Tanzania imenyimwa msaada wa fedha za MCC?

Tanzania imenyimwa msaada wa fedha za MCC?

Baadhi ya nchi nyingine zilifanikiwa kwa sababu ya nidhamu ya matumizi pamoja na kisimamia sheria za nchi kuhakikisha zinafuatwa na kila raia.Kwa hapa kwetu Tanzania tume wekeza sana kwenye matumizi kuliko kuwekeza ktk maendeleo.Tumewekeza kwenye kulindana hasa inapotokea wizi(Ufisadi)unao husisha chama chetu tukufu CCM....Tuna watetea wezi wa mali ya umma kwa kuwapa vyeo..Hatubwashitaki /hatuwafungi/hatuwafilisi mali walizo tuibia ,hivyo hata ungelipa kodi mpaka ufilisike nchi haiwezi kusonga kwa makando kando kama hayo niliyo yaainisha hapo juu.

Maendeleo huja kwa kasi lakini hakuna maendeleo kama hakuna demokrasia inayo dhihirika kwa vitendo,sahau sana tutakuwa tuna tembea mwendo wa mlevi hatua mbili mbele halafu hatua nne nyuma...

..
Point mkuu
 
Nadhani watu wengi hawaelewi kuwa hakuna anayekataa huo msaada, isipokuwa sisi kama wa-Tanzania hatuwezi kuendelea kupokea misaada inayotubana na kuingilia uhuru wa nchi yetu! Wapo wa-Tanzania wanaosema hatuwezi kushindana na wazungu, ni kweli hatuwezi kushindana nao tunawahitaji sana, lakini na wao pia wanatuhitaji sana kuliko sisi tunavyowahitaji kwa hiyo acha watunyime watakuja wenyewe!
vasco dagama alivyotuacha sisi ndio tunawaitaji zaidi ya wao wanavyotuitaji
 
Tatizo hapa sio misaada kama misaada lakini ni image ya nchi katika uso wa dunia, kwa taarifa hio kutoka kwa MCC kuwa tumekosa misaada, jee kuna uhalali wa kuitangazia dunia kuwa Tanzania ni nchi ya demokrasia? kuna haja kwa viongozi wastaafu wakina Mkapa na Kikwete kwenda nje kusuluhisha wakati wewe mwenyewe huna demokrasia? ukiacha ushabiki nikweli Tanzania tunajitosheleza kwa kila kitu kiasi kwamba hatuhitaji misaada? Jee baada ya MCC nani mwengine atafuata katika kuiwekea vikwazo Tanzania? vikwazo hivyo vikiwa implemented nini athari kwa Tanzania? tusiwe simple mind tujadili hili kwa upane wake.
 
Naombeni kuuliza swali ,Hivi Marekani inayotoa misaada kwa nchi nyingi duniani hivi yenyewe haidaiwi ???
Unadhani Marekani wao bado wanapambana kupata maji safi, lishe duni na kujenga barabara za kiwango cha rami nchi nzima? Unajidanganya nafsi yako.
 
Unadhani Marekani wao bado wanapambana kupata maji safi, lishe duni na kujenga barabara za kiwango cha rami nchi nzima? Unajidanganya nafsi yako.
Nimejidanganya vipi hilo swali langu umelielewa au umeamua tu kukurupuka ?
 
Saa nyingine ni bora tunyimwe.
Hii misaada ndiyo inayo turudisha nyuma.
Tumepumbazwa na misaada.
Ninakubaliana na mtazamo wako!

Matatizo humlazimisha binadamu kufikiria kwa upana zaidi ili kukabiliana nayo kwa ufanisi zaidi.
 
Kumbuka misaada haijengi bar hubomoa kwa kutulemaza tena ikome kabisa tujitegemee sasa.
 
