Tanzania kupeleka battalion moja Congo

Tanzania kupeleka battalion moja Congo

usiwaze kodi tunayotoa kumbuka amani inayopatikana inatoka wapi wenzako hawalali wanalinda mipaka kwa ajili yako wewe unaofanya biashara na kupulizwa upepo ikitokea vita watakaofaidi ni wanajeshi pekee wengine ni vilio tu mwanzo mwisho

kwa kuongezea pia sifikiri kuwa uwapo wa majeshi yetu kule ni matumizi ya kodi zetu zaidi sana tanzania italipwa fedha nyingi sana na Un kwa kupeleka majeshi kule ni sawa na mchezo wa pira kwamba wanajeshi wetu tuawauza kwa timu nyingine.

Pia iwao tutafanikiwa katika hiyo mision pamoja na sifa kwa Un wenyewe lakini pia ni sifa kwetu sisi kama taifa, pia tunawaongezea ujuzi wanajeshi wetu wote
mfano mzuri ni wale wanajeshi waliopigana kwenye vita vya Uganda waliijengea heshima nchi na walitizamwa kama wenye uzoefu zaidi kila mara sifa yao kubwa ilikuwa kuwa tulipigana vita ya uganda.

Tunajua kuwa haya ni maswala ya kimataifa zaidi hata South Afrika walipeleka majeshi yao huko Frika ya kati na wameuliwa kwa wingi sana leo hii wako kwenye maombolezo ya kitaifa pamoja na kwamba Raisi Zuma amekuwa akilaumiwa na wananchi wake kwa kupeleka majeshi huko lakini iwapo wangerudi salama na ushindi wa mission iliyowapeleka nafikiri Watu wa AFrika kusini wote wangejivunia hilo kuwa jeshi lao walau limeweza kutekeleza majukumu yao kitaifa na kimataifa na Rank ya S. Afrika kijeshi ingetazamwa kwa namana ya tofauti na sasa.

Yote sawa ikiwa tunaweza kufanya majukumu ya kitaifa na kimataifa basi na tuyafanye kwa maslai ya taifa na dunia kwa ujumla.

Kupatikanba kwa amani ya Congo ni jukumu letu sote na ninafikiri hapa UN wameona ni bora sasa kubadili na kuwa na Offensive Mandateto attack kuliko kujilinda kwakuwa na hawa waasi nao wamekuwa wakitumia njia hiyo kuongeza ujeuri sasa utaona silaa za waasi zitaanza kuwekwa chini kwa haraka sana yaani vikosi vya UN vikiingia tu kwenye nchi itabidi waasi wajisalimishe na kwa njia hii vita itakuwa raisi na haitatumia gharama kubwa na kutakuwa na kipindi cha mpito cha kuhakikisha amani na utulivu
 
nimewahi soma mahali kuwa kuna waasi wa congo wanasaidiwa na rwanda kivifaa etc. sasa kama rwanda inapitishia silaha zake bandarin kwetu na sehemu ya silaha hizo inawapa hao waasi tpdf itakao pambana nao inakuwaje? yaani adui tunampa silaha apambane na sisi? rwanda na uganda zinachangia matatzo ya congo
 
Mungu ibariki Tanzania. Ibariki JWTZ. Uzalendo kwanza mengine baadae
 
Hiyo ni Force keeping mission sio piece keeping mission,kuna jamaa angu yupo morogoro toka mwaka jana mwezi wa nane wanajiandaa kwa ajili ya hiyo mission.
 
Kwa umoja wa africa ulipoomba tupeleke jeshi Anjoun Comoro tulitumia muda gani pale kulirudisha jimbo na ni idadi ya wanajeshi wangapi walipoteza maisha?
 
Watanzania wenzangu hasara tuliyo pata kwa kuwatunza hawa wakimbizi kutoka Rwanda, Burundi na Congo ni kubwa sana, bahati mbaya wengi hamjafika katika kambi zao mkaona. misitu ambayo tungetumia kwa zaidi ya miaka 50 imetumika kwa muda wa miaka 5 tu. siraha walizoleta zinatumika kwenye ujambazi nchi nzima, ni bora tuwasaidie wapigane huko huko kwao ni siyo kukimbilia Tanzania. tufanye kama USA zero grazing.

