Tanzania government condemns Israel

Tanzania government condemns Israel

Umenena mkuu. Wababe ni lazima wapigwe vita kila mahali ama sivyo haki itapotea kabisa duniani. Napoleon, Hitler, Hirohito, Mussolini na wengine walitokomezwa pamoja na ubabe wao. Kama dunia Hitler asingepigwa vita sijui dunia hii ingekuwaje hadi leo. Israel isifikiri kwamba itaendelea na ubabe wake milele, na bila shaka sasa polepole inatambua kwamba the world is abandonig it, siyo kwa sababu nyingine isipokuwa ni ubabe wake tu. Siku moja itajikuta hata US itakuwa inamweka kwa mbali, ingawa hii haitakuja leo au kesho.

wengi wapo nyuma ya israel kuwasapoti, nyie wachache tu msio kuwa hata na nguvu ndo mnakuwa mnaongea sana. mnapoteza muda, fanyeni kazi kuondoa umasikini wa nchini kwenu...kama ukimwona mbabe, unatakiwa kula heshima, usipokula heshima mtu mwenyewe mbavu mbili, atakutwanga mara moja....kila kunapokucha, israel wanagundua silaha na technologia mpya...kwasasa wameshagundua technology ya kuiweka kwenye nchi yao yote, rocket za hamas na hezbohal kabla hazijafika chini ya ardhi, zitadakwa kwa makombora yaliyotegwa atomatically kwenye vituo vingi, yanayojifyatua yenyewe, na rocket zitavunjwavunjwa kulekule juu kabla ya kukida chini...zinadakiwa kulekule...

kumbuka osama na ujanja wake wote alikuwa na uwezo wa kuishambulia marekani lakini kwa israel amenyosha mikono, hadi akasema ngoja nimpige rafiki wa israel kwasababu kumpiga israel hata kuingia tu pale hawezi..fyata mkia..
 
Serikali yetu huwa inabahati ya kufanya mambo ya ajabu na maovu, haina bahati ya kufanya mambo mazuri na makini. Serikali ilishindwa kutoa tamko la PRK kuzamisha meli ya Korea kusini, haijatoa tamko kuuliwa wa wanaharakati Kenya wala DRC. Inakimbilia kutoa tamko katika suala tata la middle east. Si, ajabu wakaandaa maandamando weekend hii.
 
tuballaya.. ulitaka hizo meli zivunje naval blockade iliyowekwa na sovereign state kulinda usalama wake ili kiwe nini? ulitaka Israel wapishe tu kwa sababu ni "humanitarian aid"..hivi kweli unafikiri hakukuwa nanjia nyingine yoyote ya kupitisha misaada? Kwanini hawakulazimisha kupitisha misaada kwenye mpaka wa Misri na Gaza kwa kupiitisha magari kwa nguvu na tuone kama Misri wangeacha tu wapite kwa sababu hiyo hiyo.

Labda ni kwa sababu ya matatizo yanayoikabili CCJ, lakini Mwanakijiji unanishangaza sana kwa kulinganisha mpaka wa nchi kavu baina ya nchi na nchi -- na na access ya nchi katika open sea -- yaani eneo la bahari nchi inalolimiliki (territorial waters). Nchi yoyote inaweza kufunga mpaka wa nchi kavu kati yake na nchi nyingine kama kuna haja ya kufanya hivyo. Nchi nyingi hufanya hivyo mara kwa mara na si tatizo kubwa.

Lakini suala hapa ni ni naval blockade ya nchi nzima, eneo la bahari haki Gaza linalozuiliwa kibabe na Israel. By the way, Misri ilifungua mpaka wake na Gaza , bila shaka kwa agizo/amri ya Washington. Na yote hii ni kwa sababu ya mkate -- yaani Wamisri wanategemea sana mikate yao (yaani ngano) kutoka US. Hii ni chini ya makubaliano ya camp david ya 1979 kati ya Israel na Misri yaliyofanywa na Rais Jimmy Carter -- kwamba nchi hizi mbili zisipigane tena (baada ya kupigana vita mara nne huko nyuma).

