Tanzania imegeuka kuwa Taifa linaloshauriwa na watumiaji wa Mitandao?

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,086
6,568
Ni kweli tupo kwenye ulimwengu wa kidigital, hivyo huwezi kuwakwepa watumiaji wa mitandao. Maana mitandao kama JF huku watu wanatiririka ukweli tofauti na kwenye magazeti.

Lakini hii sio sababu ya kusema kuwa serikali iwe na watumishi amabo inawalipa mishahara alafu hawajui masuala ya kitaalamu na kiutawala. Matokeo yake eti likitokea kosa wananchi wanaotumia mitandao ya kijamii ndio wapost juu ya hilo kosa na kisha serikali kujirekebisha.

Mfano alipofariki hayati rais JPM, rais wa sasa alitangaza maobolezo kinyume na sheria ya mazishi ya viongozi, na alisema maombolezo ni siku kumi na nne. Ni aibu ofisi nyeti ya ikulu ambayo inawatalaamu wa kila namna wakiwemo wanasheria kumuingiza chaka aliyekuwa mtoa taarifa. Lakini kosa hili lilibainishwa na watumiaji wa mitandao ya kijamii hasa JF na baadae wakajirekebusha.

Hii ya kuteua kada wa Ccm awe mkurugenzi wa TPDC ni doa baya sana kwa ofisi ya rais hasa ukizingatia sifa za huyo kada ukilinganisha na unyeti wa shirika alilokuwa anapaswa kuliongoza. Nalo ni watumiaji wa mitandao ndio waliliibua na baada ya masaa 12 ndio akatenguliwa.

Hii inatupa picha mbaya sana juu ya watu ambao wanalipwa mishahara mikubwa kwa kutumia kodi za wananchi huku wakionyesha wazi kuwa hawana uwezo wa kutimiza wajibu wao.

Je, kama kungekuwa hakuna mitandoa ya kijamii ingekuwaje?
 
Genge linalomzunguka mh. Rais lilipaswa ondolewa lote, kwenye huu uteuzi hakuna msawazo wa kijinsia, yaani watu wa vetting walishindwa Cheki na utumishi wa umma na taasisi zake na kupata wamama wenye sifa?
 
Ni muda mfupi sana kwa mtu makini kuanza kuteua au kutengua hasa kwenye hizu nafasi za utendaji
 
Isingekuwepo mitandao hatujui ingekuwaje! Lakini sasa kwakuwa ipo, ndio maana ya kuwepo. Kumbuka wahusika wanaweza mshauri mkuu kwa makosa ya makusudi au ya kutokujua.

Sasa ni rahisi kujua mapokeo ya maamuzi mapema, na kama kuna haja ya kurekebisha yanafanyika haraka, hapo kuna taabu gani. Kumbuka sasa hivi bunge letu ni CCM tupu. Na washauri ni CCM vilevile. Sasa chombo pekee cha kutoa maoni bila unafiki ni mitandao ya kijamii.

Ni naona mitandao ya kijamii inachukua nafasi ya bunge katika kuisimamia na kuishauri serikali. Na kiongozi anayefuatilia na kukubali kufanyia kazi baadhi ya comments nampongeza sana.
 
Tatizo ni kutoheshimu mifumo iliyowekwa katika teuzi. Ukienda TPDC kwenye Muundo wake lazima utakuta sifa za mtu kuwa DG wa TPDC.

Ingezingatiwa hiyo huyo dogo asingepenya hata kidogo. Teuzi za sasa haziangalii hayo, ni utashi tu wa mteuzi na wanaomshauri. Hapo ndipo shida ilipoanzia. Wanaomsaidia Rais wamempotosha na wanastahili adhabu.
 
Kwa rais Samia Sio muda mfupi mkuu, alikuwa serikalini muda wote anajua uimara na udhaifu wa viongozi waandamizi serikalini
Kama uimara au udhaifu wa Serikali na yeye amechangia kwa 100% kwani yeye alikuwa Makamu wa Rais mtu wa pili kwa mamlaka Tanzania mshauri number moja wa Rais pili angalia mambo yanavyochanganya toka alivyotoa siku 14 za maombelezo, kutengua uteuzi wwake mwenyewe chini ya masaa 24 kurudisha mawaziri wote wa mtangulizi wake mama anahitaji kutulia kwanza aachane na kuchungulia mitandao afanye yale ambayo yeye na JPM waliotuambia kutufanyia mpk tukawapa kandarasi ya miaka 5 kutufanyia.
 
