Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,400
Nchi zaidi ya 50 nyingi za kutoka mabara ya Afrika na Asia zimo katika orodha iiwtayo "RED LIST",
Orodha hiyo iliwekwa kwa zile nchi ambazo hazitoi takwimu za kuridhisha juu ya idadi ya watu waloambikizwa ugonjwa wa Covid-19 na pia idadi ya vifo vilivyotokana na maambukizi ya ugonjwa huo.
Uamuzi wa kuweka orodha kulingana na nchi zinazofuata masharti ya kutoa takwimu na zile zinazojikongoja ulitolewa tarehe 8 June 2021 na baada ya hapo ipo orodha ya kijani, orodha ya njano na orodha nyekundu.
Orodha ya kijani inaruhusu wafasiri kutoka nchi zilizo katika orodha hiyo kupita na kuingia katika nchi hususan za Ulaya kama Uingereza, Ujerumani na zingine na kwenda nyumbani moja kwa moja (kama amechomwa sindano mbili za chanjo) bila kukaa karantini, ingawa msafiri atatakiwa kufanya test masaa 72 kabla ya safari na anapotua Ulaya siku ya kwanza au ya pili.
Raia kutoka nchi zilizo katika orodha ya njano wanapoingia barani Ulaya wanapaswa (kama wamechomwa chanjo mbili) kufanya test siku tatu kabla ya safari na mara wanapoingia Ulaya hutakiwa kufanya test siku wanapofika na wiki inayofuata lakini bila kukaa karantini lakini watapaswa kujitenga nyumbani kwa siku 10.
Raia wa kutoka nchi zilizo katika orodha nyekundu (hata kama wamechoma sindano mbili za chanjo) wanatakiwa kuchukua vipimo masaa 72 kabla ya safari na watapofika Ulaya watapaswa kukaa karantini hotelini (iliyoidhinishwa na serikali) kwa siku 10 na kulipa gharama ya dola 2,409 hivi huku wakichukuliwa vipimo siku ya pili baada ya kufika na siku nane baadae.
Hivyo kwa hesabu za harakaharaka mtanzania anaetaka kusafiri kwenda barani Ulaya anatakiwa juu ya nauli yake awe na hiyo dola 2409.
Tanzania iliingizwa katika orodha nyekundu yaani "RED LIST" mwezi Mei mwaka 2021 kwa sababu za kujikongoja kwenye suala la utoaji chanjo na taarifa za wagonjwa wa Covid na vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.
Serikali iloongozwa na hayati John Magufuli iliacha kutoa taarifa hizo katika shirika la Afya duniani mapema mwaka 2020
Hayati Magufuli alitangazwa kuwa amefariki tarehe 17 mwezi March mwaka huu sababu za kifo zake zikielezwa kuwa ni ugonjwa wa moyo.
Hadi leo hii, kwa mujibu wa WHO taarifa ya idadi ya watanzania waloambukizwa ugonjwa wa Covid -19 ni 509 na vifo 21 taarifa ambazo zilitolewa na Tanzania mwezi March 2020.
Lakini serikali ya awamu ya sita imechukua hatua kadhaa za kuonyesha kuwa Tanzania inaungana na jukwaa la kimataifa kwa kujiunga rasmi na mfuko wa COVAX ambao ni mfuko unosaidia nchi kadhaa kutoa chanjo kwa njia ya mkopo.
COVAX kirefu chake ni Covid-19 Vaccine Global Access ni mfumo ambayo nchi zenye uchumi wa kati na wa chini zinapewa uwezo wa kupata idadi kadhaa ya chanjo kwa bei nafuu ambayo huwa ni kwa makubaliano maalum.
Pia mfumo huu wa COVAX waitwa COVAX Vaccine Advance Market Commitment) financing instrument.
Kupitia mpango huu aina mbili ya dawa za chanjo za Pfizer-BioTech, Oxford Astra Zeneca zimeweza kusambazwa katika nchi kadhaa zikiwemop Ghana, Ivory Coast,Serbia, Slovenia, Romania na nchi zingine zenye uchumi wa kati au chini ya hapo.