Misri wanapata aid ya USD 3.5bn kila mwaka kutoka US (kwa kupitia wheat imports) na Israel inapata USD 7bn. Kwa hivyo Mubarak lazima afate amri ya wasington -- ikisema funga mpaka, bnasi hufunga mpaka, na ikisema fungua, basi inafungua. Wamiksri wanapata mikate kwa bei iliyoruzukiwa sana (subsided price) hivyo ikipanda bei thumni moja tu Mubarak yuko hatarini kung'olewa madarakani.
 
waache waandamane kwaajili ya waarabu, wakati watu darfu hapo wanakufa kwa njaa, wengi wao wakiwa wakristo na watu weusi wanaouwawa kama wanyama na janjaweed inayopigwa sapoti na rafiki mkubwa wa selikali yetu, al bashir....ni ajabu sana.
 
Labda ni kwa sababu ya matatizo yanayoikabili CCJ, lakini Mwanakijiji unanishangaza sana kwa kulinganisha mpaka wa nchi kavu baina ya nchi na nchi -- na na access ya nchi katika open sea -- yaani eneo la bahari nchi inalolimiliki (territorial waters). Nchi yoyote inaweza kufunga mpaka wa nchi kavu kati yake na nchi nyingine kama kuna haja ya kufanya hivyo. Nchi nyingi hufanya hivyo mara kwa mara na si tatizo kubwa.

Lakini suala hapa ni ni naval blockade ya nchi nzima, eneo la bahari haki Gaza linalozuiliwa kibabe na Israel. By the way, Misri ilifungua mpaka wake na Gaza , bila shaka kwa agizo/amri ya Washington. Na yote hii ni kwa sababu ya mkate -- yaani Wamisri wanategemea sana mikate yao (yaani ngano) kutoka US. Hii ni chini ya makubaliano ya camp david ya 1979 kati ya Israel na Misri yaliyofanywa na Rais Jimmy Carter -- kwamba nchi hizi mbili zisipigane tena (baada ya kupigana vita mara nne huko nyuma).

Misri wanapata aid ya USD 3.5bn kila mwaka kutoka US (kwa kupitia wheat imports) na Israel inapata USD 7bn. Kwa hivyo Mubarak lazima afate amri ya wasington -- ikisema funga mpaka, bnasi hufunga mpaka, na ikisema fungua, basi inafungua. Wamiksri wanapata mikate kwa bei iliyoruzukiwa sana (subsided price) hivyo ikipanda bei thumni moja tu Mubarak yuko hatarini kung'olewa madarakani.

misri ilifungua blockade yake ili kuonyesha kuwa inajali kuwaridhisha waarabu kwasababu wanapiga kelele mno...wala si kwasababu ya mkate unaokuja kwenye akili yako...Gaza ni eneo hatari sana kwa usalama wa israel kwasababu kuna kundi ambalo haiitambui israel na wanataka kuiondoa israel kwenye raman ya dunia, israel hawatakuja kukubali holocost ingine itokee maishani mwao na prevention is better than cure, kulinda usalama wao, wameweka blockade ili kuhakikisha mizigo inayoenda gaza ni salama,...kama wasingekuwa na wasiwasi huo, hii yote isingetokea..

Camp David accord haikuwa kwaajili ya misri kutokuja kupigana tena na israel...ni kwamba misri uwezo huo hawana, walishashindwa mama ninyi, na uchumi wao hauruhusu...labda kidogo uliposema misri ni nchi ya pili duniani kwa kupokea pesa nyingi toka marekani hapo nakubaliana na kwasababu wao ni waarabu masikini tu, wanaogopa kukosa pesa za bure hizo..inabidi wawauze waarabu wenzao kwa pesa.kama si ujinga wao ninini? nani wa kumlaumu?...

blockade inatambuliwa kimataifa, na israel si wa kwanza kuweka blockade...anayekuja kwa amani hupokelewa kwa mani na anayekuja kwa fujo hupokelewa kwa fujo...acha fikra za kidini..
 
Miafrika bana! lol utumwa wa akili hautakwisha - taabu kweli kweli. Hivi Nyerere alipokuwa akilaani vitendo vya Israel alikuwa kama nani?