Pili, jeshi letu litapata mbinu za kivita na mazoezi, tumekuwa tukijindanganya kuwa sisi ni bora east and central lakini tukajipime tuone uwezo wetu.

Tatu, wanajeshi wetu wana hamu ya vita kwani baadhi wanakaribia kustaafu bila kujua mlio wa risasi wa kifaru. matokeo yake wanaua raia kila wakati au kushirikiana na majambazi. wewe mtu unampeleka mafunzo mazito lakini hayatumii matokeo yake anaamua kupigana na aliye karibu nae. mfano juzi kawe askari wa jw waliua raia wao walijua ni simple kumbe adhabu ile hupewa mateka wa kivita. acha waende wakapate ozoefu pia nchi yetu itapat heshima kubwa.

Ni salamu kwa MSEVEN NA KAGAME wanaotaka himaya ya kitusti. wajue uwezo wetu. na hii hili litakuwa ni onyo kali kwao.

Tano: Congo ikiwa shwari tutafanya biashara na kukuza uchumi wa nchi yetu, kwaani wanatumia bandari yetu na baadhi ya bidhaa hununua Bongo usione kariakoo kuwa busy ukafiri ni wabongo tu, neda utawakuta akina mama wa kikongo wanafunga mizigo. ngano yao wanategemea AZAM, MFANO. kabla ya vita congo miaka ya Tz tulijenga tawi la BOT kigoma kwa kuwa kulikuwa na fedha nyingi za kigeni yaani US dola. lakini baada ya vita kongo majengo yale yamekuwa kumbi za miziki na ofisi za watu.


sita. Kabila mtoto wetu acheni tumsaide, najua kuna makubaliano hatuwezi kewnda tu kienyeji. kuna mlnago tutapata kitu kutoka kwa dogo kijana wetu kabila.

Tuwaombee vijana wetu warudi salama.
 
Wanajeshi wetu watapata uzoefu kidogo kupambana. This is part of field exercises, human costs not withstanding. Haiwezekani nchi inakaa tu bila battle action for decades, jeshi litadumaa kama lile la Malawi. Go, TPDF go!
Kuhusu tishio la Uganda na Rwanda, ambao wako upande wa waasi, sio suala tena. Rwanda iko UN security council na ilipiga kura jeshi lipelekwe, kwani kuwepo kwa jeshi hilo pia kunaisaidia kujikinga na waasi wa FDLR.
Pia Rwanda haiwezi kuthubutu kushambulia au kujenga uhasama wa kijeshi na Tanzania kwasababu kuu mbili: Uhusiano ndani ya EAC na pia bandari ya Dar es Salaam. Hatua hii ni mwanzo wa kumaliza matatizo DRC.

Bandari ya Dar es Salaaam kwa taarifa yako Rwanda inaitumia kwa 25% mizigo mingine yote inapitia Mombosa kwa taarifa yako ndugu yangu.Rwanda inaweza kuivamia Tanzania maana kila siri ya jeshi letu ipo Kigali simply because TPDF kuna wanyarwanda wa kutosha tu tena wana vyeo.So mimi naamini kabisa hata kama tuna jeshi gani Rwanda ikitujia tutahitaji kujipanga maana hawa jamaa wameshazoea vita, yaani tokea 1994 wao ni kupigana tu
 
Mungu ibariki Tanzania. Ibariki JWTZ. Uzalendo kwanza mengine baadae

Huo uzalendo wangefanya kwanza ndani ya nchi badala ya kupiga raia hovyo mtaani, wangejenga mahusiano mazuri na wananchi kwani wamekua na uonevu kiasi kwamba ukipata shida karibu na kambi ya jeshi hata kuomba msaada unaogopa,
Kuhusu kwenda congo ni shinikizo la UN, kwakua TZ ni mwanachama imetakiwa kupeleka majeshi congo sio uzalendo wa JWTZ
 
Naogopa kusema kuwa sasa tukiingiia DRC tumepanua wigo wa Mseveni na mwenzake Kagame kuingilia Tanzania na kuipiga
Achana na hao, unajua MALAWI pia wanapeleka askari kwenye hicho kikosi? Hatari ni kwamba wanaweza wakaanza kuzipiga wale wa jwtz na jwm huko huko kongo kama mechi ya majaribio.
 
