beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Tanzania inatarajia kupokea Dozi 500,000 za Chanjo dhidi ya COVID19 ya Pfizer kupitia Mpango wa COVAX. Imeelezwa, Dozi hizo zitachanjwa mara mbili
Akitoa Taarifa ya Wiki Jijini Mwanza amesema, "Hizi Pfizer ni sehemu ya Chanjo Dozi 3,700,000 ambazo zitaletwa na COVAX Facility. Mwisho wa mwezi huu zitakuja hizo laki tano, lakini awamu kwa awamu zitaendelea kuja zingine"
Aidha, amesema hadi kufikia Oktoba 15, 2021 Watanzania zaidi ya 940,000 walishapata Chanjo
Akitoa Taarifa ya Wiki Jijini Mwanza amesema, "Hizi Pfizer ni sehemu ya Chanjo Dozi 3,700,000 ambazo zitaletwa na COVAX Facility. Mwisho wa mwezi huu zitakuja hizo laki tano, lakini awamu kwa awamu zitaendelea kuja zingine"
Aidha, amesema hadi kufikia Oktoba 15, 2021 Watanzania zaidi ya 940,000 walishapata Chanjo