Hadi kufikia mwezi Julai 2020 nchi zipatazo 165 zilikuwa zimejiunga na mfuko huu.
Serikali ya Tanzania bado imeendelea kusuasua na haijaonyesha kujitahidi kuhakikisha taarifa zote zinazohusiana na ugonjwa wa Covid zinafika WHO kwa ufuatiliaji na angalau kuanza kufikiriwa kusogezwa juu katika orodha angalau ya njano.
Hata hivyo zoezi la kukusanya taarifa za ugonjwa wa Covid -19 zahitaji umakini mkubwa na watu waaminifu kwani linahusiaha mstakabali wa nchi kiusalama na kiuchumi.
Pia zoezi hili linahitaji kiwango cha juu cha kuhakikisha vipimo vinachukuliwa, na kuripotiwa, aina ya virusi vya Covid -19 vinavyotambuliwa au kugunduliwa na mwisho ni aina ipi ya chanjo ambayo yafaa kupambana na virusi au kirusi hicho.
Vyuo vikuu na mahospitali makubwa kama Muhimbili huu ndo ulitakiwa kuwa muda kuwa wapo "busy" wafanya uchambuzi wa taarifa na kuweka jopo la madaktari maalum kwa kumshauri raisi na serikali.
Hivyo "coordination" hiyo ambayo pia itawashirikisha waganga wakuu wa mikoa, maofisa wa afya na madaktari waandamizi inakuwa inaipa sifa nchi kuwa imekomaa katika masuala ya afya na imesomesha watu makini na ada haikwenda bure.
Hata kama leo hii serikali ya Tanzania ikiamua kuanza kazi basi itachukua si chini ya miezi mitatu kufanya mambo yote niliyoyataja hapo juu na pengine kuishia njiani.
Hali hii imesababisha wasafiri wengi wa kitanzania na wale walo na mahusiano ya karibu na nchi hiyo kuwa na wakti mgumu katika kutimiza masharti yalowekwa ya karantini hotelini na kujilipia dola 2409.
Pia wanafunzi wanotaka kwenda barani Ulaya kwa muhula wa masomo wa kuanzia mwezi September mwaka huu itabidi wajiandae na gharama za safari hiyo.
Huu ndo wasiwasi wa nchi za Ulaya katika kuruhusu raia wa nchi za kiafrika kufika nyumbani moja kwa moja wanaposafiri kwenda katika nchi zao na kuwataka kwanza kukaa hotelini na kulipia kwa siku 10 dola 2409.
Kwa kifupi twaweza sema kuwa Tanzania imewekwa kwenye orodha nyekundu "indefinetely".
Hiyo ni kwasababu raisi Samia amegoma kuendelea kutoa taarifa WHO kwa kuogopa wafuasi wa hayati Magufuli lakini huku wakificha idadi halisi ya watu walokufa kwa ugonjwa wa huu idadi ambayo ikitamkwa leo hii ardhi nzima ya Tanzania itapasuka.
Hivyo tegemeo pekee ni kuingojea nchi za wenyewe za wala mayai kuamua kuiondoa Tanzania kutoka kwenye orodha nyekundu na kuisogeza juu kulingana na hali na hali hiyo inatarajiwa kuwa ni kuanzia mwezi September mwaka huu.
Tayari ilitangazwa kuwa kutaundwa tume ambayo iliundwa na ikaja na mapendekezo yake, pia kwamba Tanzania ilikwishjiunga rasmi na mfumo wa COVAX.
Lakini je, Serikali ya Tanzania ipo serious katika kuhakikisha tunashirikiana na vyombo na majukwaa ya kimataifa katika kubadilishana taarifa hizi muhimu zinazohusiana na ugonjwa huu wa Covid-19 ambao nchi nyini sasa zimekubali kuwa hautatoweka leo?
