Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,810
- 11,981
Salaam Wakuu,
Wizara ya Elimu imesema Tanzania itajenga Chuo Kikuu cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Jijini Dodoma. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Dkt. Francis Michael Mkoani Dar es Salaam tarehe 19 Juni 2022 wakati wa kutiliana saini za Wasimamizi wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (Higher Education for Economic Transformation-HEET).
Amesema Mradi wa HEET unaofadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo imetoa kiasi cha Tsh Trilioni moja kwa malengo Mawili, kwanza ni kuwajengea uwezo Wahadhiri ili wajiendeleze kielimu. Wahadhiri wenye shahada moja wawe na mbi, wenye mbili wawe na tatu na wenye Shahada tatu wawe tatu wawe Maprofesa. Capacity building.
Lengo la Pili la Mradi wa HEET ni Kujenga miundombinu na vifaa wezeshi vya kufundishia na kufundisha ikiwemo ujenzi wa Campas mpya mikoa 17 nchini.
Chuo Kikuu cha Dar kinajenga Campas Lindi. Mikoa mingine itakayonufaika na fedha hizi ni Ruvuma, Songwe, Rukwa, Simiyu, Kigoma, Tabora, Shinyanga, Singida, Dodoma, Kagera, Mwanza, Tanga, Manyara, Mara na Katavi. Pia Chuo cha Marine Zanzibar kitapata Mgao wa fedha hizi. Mkoa wa Pwani tu ndo hakuna kitu, fedha bado zinatafutwa.
Naye, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga amezitaja Taasisi zitakazo nufaika na fedha za Benki ya Dunia ni Vyuo Vikuu 14, Taasisi za Wizara ya Elimu 3, Vyuo Vikuu vilivyo Wizara ya fedha 5 na Wizara yenyewe.
Kipanga amewataka Wasimamizi wa Mradi wa HEET kusimamia na kumaliza kazi kwa Wakati. "Kuna watu wanapewa hewa za Miradi zinakaa Miaka miwili bila kufanyiwa chochote. Safari hii usipotumia hizi hela kwa Wakati tunakunyang'anya tunampa mwingine". Amesema Kipanga.
Wasimamizi wa Mradi huu wameishukuru Banki ya Dunia na Serikali kwa kuwathamini, kuwajali na kuahidi kutekeleza mradi huu kwa Mafanikio.
====
MRADI WA HEET KULETA MAGEUZI MAKUBWA ELIMU YA JUU
▫️Benki ya Dunia yatoa takribani trilioni moja kuwezesha
▫️Wakuu wa Vyuo watakiwa kusimamia Mradi vizuri
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb) ameishukuru Benki ya Dunia kwa kutoa mkopo wa fedha takribani Shilingi trilioni moja ambazo zinakwenda kuleta mageuzi katika utoaji wa elimu juu.
Akizungumza Jijiji Dar es Salaam wakati wa utiaji saini makubaliano ya utekelezaji Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) na Vyuo Vikuu na Taasisi walionufaika amesema mkopo huo umelenga kuleta mageuzi ya kiuchumi kupitia utoaji wa elimu ya juu.
Amesema Mradi huo unakwenda kujenga miundombinu, kununua vifaa wezeshi vya kujifunzia na kusomesha wahadhiri ambapo Vyuo Vikuu vya umma 14, Taasisi Tatu zilizo chini ya Wizara zinazosimamia elimu ya juu na Taasisi Tano zilizo chini ya Wizara ya Fedha watanufaika.
Mradi wa HEET unakwenda kupeleka Vyuo Vikuu katika mikoa ambayo haina Vyuo hivyo kwa kujenga Kampasi zitakazokuwa zinalelewa na Vyuo Vikuu kamili ambavyo vinatekeleza Mradi huo. Kampasi hizo zitajengwa katika mikoa ya Mwanza, Kigoma, Lindi, Rukwa, Simiyu, Shinyanga, Tabora, Manyara, Ruvuma, Kagera, Songwe, Katavi, Mara, Singida, pia Mradi utajenga Chuo Kikuu cha Taifa cha TEHAMA, Dodoma.
“Kwenye kujenga hizi Kampasi tutakachofanya ni kuendeleza maono ya Rais wetu Samia Suluhu Hassan wakati anahutubia Bunge alisema kwamba mjaribu kutoa elimu bora ambayo inakidhi mahitaji kwa maana ya ujuzi na ufundi hivyo Kampasi zitakazojengwa tutaweka utaratibu kuwa hata kama watatoa Shahada ziwe ni za ujuzi,” amesema Waziri Mkenda.
Waziri Mkenda amewataka wakuu wa Vyuo kuhakikisha wanasimamia vizuri matumizi ya fedha hizo ili malengo ya Mradi yaweze kutimia. Amesema mradi huo ukitekelezwa vizuri utawezesha upatikanaji wa miradi mingine itakayofadhiliwa na Benki ya Dunia.
Awali Naibu Katibu Mkuu Prof. James Mdoe amesema Mradi huo unakwenda kuondoa changamoto kwenye vyuo vya elimu ya juu nchini ambapo amesema ni vizuri waratibu wa miradi waliopo kwenye Taasisi wakawa na mawasiliano ya karibu na Wizara pale wanapopata changamoto ya utekelezaji wa mradi huo ili ukamilike kwa wakati.