Uongozi wa nchi yoyote umejengwa katika misingi ya mawazo ya watu wengi. Kwa kuwa zamani haikuwa rahisi kuweza kupata mawazo ya watu wengi kwa pamoja, mifumo ya uwakilishi iliundwa. Ndo maana tuna kamati za vijiji, baraza la madiwani, bunge etc. Msingi wa yote haya ni kupata mawazo ya watu.

Tekinolojia ya habari imekuwa na sasa ni rahisi kwa watu wengi zaidi kuchangia mawazo yao nje ya mifumo in real time. Na hili siyo jambo geni au jambo baya.

Serikali yoyote makini ni ile inayosikiliza na kufanyia kazi kasoro au maoni ya watu bila kujali yamewafikua kwa njia gani.

Hivyo basi isichukuliwe kama ni udhaifu serikali kufanyia kazi maoni yatu hapa.

Siku za usoni huwenda tukawa na platform maalumu za kidijitali kwa ajili ya kuishauri serikali na kutoa maoni.
 
Kama uimara au udhaifu wa Serikali na yeye amechangia kwa 100% kwani yeye alikuwa Makamu wa Rais mtu wa pili kwa mamlaka Tanzania mshauri number moja wa Rais pili angalia mambo yanavyochanganya toka alivyotoa siku 14 za maombelezo , kutengua uteuzi wwake mwenyewe chini ya masaa 24 kurudisha mawaziri wote wa mtangulizi wake mama anahitaji kutulia kwanza aachane na kuchungulia mitandao afanye yale ambayo yeye na JPM waliotuambia kutufanyia mpk tukawapa kandarasi ya miaka 5 kutufanyia
Mkuu hakuna binadamu aliyekamilika lakini hoja iko palepale, mama Sio mgeni serikalini.Kikubwa aongeze umakini zaidi hasa kwa washauri wake, watu Kama mwanasheria mkuu wa serikali na washauri wengine awaangalie Sana, wanaweza mpotosha. Ndio hao waliomshauri siku 14 za maombolezo badala ya 21.
 
Aache kuteua teua atulie Kwanza afanye nao kazi, hii teuateua isiyo kuwa na subira ndiyo matokeo yake ndiyo hayo,kwani lazima abadilishe watu wengi wakati muhula ulishaanza tangu mwaka Jana.
 
Kama uimara au udhaifu wa Serikali na yeye amechangia kwa 100% kwani yeye alikuwa Makamu wa Rais mtu wa pili kwa mamlaka Tanzania mshauri number moja wa Rais pili angalia mambo yanavyochanganya toka alivyotoa siku 14 za maombelezo , kutengua uteuzi wwake mwenyewe chini ya masaa 24 kurudisha mawaziri wote wa mtangulizi wake mama anahitaji kutulia kwanza aachane na kuchungulia mitandao afanye yale ambayo yeye na JPM waliotuambia kutufanyia mpk tukawapa kandarasi ya miaka 5 kutufanyia
Ulitaka aendelee na mawaziri waliowachwa na hayati JPM?
 
Aache kuteua teua atulie Kwanza afanye nao kazi, hii teuateua isiyo kuwa na subira ndiyo matokeo yake ndiyo hayo,kwani lazima abadilishe watu wengi wakati muhula ulishaanza tangu mwaka Jana.
Hoja ya kumpotosha hii...
 
Uongozi wa nchi yoyote umejengwa katika misingi ya mawazo ya watu wengi. Kwa kuwa zamani haikuwa rahisi kuweza kupata mawazo ya watu wengi kwa pamoja, mifumo ya uwakilishi iliundwa. Ndo maana tuna kamati za vijiji, baraza la madiwani, bunge etc. Msingi wa yote haya ni kupata mawazo ya watu.

Tekinolojia ya habari imekuwa na sasa ni rahisi kwa watu wengi zaidi kuchangia mawazo yao nje ya mifumo in real time. Na hili siyo jambo geni au jambo baya.

Serikali yoyote makini ni ile inayosikiliza na kufanyia kazi kasoro au maoni ya watu bila kujali yamewafikua kwa njia gani.

Hivyo basi isichukuliwe kama ni udhaifu serikali kufanyia kazi maoni yatu hapa.

Siku za usoni huwenda tukawa na platform maalumu za kidijitali kwa ajili ya kuishauri serikali na kutoa maoni.
Hauko sawa kiakili unakurupuka kama unaharisha mavi.
 
Back
Top Bottom