Hoja yangu ni utegemezi, tusiishi kwa kutegemea na hasa inapoonekana tunauwezo

Kwa hali tuliyo nayo hatuwezi kujitegemea ,tuna deni la trilion zaidi ya 40 wakiamua tu kutudai tunao uwezo wa kulipa na tukasalia salama?
 
mwenye kaya nae anatuongopea kwa nyenzo zipi tutajitegemea? kama mali asili za taifa kagoma kupitia mikataba yake(madini,gesi na nk) yeye anapambana na watumishi hewa hivi kwa taifa kama hili ambalo lina changamoto kibao kwa mapato yapi tujitegemee?
Nigeria pamoja na uchumi mkubwa bado ni tegemezi iweje sisi ambao kutwa kuchwa ni ufisadi tu.
Pitia mikataba yote ya madini na gesi na fuatilia fedha zote zilizopotea kizembe BOT na hapo tunaweza angalau kupunguza utegemezi sio hizi ngonjera za majipu tu
Unaongeaa kama bavicha tu sidhani kama kunajambo unajua zaidi ya kupayuka tu.
 
Kwa hali tuliyo nayo hatuwezi kujitegemea ,tuna deni la trilion zaidi ya 40 wakiamua tu kutudai tunao uwezo wa kulipa na tukasalia salama?
Kila deni linamkataba wake na sharti lake na kila deni litalipwa kwa mujibu wa mkataba husika so usihofu mkuu nchi inakwenda kujitegemea kabisa hii.
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Sahau enzi ya mzee wa kutabasamu, hapa kazi tu na tulipe kodi!
Wazungu hawana lolote! Tukiziba mianya ya ufisadi hawana jeuri ya kutoisoma namba!
Nina imani na Magufuli! Mpaka sasa amewashikisha adabu, hajawakimbilia kuomba omba kama mtamgulizi wake alivyofanya Mara tu alipochaguliwa!

Unatoa majibu mepesi kweli kwenye hoja inayohitaji majibu. sahihi na njia zinazoonekana ....
 
maskini jeuri, hata ukiwa tajiri hela zile si za kuzipuuzia, zingefanya mengi, Mahiga tusaidie! Style ya kumuita Magu kule..
Nadhani hakuna anayesema unaweza kupuuzia, hoja ya msingi ni at what cost?

Ni nchi ngapi zimefanikiwa baada ya kuishi kwa kutegemea misaada ya Marekani na EU?
 
Nadhani hakuna anayesema unaweza kupuuzia, hoja ya msingi ni at what cost?

Ni nchi ngapi zimefanikiwa baada ya kuishi kwa kutegemea misaada ya Marekani na EU?
hivi ujeuri huu wa kuhoji mashart ya mikopo ya nchi umeanza mwezi gani. Kama kuna mtu anaejua masharti ya fedha za mcc atuwekee hapa. Naona watu wanaishi kwenye kivuli cha matumaini makuu. Hatujaifikia stage hiyo.
 
Kila deni linamkataba wake na sharti lake na kila deni litalipwa kwa mujibu wa mkataba husika so usihofu mkuu nchi inakwenda kujitegemea kabisa hii.

Katiba ile ile /kwa chama kilekile kilichoshindwa miaka karibu 50 sasa/kwa mfumo ule ule uliofeli/kwa watu wale wale /kwa fikra zile zile/ zilizokuwa zikipokea misaada na bado tumeshindwa kupiga hatua zenye kufanana na raslimali zetu,leo tuje tutarajie miujiza ya nchi kujitegemea bila misaada!!!!?.

Mkuu bado hauja niaminisha kirahisi namna hiyo..
 
Kwa hali tuliyo nayo hatuwezi kujitegemea ,tuna deni la trilion zaidi ya 40 wakiamua tu kutudai tunao uwezo wa kulipa na tukasalia salama?
Hali gani tuliyonayo? Mbona una mawazo ya kushindwa shindwa tu? Mbona unaamini kuwa MCC ndio mwarobaini ili hali huamini kauli ya rais wako kuwa hii nchi soon inajitegemea? Kuwa deni si kosa, kaza buti
 
Unatoa majibu mepesi kweli kwenye hoja inayohitaji majibu. sahihi na njia zinazoonekana ....
Nimepitia comments zako, sijaona sehemu uliyoleta majibu zaidi ya hoja za utegemezi na kuamini MCC ndio baba yako
 
Back
Top Bottom