Wakuu vilevile wakati tunajadili tamko la Serikali pia tuangalie uhusiano (kihistoria) kati ya Israeli na Tanzania tangu serikali ya awamu ya kwanza hadi sasa. Uhusiano huo umebadilika au hapana? Na kama umebadilika labda serikali ilitakiwa kutoa tamko gani mbadala.

Mimi binafsi ninaona kama miaka ya hivi karibuni (ninamaanisha kuanzia miaka ya 90) serikali haikuendelea na misimamo yake katika nyanja za kimataifa kama ilivyokuwa kwa serikali ya awamu ya kwanza. Hapa ninamaanisha uhuru wa kusimamia ukweli na haki kama nchi na haijalishi kama nchi ni masikini au tajiri. Ninaamini heshima Tanzania inayoipata sasa hivi katika mahusiano ya kimataifa ilitokana na hayo yaliyofanywa kipindi nyuma na ninafikiri itakuwa vyema kuiendeleza heshima hiyo kwa kusimamia ukweli na haki na kuendelea kutoa matamko katika maswala mbalimbali ya kimataifa.
 

Asante Mkuu Ubungoubungo kwa kutuonyesha huto tusilaha tulikosemekana tulikutwa ndani ya meli za wanaharakti – yaani jambia, visu, nondo etc, ambavyo umeamua kuvifanyia promotion kubwa. Pia kuna uwezekano hizo zana zilikuwa planted na maajenti wa Israel, hasa ikizingatiwa kwamba kulitokea blackout of news baada ya meli kushambuliwa, except journalists imbedded with Israel forces.

Lakini tukubali kwamba hizo zana zilikutwa among the activists in the ships. Sasa Mkuu, mbona hujatuletea video za silaha walizotumia IDF-destroyers, helicopters, machineguns, stun guns, grenades -- kwa ulinganisho?

Halafu usisahau tena –- unapenda sana kusahau: Israel forces wali-descend upon the decks of the ships and started firing. Wenyewe Israel (msemaji wao wa kijeshi) alisikika akisema kwamba askari wao walipodescend walianza kushambuliwa kwa nondo, visu etc, na wao wakajibu on self defence kwa kutumia silaha kali. Who started the whole incident? israel sodiers who descended on the activists.

Kwanza mimi sikuelewa vyema, nilifikiri activists ndiyo walikwenda kwenye meli ya kivita ya Israel na kuanza kuwashambulia Israel soldiers. Kumbe ni kinyume chake!
 
Kuna watu humu wanajichanganya tu kuhusu suala la Gaza -- bila shaka wanaendeshwa kwa chuki tu. Wao wanaona kuwa Wagaza kwa kuwa ni dhaifu, ni lazima wafate amri ya Israel, kwani hawafui dafu kwao. Si wadhaifu wengi wako tayari kulikubali hili. In fact ni sign ya defeatism, na kwa mpambanaji wa haki, lugha hiyo hawana. Wangekuwa nayo, wapigania uhuru wa kizalendo Kusini mwa Afrika (Namibia, Afrika ya Kusini na Zimbabwe wasingejikomboa kutoka kwa Wazungu hadi leo. Si wangesema tu "Ah, hao hatuwawezi bwana, wana silaha kali, bora tukafata amri tu."

Hawakufanya hivyo. Vivyo hivyo Wagaza (au tuseme Wapalestina kwa ujumla) hawaezi kusema basi, mwenye nguvu mpishe. Aidha kuna baadhi wanasema kwamba kama Wazungu wasingekubali kuondoka madarakani huko Afrika ya Kusini, wazalendo wangeanza kujilipua. Perhaps.