Naogopa kusema kuwa sasa tukiingiia DRC tumepanua wigo wa Mseveni na mwenzake Kagame kuingilia Tanzania na kuipiga

Mbona mna wabudu sana Mseveni na kagame hivyo? wao wakoje ukilinganisha na watu wa nchi nyingine? au wao siyo wa kawaida? acheni ujinga bwana!
 
Bandari ya Dar es Salaaam kwa taarifa yako Rwanda inaitumia kwa 25% mizigo mingine yote inapitia Mombosa kwa taarifa yako ndugu yangu.Rwanda inaweza kuivamia Tanzania maana kila siri ya jeshi letu ipo Kigali simply because TPDF kuna wanyarwanda wa kutosha tu tena wana vyeo.So mimi naamini kabisa hata kama tuna jeshi gani Rwanda ikitujia tutahitaji kujipanga maana hawa jamaa wameshazoea vita, yaani tokea 1994 wao ni kupigana tu


Hawawezi kufanya kitu tunawajua sana kuliko mnavyopiga kelele kwenye keyboard!tena ukitakan kuona mwisho wao wajaribu waone itakua ndiyo mwisho wao na wewe utarudi kwenu rwanda!
 
'Fighting is a Serious Business' (John Garang - UDSM, 1997). Nafikiri tunayo matatizo mengi nchini. Tumepigana vita vya ukombozi kusini mwa Africa,Tumepigana Uganda _ TUMEFAIDI NINI? Hebu tuangaike na mambo yetu ya ndani... Watanzania tutajifunza lini kuachana na mambo yasiyo na tija?
 
Bandari ya Dar es Salaaam kwa taarifa yako Rwanda inaitumia kwa 25% mizigo mingine yote inapitia Mombosa kwa taarifa yako ndugu yangu.Rwanda inaweza kuivamia Tanzania maana kila siri ya jeshi letu ipo Kigali simply because TPDF kuna wanyarwanda wa kutosha tu tena wana vyeo.So mimi naamini kabisa hata kama tuna jeshi gani Rwanda ikitujia tutahitaji kujipanga maana hawa jamaa wameshazoea vita, yaani tokea 1994 wao ni kupigana tu
kawaambie hao wajomba zako wakiamua kuleta upuuzi wao huku kwetu tutawapaka samli na kuwachoma kama maiti za kihindi. Tunapenda amani lakini tuna roho mbaya sana!! ... stay away from us.
 
Kwa umoja wa africa ulipoomba tupeleke jeshi Anjoun Comoro tulitumia muda gani pale kulirudisha jimbo na ni idadi ya wanajeshi wangapi walipoteza maisha?

Tulitumia kama siku 5 tano tu kumaliza mchezo, hakuna shujaa wetu aliyekufa katika uwanja wa mapambano. Tulipoteza shujaa wetu mmoja wakati wanapakua mizigo pwani ya Tanzania baada ya kurudi.
 
Kwa mujibu wa Membe, Serikali inatarajia kuomba ridhaa ya Bunge kupeleka battalion 1 huko Kongo(Si chini ya wanajeshi 850) kulinda amani. Ikumbukwe kwamba wanajeshi hawa wamepewa mandate ya kupambana na waasi.
Je
1. Wanajeshi wetu wameandaliwaje kupambana na waasi huko Kongo? Any special training?

2.Kwa kuwa Idadi hiyo ni kubwa, je ipo mikakati ya kuhakikisha hatupungukiwi wakati hao wapo huko?

3. Any consideration and special attention to their families?Najua wamekula kiapo cha utii kuilinda mipaka ya Nchi yetu japo cjui kama kiapo hicho kinawalazimu kwenda mission hizi.

Maswali haya yanawezakuwa hayana mantic mana sina ufahamu wakutosha wakijeshi.

Otherwise nawatakia mafanikio mema hasa ukizingati wamekuwa na record nzuri huko Darfur, Syria na Lebanon

Aaah nilisikia kitambo tuu hao jamaa walikuwa ngerengere....toka mwezi wa kumi na mbili wako training tayari kwa kwenda kongo....unaposikia wanajeshi wanaenda kwenye mission za namna hiyo lazima wajifue sana
 
Back
Top Bottom