Wizara ya Elimu imesema Tanzania itajenga Chuo Kikuu cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Jijini Dodoma. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Dkt. Francis Michael Mkoani Dar es Salaam tarehe 19 Juni 2022 wakati wa kutiliana saini za Wasimamizi wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (Higher Education for Economic Transformation-HEET).
Amesema Mradi wa HEET unaofadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo imetoa kiasi cha Tsh Trilioni moja kwa malengo Mawili, kwanza ni kuwajengea uwezo Wahadhiri ili wajiendeleze kielimu. Wahadhiri wenye shahada moja wawe na mbi, wenye mbili wawe na tatu na wenye Shahada tatu wawe tatu wawe Maprofesa. Capacity building.
Lengo la Pili la Mradi wa HEET ni Kujenga miundombinu na vifaa wezeshi vya kufundishia na kufundisha ikiwemo ujenzi wa Campas mpya mikoa 17 nchini.
Chuo Kikuu cha Dar kinajenga Campas Lindi. Mikoa mingine itakayonufaika na fedha hizi ni Ruvuma, Songwe, Rukwa, Simiyu, Kigoma, Tabora, Shinyanga, Singida, Dodoma, Kagera, Mwanza, Tanga, Manyara, Mara na Katavi. Pia Chuo cha Marine Zanzibar kitapata Mgao wa fedha hizi. Mkoa wa Pwani tu ndo hakuna kitu, fedha bado zinatafutwa.
Naye, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga amezitaja Taasisi zitakazo nufaika na fedha za Benki ya Dunia ni Vyuo Vikuu 14, Taasisi za Wizara ya Elimu 3, Vyuo Vikuu vilivyo Wizara ya fedha 5 na Wizara yenyewe.
Kipanga amewataka Wasimamizi wa Mradi wa HEET kusimamia na kumaliza kazi kwa Wakati. "Kuna watu wanapewa hewa za Miradi zinakaa Miaka miwili bila kufanyiwa chochote. Safari hii usipotumia hizi hela kwa Wakati tunakunyang'anya tunampa mwingine". Amesema Kipanga.
Wasimamizi wa Mradi huu wameishukuru Banki ya Dunia na Serikali kwa kuwathamini, kuwajali na kuahidi kutekeleza mradi huu kwa Mafanikio.
====
MRADI WA HEET KULETA MAGEUZI MAKUBWA ELIMU YA JUU
▫️Benki ya Dunia yatoa takribani trilioni moja kuwezesha
▫️Wakuu wa Vyuo watakiwa kusimamia Mradi vizuri
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb) ameishukuru Benki ya Dunia kwa kutoa mkopo wa fedha takribani Shilingi trilioni moja ambazo zinakwenda kuleta mageuzi katika utoaji wa elimu juu.
Akizungumza Jijiji Dar es Salaam wakati wa utiaji saini makubaliano ya utekelezaji Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) na Vyuo Vikuu na Taasisi walionufaika amesema mkopo huo umelenga kuleta mageuzi ya kiuchumi kupitia utoaji wa elimu ya juu.
Amesema Mradi huo unakwenda kujenga miundombinu, kununua vifaa wezeshi vya kujifunzia na kusomesha wahadhiri ambapo Vyuo Vikuu vya umma 14, Taasisi Tatu zilizo chini ya Wizara zinazosimamia elimu ya juu na Taasisi Tano zilizo chini ya Wizara ya Fedha watanufaika.
Mradi wa HEET unakwenda kupeleka Vyuo Vikuu katika mikoa ambayo haina Vyuo hivyo kwa kujenga Kampasi zitakazokuwa zinalelewa na Vyuo Vikuu kamili ambavyo vinatekeleza Mradi huo. Kampasi hizo zitajengwa katika mikoa ya Mwanza, Kigoma, Lindi, Rukwa, Simiyu, Shinyanga, Tabora, Manyara, Ruvuma, Kagera, Songwe, Katavi, Mara, Singida, pia Mradi utajenga Chuo Kikuu cha Taifa cha TEHAMA, Dodoma.
“Kwenye kujenga hizi Kampasi tutakachofanya ni kuendeleza maono ya Rais wetu Samia Suluhu Hassan wakati anahutubia Bunge alisema kwamba mjaribu kutoa elimu bora ambayo inakidhi mahitaji kwa maana ya ujuzi na ufundi hivyo Kampasi zitakazojengwa tutaweka utaratibu kuwa hata kama watatoa Shahada ziwe ni za ujuzi,” amesema Waziri Mkenda.
Waziri Mkenda amewataka wakuu wa Vyuo kuhakikisha wanasimamia vizuri matumizi ya fedha hizo ili malengo ya Mradi yaweze kutimia. Amesema mradi huo ukitekelezwa vizuri utawezesha upatikanaji wa miradi mingine itakayofadhiliwa na Benki ya Dunia.
Awali Naibu Katibu Mkuu Prof. James Mdoe amesema Mradi huo unakwenda kuondoa changamoto kwenye vyuo vya elimu ya juu nchini ambapo amesema ni vizuri waratibu wa miradi waliopo kwenye Taasisi wakawa na mawasiliano ya karibu na Wizara pale wanapopata changamoto ya utekelezaji wa mradi huo ili ukamilike kwa wakati.