Lakini kwa kumalizia naweza kusema kuwa katika miaka ya 70 na 80, sikutegemea kabisa iwapo wazalendo wangejitawala Afrika ya Kusini, namibia na Zimbabwe. wakati huo ilikuwa hali mbaya sana kwa wazalendo, has ikizingatiwa kuwa nchi za Magharibi, hasa Marekani ilikuwa inawaunga mkono sana wazungu wao kule.
 
wamejitahidi kuandika ili kuwapoza "WATU FULANI HIVI.."sitaki kuwataja, hapa tz..wala haitoki moyoni...kwasababu hawana point hata moja..to be fair, kitu ambacho walitakiwa kukisema ni kwamba, israel walitakiwa kuwa wapole kidogo na wangewavumilia wale watu wakaidi waliokuwa wanataka international publicity....ila sio kusema kuwa kulikuwa na clear violation of international law...HIVI HAWA VILAZA wanasheria wa wizara ya mambo ya nje ni kina nani?...ni mwanasheria gani anaweza kuongea kuwa umevunja kifungu cha sheria bila kukitaja? which international humanitarian law israel has violated? they were supposed to mention it jamani au siyo....sasa hao wanasheria walioko wizara ya mambo ya nje, hawajui sheria za kimataifa? kama wanajua mbona hawajataja? kama hawajaitaja, je ipo iliyovujwa? kama ipo, naomba nipeni ipi sheria imevunjwa hapo..HAKUNA SHERIA YA KIMATAIFA IMEVUNJWA HAPO na selikali yetu inaonyesha namna gani ilivyo kilaza kwa kila kitu kuanzia mambo yetu sisi wenyewe ya ndani hapahapa hadi kwenye mambo ya kimataifa... pia, kwani israel ina wahusu nini Tz wakati tangu zamani Tanzania amekuwa adui wa israel? ndio maana israel waliweka ubalozi Kenya, ubalozi mkubwa tu...lakini Tz hakuna ubalozi,...kuna kaofisi tu ambako kanatusaidia sisi wakristo tunapokwenda kutembelea israel, nakama wakristo tusingekuwa tunapata shida kwenda kenya kupata visa, hata hako kasingekuwepo kwasababu moja ya nchi ambazo Israel wanajijua si marafiki ni Tanzania, sasa maneno yanawatoka mdomoni kwa watu ambao hata hawana uhusiano nao....hawa ni wagumu wa kufikiri kwenye selikali yetu..KAMA KUNA MTU ANAJUA ISRAEL WAMEVUNJA SHERIA YA KIMATAIFA AITAJE HAPA ILI NA MIMI NIMWAMBIA UKWELI ULIVYO...acheni soga za kina kikwete... however, kama nilivyosema mwanzo, walikuwa wanajikosha tu kuwaonyesha watu fulani kuwa wanajali...ila hawana hata msingi wowote kuongea kama walivyoongea, labda wangekuwa wamesema kuwa israel walitakiwa kuwa wapole kidogo na sio kusema wamevunja sheria ya kimataifa, kuongea hivyo wameonyesha ukilaza na umbumbumbu wa kutokua sheria ya kimataifa,wangeenda kumwuliza hata Prof Mainda peter pale udsm nafikir angewasaidia...

Vitendo vinavyofanywa na Israel havihitaji weledi wa kisheria kujua kama ni kosa. Maneno yako yanaonesha we ndie mwanasheria kilaza
 

Asante Mkuu Ubungoubungo kwa kutuonyesha huto tusilaha tulikosemekana tulikutwa ndani ya meli za wanaharakti – yaani jambia, visu, nondo etc, ambavyo umeamua kuvifanyia promotion kubwa. Pia kuna uwezekano hizo zana zilikuwa planted na maajenti wa Israel, hasa ikizingatiwa kwamba kulitokea blackout of news baada ya meli kushambuliwa, except journalists imbedded with Israel forces.

Lakini tukubali kwamba hizo zana zilikutwa among the activists in the ships. Sasa Mkuu, mbona hujatuletea video za silaha walizotumia IDF—destroyers, helicopters, machineguns, stun guns, grenades -- kwa ulinganisho?

Halafu usisahau tena –- unapenda sana kusahau: Israel forces wali-descend upon the decks of the ships and started firing. Wenyewe Israel (msemaji wao wa kijeshi) alisikika akisema kwamba askari wao walipodescend walianza kushambuliwa kwa nondo, visu etc, na wao wakajibu on self defence kwa kutumia silaha kali. Who started the whole incident? israel sodiers who descended on the activists.