Natoa wito kwa serikali kufikiria kwa makini mwenendo wake katika kushughulikia suala hili nyeti kwa taifa.
Orodha hiyo iliwekwa kwa zile nchi ambazo hazitoi takwimu za kuridhisha juu ya idadi ya watu waloambikizwa ugonjwa wa Covid-19 na pia idadi ya vifo vilivyotokana na maambukizi ya ugonjwa huo.
Uamuzi wa kuweka orodha kulingana na nchi zinazofuata masharti ya kutoa takwimu na zile zinazojikongoja ulitolewa tarehe 8 June 2021 na baada ya hapo ipo orodha ya kijani, orodha ya njano na orodha nyekundu.
Orodha ya kijani inaruhusu wafasiri kutoka nchi zilizo katika orodha hiyo kupita na kuingia katika nchi hususan za Ulaya kama Uingereza, Ujerumani na zingine na kwenda nyumbani moja kwa moja (kama amechomwa sindano mbili za chanjo) bila kukaa karantini, ingawa msafiri atatakiwa kufanya test masaa 72 kabla ya safari na anapotua Ulaya siku ya kwanza au ya pili.
Raia kutoka nchi zilizo katika orodha ya njano wanapoingia barani Ulaya wanapaswa (kama wamechomwa chanjo mbili) kufanya test siku tatu kabla ya safari na mara wanapoingia Ulaya hutakiwa kufanya test siku wanapofika na wiki inayofuata lakini bila kukaa karantini lakini watapaswa kujitenga nyumbani kwa siku 10.
Raia wa kutoka nchi zilizo katika orodha nyekundu (hata kama wamechoma sindano mbili za chanjo) wanatakiwa kuchukua vipimo masaa 72 kabla ya safari na watapofika Ulaya watapaswa kukaa karantini hotelini (iliyoidhinishwa na serikali) kwa siku 10 na kulipa gharama ya dola 2,409 hivi huku wakichukuliwa vipimo siku ya pili baada ya kufika na siku nane baadae.
Hivyo kwa hesabu za harakaharaka mtanzania anaetaka kusafiri kwenda barani Ulaya anatakiwa juu ya nauli yake awe na hiyo dola 2409.
Tanzania iliingizwa katika orodha nyekundu yaani "RED LIST" mwezi Mei mwaka 2021 kwa sababu za kujikongoja kwenye suala la utoaji chanjo na taarifa za wagonjwa wa Covid na vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.
Serikali iloongozwa na hayati John Magufuli iliacha kutoa taarifa hizo katika shirika la Afya duniani mapema mwaka 2020
Hayati Magufuli alitangazwa kuwa amefariki tarehe 17 mwezi March mwaka huu sababu za kifo zake zikielezwa kuwa ni ugonjwa wa moyo.
Hadi leo hii, kwa mujibu wa WHO taarifa ya idadi ya watanzania waloambukizwa ugonjwa wa Covid -19 ni 509 na vifo 21 taarifa ambazo zilitolewa na Tanzania mwezi March 2020.
Lakini serikali ya awamu ya sita imechukua hatua kadhaa za kuonyesha kuwa Tanzania inaungana na jukwaa la kimataifa kwa kujiunga rasmi na mfuko wa COVAX ambao ni mfuko unosaidia nchi kadhaa kutoa chanjo kwa njia ya mkopo.
COVAX kirefu chake ni Covid-19 Vaccine Global Access ni mfumo ambayo nchi zenye uchumi wa kati na wa chini zinapewa uwezo wa kupata idadi kadhaa ya chanjo kwa bei nafuu ambayo huwa ni kwa makubaliano maalum.
Pia mfumo huu wa COVAX waitwa COVAX Vaccine Advance Market Commitment) financing instrument.
Kupitia mpango huu aina mbili ya dawa za chanjo za Pfizer-BioTech, Oxford Astra Zeneca zimeweza kusambazwa katika nchi kadhaa zikiwemop Ghana, Ivory Coast,Serbia, Slovenia, Romania na nchi zingine zenye uchumi wa kati au chini ya hapo.
