Tanzania imenyimwa msaada wa fedha za MCC?

Tanzania imenyimwa msaada wa fedha za MCC?

Tusidanganyane. Ni mjinga pekee yake anayeweza kukaa chini na kusema, 'hiyo pesa tunyimwe kwa kuwa tuna uwezo wa kujitegemea'. Hiyo pesa kwa Tanzania ni muhimu sana. Ni hela hiyo ya MCC ndiyo iliyojenga barabara nyingi mpya za lami na madaraja wakati wa JK, pamoja na miradi mikubwa ya umeme intondelea. Leo karibia miradi yote ya ujenzi imesimama.

Dola karibia milioni 500 ni hela nyingi sana kwa nchi kama Tanzania ambayo pesa hiyo ni sawa na makusanyo yote ya kodi kwa mwezi. Ebu jiulize, hivi unaweza kukubali kiurahisi kuwa ukose mshahara wako wote wa mwezi unaoitegemeza familia yako?

Magu asijidanganye, tunatakiwa kujitegemea lakini siyo kwa namna anayoifikiria. Kwa sasa ni wakati wa kukusanya nguvu zote, iwe ni misaada, mikopo, makusanyo ya kodi kwaajili ya kupata nguvu za kuweza kujitegemea mbeleni. Tanzania kwa makusanyo yake ya pesa ya madafu trilioni 1, haina uwezo wa kujitegemea ghafla kutoka kwenye dependence ya 40%.

Magu asitupeleke iliko Zimbabwe ambako kiburi cha Mugabe kinawatesa Wazimbabwe balaa. Madaktari, manesi na walimu Wazimbabwe wameishia kuwa waiters SA. Ni aheri kuwa waiter SA kuliko kuwa daktari Zimbabwe.

Mwalimu naye aliwahi kujitahidi kutaka kufanya haya ya Magufuli, waliokuwepo wanajua. Hata sabauni za kufulia, mafuta ya kupikia na chumvi viliadimika.

Kumbukeni kuwa hiyo 470 milioni ni pesa ya kigeni, na ina impact kubwa kwa Tanzania. Kwa nini Watanzania wachelewe kupata maendeleo au wateseke kwa mambo ambayo ni rahisi kutekeleza? Afadhali tungenyimwa huo msaada kwa kutetea mambo ya msingi, mambo yenye faida kwa Taifa. Hapo tungesema tunalinda uhuru wa Taifa. Lakini sasa tutanyimwa kwa mambo ya kipumbavu, kutetea udikteta uliofanyika Zanzibar!

Hii ni sawa na mtu ambaye ni mchafu, hana choo, hafui nguo zake, anapikia chakula kwenye mazingira machafu. Halafu anatokea jirani anakuambia kuwa nitakujengea nyumba ambayo itakuwa na choo kizuri ndani, itakuwa haina vumbi kwa sababu nitakuwekea tiles LAKINI ili nikufanyie hayo kwanza nataka unioneshe unauchukia uchafu, uache kujisaidia kwenye upenu wa nyumba yako. Halafu wewe unasimama na kusema unaingilia uhuru wangu, kama ni hivyo ni aheri usinipe huo msaada. Naenda kufyeka msitu, nikapande michungwa baada ya miaka 5 nitaweza kujenga mwenyewe kwa sababu nina uwezo.

Kwanza masharti ya MCC siyo kwa faida ya USA, ni kwaajili yetu wenyewe. Yaani udikteta uliofanyika Zanzibar kwa manufaa ya Shein na CCM, udikteta ambao umemwudhi kila mtu mstaarabu Duniani, ndiyo sisi utufanye kuonekana ni wetu wenye msimamo? Kama huo ndiyo msimamo basi ni msimamo wa mtu mjinga.

