasemekana alikuta wananchi wanakula mizizi na kuvaa kaniki. sasa ili kutatua tatizo hilo Salim Salim akaagiza wapewe nguo za mitumba.
..pamoja na kwamba maamuzi hayo yalikuwa ni mazuri na yenye msaada kwa wananchi, lakini sidhani kama yanatosha kumfanya mhusika afikiriwe kwa madaraka makubwa zaidi kama Raisi.
NB:
..binafsi ningemkubali Salim Salim kama angeweza kuja na program ya kilimo mikoa ya kusini ili wananchi wasikumbwe tena na tatizo la njaa. inaelekea baada ya kuwapa chakula cha msaada na nguo za mitumba na yeye kusifiwa magazetini basi wananchi wale wa kusini wamesahauliwa.