Kwanza mimi sikuelewa vyema, nilifikiri activists ndiyo walikwenda kwenye meli ya kivita ya Israel na kuanza kuwashambulia Israel soldiers. Kumbe ni kinyume chake!

Bwana mdogo, nakupa fanya experiment moja, chukua jambia moja, kaa barabarani, ukiona kuna gari ya wanajeshi inakuja kwako, chukua jambia anza kuwakata wanajeshi, chukua nyundo na marungu wapige wale wanajeshi, kamata wengine weka katikati ya barabara ili wafe kwa kugongwa, alafu utasikilizia wale wanajeshi wenye silaha kama watasema wewe huna silaha nzito....utapata cha mtema kuni...

video inaonyesha wazi kuwa activists walikuwa violent, waliwapiga wanajeshi wa israel waziwazi mwenyewe umeona, walianza kurusha risasi baada ya kuona wale makomandoo walioshukia kwenye meli wamepigwa na wanarushwa baharini na hao unaowatetea...ulitegemea israel watulie tu wakati wana silaha nzito kuwaacha makomandoo wao kutumbukizwa kwenye maji? mnatoa povu bure bila kufikiri akili kumkichwa..
 
😛ainkiller:wamejitahidi kuandika ili kuwapoza "WATU FULANI HIVI.."kwani israel ina wahusu nini Tz wakati tangu zamani Tanzania amekuwa adui wa israel?

Ni uungwana tuu wa kawaida kwa nchi kutoa kauli ya pongezi au masikitiko pindi yanapotokea matukio yasiyo ya kiungwana duniani kama hili la uvamizi wa Makomandoo wa Israel dhidi ya Meli ya Kituruki.

Sasa kama Wizara ya Mambo ya Nje imefanya hivyo, ubaya uko wapi? mambo mengine madogo kama haya wala haifai kuyalalamikia.

Na hii hoja yako kwamba mbona Israel haina Ubaozi Tanzania, mimi nadhani haina uzito sana. kwa hiyo kama Israel inaoperate from Nairobi so what? kwani ni lazima kila nchi iwe na Ubalozi Tanzania ndio kiwe kigezo cha uhusiano na ushirikiano wa karibu zaidi na urafiki.? Mbona hata Tanzania haina Ubalozi wake Israel na imekuwa ikishirikiana vizuri tuu na Israel katika masuala mbalimbali? Mimi nadhani si vyema kulalamikia tuu kila jambo.

Kuhusu sheria gani ya kimataifa iliyovunjwa kwa shambulio hilo, kwani ndugu yangu wewe hufahamu kwamba kitendo tuu cha kuishambulia kijeshi meli ya kiraia na kupoteza maisha ya raia wasio na hatia waliokuwemo kwenye meli ile (Mavi Marmara) ni kinyume cha sheria? Au kwa vile hapakuwa na Mtanzania mule ndani basi ndio Serikali ikae tuu kimya? Umesahau kwamba Tanzania pia inao askari wake waliopo katika ulinzi wa amani chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa huko Darfur na Lebanon? Hivi kwa bahati mbaya litokee tukio la kikatili kama lililofanywa na Makomandoo wa Israel dhidi yao halafu dunia ikae tuu kimya bila kulaani? Nadhani huo hautakuwa uungwana. Big up Waziri Membe na Wizara ya Mambo ya Nje kwa kuungana na nchi nyingine duniani pamoja na viongozi wengine katika kulaani kitendo hiki cha Israel...
 
Bwana mdogo, nakupa fanya experiment moja, chukua jambia moja, kaa barabarani, ukiona kuna gari ya wanajeshi inakuja kwako, chukua jambia anza kuwakata wanajeshi, chukua nyundo na marungu wapige wale wanajeshi, kamata wengine weka katikati ya barabara ili wafe kwa kugongwa, alafu utasikilizia wale wanajeshi wenye silaha kama watasema wewe huna silaha nzito....utapata cha mtema kuni...

video inaonyesha wazi kuwa activists walikuwa violent, waliwapiga wanajeshi wa israel waziwazi mwenyewe umeona, walianza kurusha risasi baada ya kuona wale makomandoo walioshukia kwenye meli wamepigwa na wanarushwa baharini na hao unaowatetea...ulitegemea israel watulie tu wakati wana silaha nzito kuwaacha makomandoo wao kutumbukizwa kwenye maji? mnatoa povu bure bila kufikiri akili kumkichwa..