Juzi Magufuli wakati anazindua mradi wa umeme mradi wa Kinyerezi alisema wazi kuwa hatuwezi kuacha hela ya bure tuliyopewa na Japani kwa sharti la kuchangia 15% ya gharama ya mradi. Pesa itakayotolewa na Japani kwa mradi wa Kinyerezi ni ndogo kuliko hiyo ya MCC. Ya Japan ni mkopo nafuu, ya MCC ni ya msaada, 100% free money, gharama yake ni kudhibhirisha tu kuwa tunaheshimu maamuzi ya wananchi wetu kwa vitendo.
Kiuhalisia wazungu huchukua utajiri Mkubwa zaidi kutoka kwetu kwa njia ya mikataba mibovu ya kifisadi, ukwepaji kodi na misamaha ya kodi kuliko kiasi wanachotupa kama misaada!
Si uliona awamu iliyopita ilivyopitisha mikataba mibovu ya kifisadi kwa hati ya dharula! Wazungu ndo wanapenda watawala wa hivyo! Magufuli tukimpa sapoti kwa kufanya kazi kwa bidii, na tukakubali kulipa kodi kwa furaha, na mikataba tukaipitia upya, wazungu wataisoma namba!
 
Naomba kujua hivi huu ni MSAADA ambao ni kama sadaka au MSAADA MKOPO ambao tutapaswa kurudisha?
 
Huwa nasikitika sana kusikia kauli wanazotoa viongozi wetu kama alivyofanya JPM. Wakati mwingine ni bora kuwa kimya huku ukirekebisha tatizo kimkakati. Siku zote nchi yetu hutegemea misaada na mikopo nafuu kwa shughuli za maendeleo. Kuondokana na hali hiyo si suala la kuamka siku moja na kusema "hatuna haja ya misaada tena!" Hiyo ni "political rhetoric". Haina maana yoyote.

Kikubwa zaidi, unakujaje na kauli ya "jeuri ya kujitegemea" mara baada ya "kunyimwa"? That's not serious. Anza kwanza kujiuliza ni sera au tunu ipi ya kitaifa unayoitetea/unayoisimamia kiasi cha kuwa radhi kukosa fursa ya pesa/mtaji? Is it worth it? Na una jeuri ya kusimama imara hadi mwisho?

Halafu tusije kusahau kuwa hapa duniani hata nchi zilizoendelea kutuzidi sana huko Ulaya, Asia na Amerika huhitaji misaada (bail out) mara kwa mara ili kujiweka sawa. Na wanajadili kwa undani masharti yote huku wakisimamia tunu zao za kitaifa kikamilifu. Hivi karibuni tumeona Ugiriki ikihangaika kujadili na EU masharti ya bailout kwa msimamo thabiti bila kauli za "kimipasho".


Hii jeuri ya kunyimwa pesa ndipo unadai "sizihitaji!" ni kutaka kuweka shule pembeni na kuingiza mipasho kwenye masuala muhimu ya kiuchumi kitaifa. Leta jeuri hiyo wakati unakopesheka; unasaidika na unaweza kuzisomesha taasisi za fedha masharti yako.
 
End on neo colonialisms
End of economic dependency

Nampongeza rais kwa kauli yake

Hakuna nchi iliyoendelea dunian kwa kutegemea mikopo ya kinyonyaji
"hakuna nchi iliyoendelea duniani kwa kutegemea mikopo ya kinyonyaji" Hii kauli ni kweli. Lakini usipongeze kauli pongeza vitendo.

Hakuna nchi ya dunia ya tatu iliyoweza kukimbia makucha ya Neo colonialism na economic dependancy. Ukisema ipo unajidaganya mwenyewe, tena unasema kwa uhakika kabisa eti unapongeza kauli. Je kauli inaweza kututoa kwenye ukoloni mamboleo na uchumi tegemezi?

Kutoka kwenye ukoloni mamboleo na uchumi tegemezi kunahitaji maono na dira mpya itakayobadilisha sera zote za nchi na kuleta commitment ya hali ya juu kwa viogozi na wananchi kwa ujumla.

