Tanzania confirms TAZARA split, Zambia not aware

Tanzania confirms TAZARA split, Zambia not aware

TAZARA imekuwa domant kwa miaka miingi sana. Sioni kazi yake mpaka sasa. Zaidi kunatakiwa kuifanya iwe na uwezo mkubwa zaidi hasa kufanya kazi ya kusafirisha mizigo yote kutoka huko Nyanda za juu na kujenga maghala katika kila mkoa ambayo yatatumika kubeba mzigo kutoka bandarini.

Kwa namna ilivyo haina kitu. Tunakokwenda itabaki kama reli ya Arusha.
 
Nilikuwa ninajaribu kuwaza kwa sauti tu mkuu. Maana hats migodi hatuna share an jirani lakini haitusaidii. Tuna teli ya Kati nayo haitusaidii, nayo ndiyo tena. Hatuna mfano was kuonyesha kuwa tuki stand Aline Luna tuwezacho.
What if Zambia nao wakiamua kujenga reli kuelekea Mozambique?
Ninasema kuwa ninawaza kwa sauti kwa kuwa ninaamini sina uelewa mzuri juu ya saga hii, lakini kadili mjadala unavyoendelea nina hakika kuna vitu Nita catch up, pia kauli ya waziri no muhimu.
Yaani tuondokane na mawazo mgando kuwa ili reli zetu zifanye kazi lazima ziunganishwe na nchi jirani!!! nchi yetu ni kubwa sana tunaweza kuendesha wenyewe..kwa faida zetu za kiuchumi..watu bado mnalalamika tu wakati hatua za kurekebisha kasoro zinachukuliwa kama hiyo ya ku-split tzr kama ni kweli badala ya kuongelea the best way ya kuitumia hiyo reli mijitu inalalamikia nchi za jirani au mnalipwa!!!usafiri wa kusini nyanda za juu unaweza ukaimarika sana pengine ukachukua muda mfupi zaidi kufika mbeya na mikoa mingine kama tzr itawekezwa ndani ya TZ nakubakiza kipande cha zambia kwa matumizi yao kama watahitaji!!!
 
Mhhh!!!! Hivi walishakaaa name kushauliana kabla hawajaamua mi naamini tz ni watu wa diplomasia kutengana haitasaidia hivi ziko wapi meli za mtwara; iwapi reli ya kati, na atcl haaaaaa du hata name uda nayo tumeipoteza. If u fail plan, U plan to fail.....mi naamini hapa tu si bahati mbaya ni mipango mibaya ya watu
 
Reli ya kuvurugaTAZARA ilijengwa maalum kwa ajili ya kusafirisha mizigo ya Zambia na Malawi. Mbeya sio tu hakuna abiria wa kujaza train kwa vile watu wanapendelea mabasi na saizi middle class wanapanda ndege, hakuna mizigo ya kutosha kwenda Mbeya toka Dar ya kuwezesha kuendesha reli profitably. Kiwanda pekee kinachouza nje ya Mbeya ni Mbeya Cement, TBL wanazalisha bia za kutumika hukohuko tu. Kwa mantiki hiyo kuitenganisha TAZARA na Zambia na Malawi ni sawa na kuipeleka kibra.

Ndio shida ya kuokoteza wanasiasa kuongoza sekta muhimu za kiuchumi. Anyway labda wanaendeleza kampeni yao ya kuhakikisha malori ya akina Riziwani yanakuwa na mizigo ya kutosha kupeleka Zambia na
 
Yaani tuondokane na mawazo mgando kuwa ili reli zetu zifanye kazi lazima ziunganishwe na nchi jirani!!! nchi yetu ni kubwa sana tunaweza kuendesha wenyewe..kwa faida zetu za kiuchumi..watu bado mnalalamika tu wakati hatua za kurekebisha kasoro zinachukuliwa kama hiyo ya ku-split tzr kama ni kweli badala ya kuongelea the best way ya kuitumia hiyo reli mijitu inalalamikia nchi za jirani au mnalipwa!!!usafiri wa kusini nyanda za juu unaweza ukaimarika sana pengine ukachukua muda mfupi zaidi kufika mbeya na mikoa mingine kama tzr itawekezwa ndani ya TZ nakubakiza kipande cha zambia kwa matumizi yao kama watahitaji!!!

Huko kusini nyanda za juu mna nini cha kusafirisha kwa reli kama hata LIFT ya kwenye ghorofa mmezindua June 2014??
 
Usichanganye mambo!!! kama huelewi kitu ni bora kukifuatilia au kuomba mwenye taarifa rasmi ya huo mpango mzima amwage data hapa ili tujue, pengine ni kwa manufaa ya TZ.Tazara kama ilivyo kwa sasa haina faida yeyote na wawekezaji hawawezi kuingia kitu ambacho kimeganda kama barafu...yaani Dar to Kapirimposhi only..Tanzania inaweza kunufaika kama TZR itakuwa diversified. Pengine wenzetu bado hawako tayari kwa mfano kuweka express train from Dar to Mbeya ambayo itaongeza uzalishaji kwenye mikoa ya kusini..sasa kama Zambia hawataki kuwekeza zaidi tufanyeje..???
Mi naunga mkono hoja and is the step towards the right direction..Nyie watu wa kaskazini kazi yenu kupinga kila kitu..mpaka mkataba afanye Mtei na Mbowe ndo mnaona wa akili...