Mheshimiwa, your are as elusive as an eel -- unakwepa kujibu hoja hii ya msingi ya counterpunch. Nairudia hapa in red.: Halafu usisahau tena –- unapenda sana kusahau: Israel forces wali-descend upon the decks of the ships and started firing. Wenyewe Israel (msemaji wao wa kijeshi) alisikika akisema kwamba askari wao walipodescend walianza kushambuliwa kwa nondo, visu etc, na wao wakajibu on self defence kwa kutumia silaha kali. Who started the whole incident? israel sodiers who descended on the activists.

Kwanza mimi sikuelewa vyema, nilifikiri activists ndiyo walikwenda kwenye meli ya kivita ya Israel na kuanza kuwashambulia Israel soldiers. Kumbe ni kinyume chake!
 
Hiyo shutuma ya Tanzania dhidi ya Israel mimi wasiniweke kabisa ni bora wangekaa kimya; kwani nani angetulaumu kwa kukaa kimya? Tunapiga makelele kama vile tunataraji kitu kwa kujiingiza kwenye malumbano ya hao Waturuki Vs Israel. Mbona Kenya, Uganda, Rwanda, na Burundii wamekaa zao kimya na wako poa tu?
Mkuu kwani hujui kura za membe baada 2015 zitatoka wapi?
Kwani ni mara ya kwanza kutoa kauli tata? Jiulize
 
😛ainkiller:wamejitahidi kuandika ili kuwapoza "WATU FULANI HIVI.."kwani israel ina wahusu nini Tz wakati tangu zamani Tanzania amekuwa adui wa israel?

Ni uungwana tuu wa kawaida kwa nchi kutoa kauli ya pongezi au masikitiko pindi yanapotokea matukio yasiyo ya kiungwana duniani kama hili la uvamizi wa Makomandoo wa Israel dhidi ya Meli ya Kituruki.

Sasa kama Wizara ya Mambo ya Nje imefanya hivyo, ubaya uko wapi? mambo mengine madogo kama haya wala haifai kuyalalamikia.

Na hii hoja yako kwamba mbona Israel haina Ubaozi Tanzania, mimi nadhani haina uzito sana. kwa hiyo kama Israel inaoperate from Nairobi so what? kwani ni lazima kila nchi iwe na Ubalozi Tanzania ndio kiwe kigezo cha uhusiano na ushirikiano wa karibu zaidi na urafiki.? Mbona hata Tanzania haina Ubalozi wake Israel na imekuwa ikishirikiana vizuri tuu na Israel katika masuala mbalimbali? Mimi nadhani si vyema kulalamikia tuu kila jambo.

Kuhusu sheria gani ya kimataifa iliyovunjwa kwa shambulio hilo, kwani ndugu yangu wewe hufahamu kwamba kitendo tuu cha kuishambulia kijeshi meli ya kiraia na kupoteza maisha ya raia wasio na hatia waliokuwemo kwenye meli ile (Mavi Marmara) ni kinyume cha sheria? Au kwa vile hapakuwa na Mtanzania mule ndani basi ndio Serikali ikae tuu kimya? Umesahau kwamba Tanzania pia inao askari wake waliopo katika ulinzi wa amani chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa huko Darfur na Lebanon? Hivi kwa bahati mbaya litokee tukio la kikatili kama lililofanywa na Makomandoo wa Israel dhidi yao halafu dunia ikae tuu kimya bila kulaani? Nadhani huo hautakuwa uungwana. Big up Waziri Membe na Wizara ya Mambo ya Nje kwa kuungana na nchi nyingine duniani pamoja na viongozi wengine katika kulaani kitendo hiki cha Israel...