Kwanini nchi za dunia ya tatu haziwezi kujinasua na makucha ya ukoloni mamboleo na uchumi tegemezi? kujibu swali hili ina kupasa kuangalia matatizo yote yanayokabili hizo nchi pia kuangalia je matatizo hayo wanayatambua ? na kama wanayatambua wamefanya juhudi gani kuyatatua wenyewe pasipo mkono wa mkoloni mamboleo? Je ni kwa kiasi gani wananchi wapo aware na matatizo hayo? au wapo kiushabiki wa kisiasa tuu?
Tatizo la dunia ya Tatu ni kuigiza kuwa hakuna matatatizo na kama yapo ni madogo sana na yanaweza kutatuliwa kwa haraka zaidi kipindi wanapoomba kura kwa wananchi . Masikini sijui ni lini nchi dunia ya Tatu zitakapo kubali kuwa zina matatizo na kuazimia kuyatatua wenyewe badala ya kuhaidiwa ahadi tamu zisizo tekelezeka yani wananchi wamekuwa wakitegemea sugarcoated politics kutatua matatizo yao. Shida tuliyonayo wakazi wa dunia ya Tatu ni kuigiza kuwa hatuna matatizo kwa kuwa tunaishi kwa ushabiki wa kisiasa badala ya kuangalia maslahi ya mataifa yetu.

Baadhi ya Matatizo yanayo fanya nchi za dunia ya Tatu kuendelea kuwa watumwa wa wakoloni mamboleo kupitia uchumi tegemezi ni :-
1. Ukosefu wa uzalendo kwa viongozi wa dunia ya tatu. Bado dunia ya Tatu haijapata viongozi wazalendo hata hao wakina Mugabe sio wazalendo kwa Africa na nchi zao binafsi kwa kuwa wapo kimaslahi binafsi na ndiyo maana wanang'ang'ania. madaraka ili kutimiza maslahi yao binafsi.

2. Matumizi mabaya ya madaraka kwa nchi za dunia ya Tatu hususani kusini mwa jangwa la Sahara imekuwa ni chronic disease kwakuwa hakuna utaratibu rasmi ndiyo maana hakuna uwazi katika maslahi ya taifa ni urasimu tuu . Hivyo upelekea mikataba mibovu, Rushwa, ufisadi na wizi wa Mali ya umma. Na kwa kuwa kuna double standards hakuna hatua inayo chukuliwa kwa watu hao . Bado matumizi mabaya ya rasilimali yani dunia ya Tatu rasilimali zimekuwa laana badala ya NEEMA

3. Mifumo mibovu ya elimu inayoandaa watu kuajiriwa kwa kuwa wamefundishwa kufanya kazi badala ya kuwa wataalamu wenye kutumia taaluma zao kivitendo katika kutatua matatizo. Hivyo tumejikuta tuna lundo la wasomi wasiozalisha maana hawana kazi. Wakati nchi za dunia ya kwanza wamewekeza katika elimu ya vitendo ndio maana kila kukicha wanafanya uvumbuzi mkubwa wa kiteknolojia na wanaanzisha viwanda vinavyowezesha serikali zao kuneemeka kwa kulipa kodi.


4. Nchi za dunia ya tatu hazina viwanda hata kidogo yani zaidi ya 90% ya bidhaa zote zinatoka dunia ya kwanza. Sasa tutawezaje kuondokana na makucha ya mkoloni mamboleo bila uwezo wa kuzalisha bidhaa zetu wenyewe na kuuza nje? Hata wachumi wanasema ili nchi iondokane na utegemezi ni lazima iweze kuexport zaidi kuliko kuimport (favorable balance of payment/ trade) . Dunia ya Tatu hakuna teknolojia, nishati ya uhakika, wataalamu wenye ujuzi wakivitendo ndiyo maana tunakuwa tegemezi wa kila kitu.

5. Migigoro ya kisiasa, kikabila inayochochewa na watu wa dunia ya kwanza kwa kutengeneza vibaraka wa kisiasa ili kutimiza mahitaji yao na kwa kuwa watu wa dunia ya Tatu sio wazalendo wanakubali kutumika.

6. Dunia ya Tatu imetengwa kwenye geopolitics, diplomasia ya kimataifa katika vyombo muhimu vya kufanya maamuzi yenye maslahi kwao na hakuna juhudi yoyote iliofanywa kuihusisha dunia ya Tatu, watu wa dunia ya kwanza wanasema vingozi wa dunia ya Tatu hawafuati kanuni za utawala bora na wanakiuka haki za binadamu na ndio maana The Hague imekuwa shubiri kwao.
Dunia ya Tatu haina veto power kwenye maamuzi makubwa kabisa ya dunia wala ushawishi kama wale wa P5+, G7,G8, G20 nk... pia haina nguvu kwenye mifumo ya fedha ya IMF na WB, pia katika WTO na WCC hadi kwenye michezo. Sasa kuondoka kwenye mifumo hii yenye kuifanya dunia ya Tatu kuwa hivi ilivyo inahitaji mtazamo mpya na utawala bora na commitment za ukweli zisizo na maslahi binafsi ya kisiasa.
 
