..nimefanya ka-research kadogo nikakuta kwamba Zambia wana miradi ya reli kwenda Angola[benguela railway], na mradi mwingine wa reli kwenda Mozambique[nacala port].
..pia nimegundua kwamba wa-Zambia hawana haraka ya kufufua Tazara kwasababu wanaona reli hiyo ni ndefu na haina ufanisi.
..jambo lingine ni kwamba jirani yao upande wa magharibi, yaani ANGOLA, ana mafuta na mapesa mengi mno. sasa it makes more sense kwao kujenga miundo mbinu kama reli kuelekea Angola ambako kuna visima vya mafuta.
..Angola pia wana mradi wa kurefusha reli yao mpaka jimbo la Katanga in DRC. tayari mradi huo umeshaanza kutekelezwa kwa kutumia mapato ya mafuta na gesi ya Angola.
..Malawi wana mpango wa kuimarisha reli kuelekea bandari ya Nacala ya Mozambique. Mtakumbuka tulikuwa tuna mipango ya kutumia bandari ya Mtwara kuhudumia Malawi.
..kwa kifupi Tanzania tunahitaji kutimua mbio sasa hivi, kwasababu wenzetu wameshatangulia.
cc Koborer, Ogah, Masanja, Ritz, Mdondoaji, NasDaz, Nguruvi3, Ngongo
Joka Kuu,
Hii nchi kwa ilipofikia hakuna mtu atakayeweza kuikwamua ilipo. Tukozaidi kibanafsi kuliko kimaslahi ya nchi. Tunaenda kujenga bandari ya bagamoyo kubwa tunaiacha bandari ya dar ikipoteza ufanisi wake na umakini. Tunaiacha bandari ya mtwara iliyokuwa na kina kirefu kuliko vyote na natural harbour. Tunaiacha bandari ya Tanga. Tumeshindwa kuimarisha reli tunabakia kuongeza idadi ya malori ya kubeba makontena kisa inawapatia vipato watu fulani fulani. Mwisho wa siku ufanisi hakuna, barabara zinaharibika na taifa linaporomoka kiuchumi. Uchumi wetu unakuwa kwa kasi kwasababu ya uwekezaji na siku wawekezaji wakipungua na uchumi nao unaporomoka (kama mnakumbuka 2009 wakati wa mdororo wa kiuchumi).
Tatizo kubwa la nchi ni ufisadi na kushindwa kwetu kupunguza na kuondoa ufisadi if possible. Kila mtu ni fisadi sasa Tanzania mpaka watchmen anahongwa hela anaruhusu watu walale au wageuze lindo lake liwe guest house. Taifa limekuwa kama yatima halina mtetezi zaidi ya kubakia lipo lipo tu.
Hivyo Joka Kuu wacha majirani watukimbie we are not serious at all in so many issues. Our seriousness ipo katika madili ya 10% basi.