meli ya raia kisheria inaweza kushambuliwa kama itakuwa imegeuzwa kuwa military object, ndege ya raia au hata magari ya raia, kama kutakuwa na military necessity kwasababu imegeuzwa kuwa military object inaweza kushambuliwa ktk sheria za kimataifa, soma sanremo manual on international law of conflicts at sea...utaelewa...just google "international humanitarian law"...pdf utapata material mengi sana ya kukusaidia kuelewa kuwa, wakati mwingine vitu vingine vinakuwa ni civilian objects lakini vinaweza kugeuzwa kuwa military objects kama kutakuwa na necessity ya kivita..ndio maana unaona hadi leo hii, magaidi wa iraq wakijificha kwenye misikiti wakawa wanapanga njama zao toka mle, msikiti mzima unalipuliwa hata kama kuna watu alimradi tu onyo lilitolewa...hawa jamaa onyo liilitolewa na zaidi sana international humanitarian law haikuwa applied sana, zaidi ya yote walikuwa kwenye ''SELF DEFENCE" kutokana na kushambuliwa walipoishukia meli...

NAFIKIR KWA NJIA HII NITAKUWA NIMEMSAIDIA JAMAA ALIYEULIZWA SWALI..ubungo ubungo naomba kama una uelewa kidogo na hizi sheria, nenda nao taratibu hawa jamaa kwasababu naona tunataka kuharibu kama tukienda kwa chuki...asante..
 
Mkuu kwani hujui kura za membe baada 2015 zitatoka wapi?
Kwani ni mara ya kwanza kutoa kauli tata? Jiulize

Mkuu umenikumbusha zile pesa za shetani alizokuwa anadai tutazipata kwa kuwa na uhusiano na Taasisi fulani ya Kidini.
 
Mjadala huu ni muhimu sana maana unatuonyesha political psych ya watanzania wapya. Unapoona hata "wapambanaji" na "wazee wa principles" wanakuwa tayari kuchukua upande wa wababe dhidi ya wanyonge ujue hapo kuna tatizo kubwa kwa mustakabali mzima wa "ukombozi"...Inapofikia "wazalendo" wanapoona serikali yao inapaswa kukemea ubabe wanaofayiwa wanyonge wa "aina yao" na sio wanapofanyiwa ubabe "wanyonge wengineo" ni rahisi kutambua ni wapi uzalendo/wazalendo wa aina hiyo unapotupeleka.

omarilyas
 
jamani sie Watanga na Nyika kweli sasa nimeamini, haya sasa yakwetu yametushindwa tunarukia ya watu, is it true kwamba hatuna mambo yetu makubwa hadi tuingilie yasiyotuhusu?? Hivi kweli Sisimizi anaweza akamlaumu Tembo hata siku moj au nikutaka tu kuingilia mambo yasiyotuhusu???

Au nikubaliane na mchangia hoja hapo juu kuwa Tanzania imefanya hivyo ili kuwaridhisha tu watu flani......? Nadhani pia hii inawezekana hasa ukizangatia mikutano ya DINI inayofanywa na Mwakasege ambaye amekuwa akiitetea Israel sikuzote.....naamini swala si Israel, kuna jambo lingine
 
Mkuu Omaryas kuna kazi kubwa sana iliyoko mbele yetu kutokana na Elimu ya kukariri ambayo ni ya Kitumwa.
Nyerere alisema ili tuendelee tunahitaji 1. WATU....na watu wenyewe ndio hawa....
Miaka 49 ya Uhuru tuko nyuma zaidi na mawazo kama haya ndizo sababu kubwa. For any changes hata kama tuna Uongozi bora bado WATU wamesimama namba moja.. Kwa mawazo kama haya ya kushikiwa, tumefikia hadi kusema mbona wazungu wa mataifa makubwa hawajasema lolote! meaning we can't tell what's wrong kabla wazungu hawaja comment! as if hatuna akili zetu wenyewe kufanya maamuzi..
Je, tunategemea vipi nchi yetu kuendelea!!
 
Ndiyo tatizo la kuwa na watawala (membe na timu yake) wasio jua nini cha kufanya. Israel inaiona Tanzania kama sisimizi.
 
Back
Top Bottom