Utoe pesa uwape akina
Nkurunzinza hawa wa bongo?
Hata mim nisingetoa bnaa wana
zitumbua pesa zingine ndo wanunulia magari ya maji ya
kuwasha ili wananchi tukiwadai
Pesa zetu watumwagie mimaji
ya kuwashaa
 
Kiuhalisia wazungu huchukua utajiri Mkubwa zaidi kutoka kwetu kwa njia ya mikataba mibovu ya kifisadi, ukwepaji kodi na misamaha ya kodi kuliko kiasi wanachotupa kama misaada!
Si uliona awamu iliyopita ilivyopitisha mikataba mibovu ya kifisadi kwa hati ya dharula! Wazungu ndo wanapenda watawala wa hivyo! Magufuli tukimpa sapoti kwa kufanya kazi kwa bidii, na tukakubali kulipa kodi kwa furaha, na mikataba tukaipitia upya, wazungu wataisoma namba!

"Wazungu" hawakupi masharti ya kusaini mikataba mibovu, kujiibia kwa manunuzi ya kihuni (rada, ndege ya rais, malori ya jeshi, n.k.) na kuchota toka BOT (EPA) ... Ni juu yako kujadili masharti yao kwa ujuzi na jeuri yako kama unayo. Hatuwezi kulaumu watu wa nje kwa ufisadi wanaofanya viongozi wetu kwa kupitia makampuni ya kigeni. Halafu sahau uwezekano wa kuwasomesha namba "wazungu". That's a tall order for the type of leadership we have and cherish!
 
"Wazungu" hawakupi masharti ya kusaini mikataba mibovu, kujiibia kwa manunuzi ya kihuni (rada, ndege ya rais, malori ya jeshi, n.k.) na kuchota toka BOT (EPA) ... Ni juu yako kujadili masharti yao kwa ujuzi na jeuri yako kama unayo. Hatuwezi kulaumu watu wa nje kwa ufisadi wanaofanya viongozi wetu kwa kupitia makampuni ya kigeni. Halafu sahau uwezekano wa kuwasomesha namba "wazungu". That's a tall order for the type of leadership we have and cherish!
Sahau enzi ya mzee wa kutabasamu, hapa kazi tu na tulipe kodi!
Wazungu hawana lolote! Tukiziba mianya ya ufisadi hawana jeuri ya kutoisoma namba!
Nina imani na Magufuli! Mpaka sasa amewashikisha adabu, hajawakimbilia kuomba omba kama mtamgulizi wake alivyofanya Mara tu alipochaguliwa!
 
mtegemea cha nduguye hufa masikini...ni bora tutafute vyetu kama wao wmegoma tuachane nao tufocus kwenye vyanzo vingine japo itatuwia vigumu but govt ikikaza kukusanya kodi with good faith tutafika tu
 
The only reason we have been begging all these years is because of poor leadership & hypocrite elites. Now that we have Magufuli It's time to say NO to conditioned grants.
 
Trillion moja? Si nimesikia tra wanakusanya hiyo trillion kwa mwezi mmoja tu? Kumbe tunaweza kujitegemea.
 
Misaada yenyewe midogo, sasa hiyo $472 million itasaidia nini! Kila mwaka wanatoa imesaidia nini hadi leo??

1. Mkuu Trilion moja ni pesa kidogo?? Hivi unafahamu kuna wanafunzi wangapi wanakaa chini? Kuna wagonjwa wangapi wanalala chini?? Kuna wanachuo wangapi wamekosa mikopo ?

2. ...''Kila mwaka wanatoa imesaidia nini hadi leo'?.... Itasaidiaje wakati mnalipa wafanyakazi hewa? Inasaidiaje wakati badala ya kuitumia kuimarisha miundombinu mnagawana na wakandarasi na matokeo yake barabara haijaisha ni mashimo tupu? itasaidiaje wakati 1 km ya barabara mnajenga kwa 3-4 bill badala ya 1bill? Itasaidiaje wakati mita za mafuta kule bandarini mmezifunga ili mkwepe kodi halali? Zitasaidiaje wakati mabwawa kule mtera yakijaa maji mnayafungua ili muuze mafuta??...the list goes on...Huyu baniani mnamuona mbaya sanaaa lakini kiatu chake dawa!!
 