Hadi kufikia mwezi Julai 2020 nchi zipatazo 165 zilikuwa zimejiunga na mfuko huu.
Serikali ya Tanzania bado imeendelea kusuasua na haijaonyesha kujitahidi kuhakikisha taarifa zote zinazohusiana na ugonjwa wa Covid zinafika WHO kwa ufuatiliaji na angalau kuanza kufikiriwa kusogezwa juu katika orodha angalau ya njano.
Hata hivyo zoezi la kukusanya taarifa za ugonjwa wa Covid -19 zahitaji umakini mkubwa na watu waaminifu kwani linahusiaha mstakabali wa nchi kiusalama na kiuchumi.
Pia zoezi hili linahitaji kiwango cha juu cha kuhakikisha vipimo vinachukuliwa, na kuripotiwa, aina ya virusi vya Covid -19 vinavyotambuliwa au kugunduliwa na mwisho ni aina ipi ya chanjo ambayo yafaa kupambana na virusi au kirusi hicho.
Vyuo vikuu na mahospitali makubwa kama Muhimbili huu ndo ulitakiwa kuwa muda kuwa wapo "busy" wafanya uchambuzi wa taarifa na kuweka jopo la madaktari maalum kwa kumshauri raisi na serikali.
Hivyo "coordination" hiyo ambayo pia itawashirikisha waganga wakuu wa mikoa, maofisa wa afya na madaktari waandamizi inakuwa inaipa sifa nchi kuwa imekomaa katika masuala ya afya na imesomesha watu makini na ada haikwenda bure.
Hata kama leo hii serikali ya Tanzania ikiamua kuanza kazi basi itachukua si chini ya miezi mitatu kufanya mambo yote niliyoyataja hapo juu na pengine kuishia njiani.
Hali hii imesababisha wasafiri wengi wa kitanzania na wale walo na mahusiano ya karibu na nchi hiyo kuwa na wakti mgumu katika kutimiza masharti yalowekwa ya karantini hotelini na kujilipia dola 2409.
Pia wanafunzi wanotaka kwenda barani Ulaya kwa muhula wa masomo wa kuanzia mwezi September mwaka huu itabidi wajiandae na gharama za safari hiyo.
Huu ndo wasiwasi wa nchi za Ulaya katika kuruhusu raia wa nchi za kiafrika kufika nyumbani moja kwa moja wanaposafiri kwenda katika nchi zao na kuwataka kwanza kukaa hotelini na kulipia kwa siku 10 dola 2409.
Kwa kifupi twaweza sema kuwa Tanzania imewekwa kwenye orodha nyekundu "indefinetely".
Hiyo ni kwasababu raisi Samia amegoma kuendelea kutoa taarifa WHO kwa kuogopa wafuasi wa hayati Magufuli lakini huku wakificha idadi halisi ya watu walokufa kwa ugonjwa wa huu idadi ambayo ikitamkwa leo hii ardhi nzima ya Tanzania itapasuka.
Hivyo tegemeo pekee ni kuingojea nchi za wenyewe za wala mayai kuamua kuiondoa Tanzania kutoka kwenye orodha nyekundu na kuisogeza juu kulingana na hali na hali hiyo inatarajiwa kuwa ni kuanzia mwezi September mwaka huu.
Tayari ilitangazwa kuwa kutaundwa tume ambayo iliundwa na ikaja na mapendekezo yake, pia kwamba Tanzania ilikwishjiunga rasmi na mfumo wa COVAX.
Lakini je, Serikali ya Tanzania ipo serious katika kuhakikisha tunashirikiana na vyombo na majukwaa ya kimataifa katika kubadilishana taarifa hizi muhimu zinazohusiana na ugonjwa huu wa Covid-19 ambao nchi nyini sasa zimekubali kuwa hautatoweka leo?
Natoa wito kwa serikali kufikiria kwa makini mwenendo wake katika kushughulikia suala hili nyeti kwa taifa.