Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,062
- 136,431
Zile habari za Tanzania ni kisiwa cha amani, sasa kwisha!
Siku hizi kwenye news bulletins na headlines za kimataifa, tunatajwa kuhusiana na utekaji, uuaji, uminywaji wa demokrasia, na upumbavu unaofanana na hayo.
Habari za Agatha na Boniface kuteswa kingono zimeshavuka mipaka ya Tanzania.
Sifa ya nchi ishachafuka na watawala wamekuwa mabubu!
Leo tumezungumziwa hivi na Firstpost:
==============
Wanaharakati wawili kutoka Kenya na Uganda wameibuka hadharani wakitoa madai ya kusikitisha kuhusu ukatili wa kingono waliodai kufanyiwa walipokuwa kizuizini jijini Dar es Salaam, Tanzania. Wanasema walikamatwa baada ya kuonyesha uungwaji mkono kwa kiongozi wa upinzani, Tundu Lissu, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhaini.
Kwa mujibu wa wanaharakati hao, walitekwa kutoka katika vyumba vyao vya hoteli, wakawekwa chini ya ulinzi mkali, na kuhojiwa kwa muda mrefu huku wakikumbana na vipigo na unyanyasaji wa kijinsia kutoka kwa maafisa wa usalama wa Tanzania. Maelezo yao yanatisha na yanaonyesha hali ya kuvunjwa kwa haki za binadamu na ukandamizaji wa kisiasa unaozidi kushika kasi kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
Siku hizi kwenye news bulletins na headlines za kimataifa, tunatajwa kuhusiana na utekaji, uuaji, uminywaji wa demokrasia, na upumbavu unaofanana na hayo.
Habari za Agatha na Boniface kuteswa kingono zimeshavuka mipaka ya Tanzania.
Sifa ya nchi ishachafuka na watawala wamekuwa mabubu!
Leo tumezungumziwa hivi na Firstpost:
==============
Wanaharakati wawili kutoka Kenya na Uganda wameibuka hadharani wakitoa madai ya kusikitisha kuhusu ukatili wa kingono waliodai kufanyiwa walipokuwa kizuizini jijini Dar es Salaam, Tanzania. Wanasema walikamatwa baada ya kuonyesha uungwaji mkono kwa kiongozi wa upinzani, Tundu Lissu, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhaini.
Kwa mujibu wa wanaharakati hao, walitekwa kutoka katika vyumba vyao vya hoteli, wakawekwa chini ya ulinzi mkali, na kuhojiwa kwa muda mrefu huku wakikumbana na vipigo na unyanyasaji wa kijinsia kutoka kwa maafisa wa usalama wa Tanzania. Maelezo yao yanatisha na yanaonyesha hali ya kuvunjwa kwa haki za binadamu na ukandamizaji wa kisiasa unaozidi kushika kasi kuelekea uchaguzi mkuu ujao.