Tukubali ukweli ingawa ukweli unauma Siku zote lakini ni dawa ya kupata ufumbuzi wa matatizo
Kwanza wazungu wana elimu kutuliko
Pili wazungu wana umoja na wanashirikiana katika maamuzi yao wanaunganisha nguvu zao za kiuchumi kwa malengo ya kuhakikisha waafrika katu hawajitegemei kwa chochote.
Ili hawo wazungu wawe na fursa nzuri ya kuendelea kututawala kiuchumi na kutunyonya

Sera za kibeberu za kimagharibi ndio zinazotawala dunia kwa sasa ndio watengeneza Sera za kichumi duniani ndio wenye maamuzi ya. kupanga bei ya mafuta duniani bei ya kahawa ,katani tumbaku pamba nk
 
...utawala uliopita umeilemaza sana TZ....yani mkuu wa nchi alifikia mahali anasema eti asiposafiri hatutoweza kula kweli??...na wabongo wakawa wanakaa wanamsikiliza bila aibu....eti anafika mahali anahutubia taifa kwa kuelezea safari zake za kwenda kuomba nje na watu wanakaa wanamsikiliza!....yani nchi aligeuzwa ombaomba wa dunia kwa miaka 10....sasa kwa kweli ni vema JPM ameliona hili...maana hata zile safari za mkwere zimedhihirika zilikuwa hasara tu kwa taifa....na ndio maana JPM mwenyewe ka mute kusafiri....Ukitaka kujua majanga ya gharama za safari za mkwere...rejea uzi wa safari zake humu....
 
Sahau enzi ya mzee wa kutabasamu, hapa kazi tu na tulipe kodi!
Wazungu hawana lolote! Tukiziba mianya ya ufisadi hawana jeuri ya kutoisoma namba!
Nina imani na Magufuli! Mpaka sasa amewashikisha adabu, hajawakimbilia kuomba omba kama mtamgulizi wake alivyofanya Mara tu alipochaguliwa!

Magufuli anao ubavu wa kung'oa mizizi mikubwa ya ufisadi iliyowekwa na JK na BWM? Leo angalau nilipata faraja kusikia Wabunge wamekamia kuung'oa mmoja wa IPTL. Nasubiri kuona Magufuli akitinga maeneo hayo yanayofilisi taifa kwa namna ya kutisha. Sio hii mipasho ya kusingizia "wazungu" uovu wa viongozi wetu wenyewe.
 
Trillion moja? Si nimesikia tra wanakusanya hiyo trillion kwa mwezi mmoja tu? Kumbe tunaweza kujitegemea.
Kwahiyo tunaweza kujitegemea kwa tirioni 12? wakati bajeti yetu ya FY2015/16 ilikuwa tirioni 22.5. Je tutaweza kujitegemea kwa deficit budget? iliyo na upunguvu wa tirioni 10.5?
 
Tuwe na aibu kidogo, kujilizaliza eti tunanyimwa misaada ni udhaifu mkubwa sana.
 
Daaah! Tukikosa huo mpunga itakuwa ni pigo kubwa sana...
Hakuna pigo lolote. Tzs 1bn ni mapato ya kodi kwa wezi moja tu. Kila mtu akilipa kodi halali na serikali ikibana matumizi hatuhitaji msaada huo. Tuanze kujitegemea ndipo wazungu watatuheshimu.
 
Nadhani watu wengi hawaelewi kuwa hakuna anayekataa huo msaada, isipokuwa sisi kama wa-Tanzania hatuwezi kuendelea kupokea misaada inayotubana na kuingilia uhuru wa nchi yetu! Wapo wa-Tanzania wanaosema hatuwezi kushindana na wazungu, ni kweli hatuwezi kushindana nao tunawahitaji sana, lakini na wao pia wanatuhitaji sana kuliko sisi tunavyowahitaji kwa hiyo acha watunyime watakuja wenyewe!
 
Back
Top Bottom