Kama huelewi vitu bora kukaa kimya kuliko kujiaibisha hapa. Pale Kapiri Mposhi kuna mtandao wa reli wa kisasa kwenda Ndola kwenye copper belt na nyingine inaenda Lusaka. Mizigo yote ya Zambia inafika vizuri kwa TAZARA kuliko njia zingine. Sasa hivi foleni ya malori pale boda Tunduma imefika hadi Mpemba, kilomita 15, gari zinakaa hadi siku mbili kusubiri kuvuka boda wakati kwa train ni dakika kumi tu train inatoka Tunduma na kuingia Nakonde then Isoka. Reli toka ipewe mtaji na wachina wakati inaanzishwa haikuwahi kuongezewa mtaji zaidi ya msaada wa vichwa toka ujerumani. Faida inayopatikana watu wanaifanyia ufisadi, wameuza hadi nyumba za TAZARA then mnasema TAZARA itaendelea kwa kugawanyika? No way, hii nchi ina laana kubwa sana ya kubaki maskini
 
UNACHEZEA LUGHA YA MALKIA WEWE? lakin mwakyembe nae INGLES haipand kwani?
 
Mkuu Ogah kwanza nianze kuunga mkono bandiko lako hakika wengi wetu humu hatujui kwanini Tanzania inachukua msimamo wa kila nchi kuendesha TAZARA kivyake.

Kwa muda mrefu sana kumekuwa na urasimu usio na faida hasa toka upande wa Zambia linapokuja suala la uendeshaji wa TAZARA.Sheria na taratibu za uendeshaji TAZARA ni lazima mtendaji mkuu atoke Zambia na msaidizi ndio atoke Tanzania hii imesababisha TAZARA kuendeshwa kwa matakwa ya Zambia.Mfano Tanzania ilitaka kutumia miundombinu ya TAZARA kwaajili ya usafiri wa Dar Zambia wakagoma,Tanzania ilitaka kuongeza safari za treni za ndani kuanzia Dar hadi Mbeya baada ya route hiyo kubainika itaongeza faida maradufu Zambia ikakataa.Masuala ya fedha lazima yapate baraka toka Zambia matokeo yake unakuta fedha nyingi za TAZARA zimerundikana katika account za TAZARA Zambia na kusababisha uzorotaji wa utoaji wa huduma pasipo sababu za msingi.

Muundo wa sasa wa TAZARA umepitwa na wakati kwakuwa ulijikita zaidi katika masuala ya siasa badala ya biashara.Naungana na Dr Mwakyembe katika kuligawa shirika hili ili kuongeza ufanisi zaidi.

Mkuu......inawezekana sisi tukawa wajinga sana lakini.....tufike mahali hawa majirani zetu.... should not take us for a ride...! to hell na huo ujirani ambao hauna mutual benefit......yaani tusifanye mambo yetu kisa lazima tum-consult jirani.....yaani tusifanye safri za ndani mpaka tuwa-consult Zambia!!.....
 
Last edited by a moderator:
Yaani mawaziri wetu ni waongo waongo kama boss wao, majuzi hapa mwakyembe katoka kuzungumza na vyombo vya habari nikamsikia kwa masikio yangu mwenyewe anasema kwamba nchi mbili hizi zimekubaliana kulipa malimbikizo ya mishahara leo anakuja na issue ingine,

haya sasa wazambia wanasema hii kitu haikujadiliwa.

Kikwete uondoke utuachia nchi yetu salama, uondoke kwenye uongozi salama tafadhali, historia yako ya uongozi Taifa hili imegubikwa na uharibifu mtupu.
 
Zambia is simply no longer interested in TAZARA. The time when it was a necessity for them has long passed. They can now export their copper through South Africa and they are busy exploring the Beira route through Mozambique. The time when Tanzania was doing things politically rather than economically has also long gone.
The nonsense that TAZARA general manger should always be a Zambian does no longer hold water. Since Zambia has shown very little desire to improve TAZARA, we should simply go alone. A split will eventually benefit Tanzania economically. We should start thinking of developing a proper railway network in the country. Its cheaper than roads and uplifts the economy much faster than roads as the transportation costs are greatly reduced.
The improvement of the central railway to a standard gauge should be part of the whole plan where the two railway lines can be connected. Meanwhile, why not extend TAZARA to Ruvuma through Makambako all the way to Mtwara port and Sumbawanga through Tunduma? Just as we are saying we going to connect all regions by tarmac, we should in fact start the connection by railways!
 
Mkuu Ogah kwanza nianze kuunga mkono bandiko lako hakika wengi wetu humu hatujui kwanini Tanzania inachukua msimamo wa kila nchi kuendesha TAZARA kivyake.

Kwa muda mrefu sana kumekuwa na urasimu usio na faida hasa toka upande wa Zambia linapokuja suala la uendeshaji wa TAZARA.Sheria na taratibu za uendeshaji TAZARA ni lazima mtendaji mkuu atoke Zambia na msaidizi ndio atoke Tanzania hii imesababisha TAZARA kuendeshwa kwa matakwa ya Zambia.Mfano Tanzania ilitaka kutumia miundombinu ya TAZARA kwaajili ya usafiri wa Dar Zambia wakagoma,Tanzania ilitaka kuongeza safari za treni za ndani kuanzia Dar hadi Mbeya baada ya route hiyo kubainika itaongeza faida maradufu Zambia ikakataa.Masuala ya fedha lazima yapate baraka toka Zambia matokeo yake unakuta fedha nyingi za TAZARA zimerundikana katika account za TAZARA Zambia na kusababisha uzorotaji wa utoaji wa huduma pasipo sababu za msingi.

Muundo wa sasa wa TAZARA umepitwa na wakati kwakuwa ulijikita zaidi katika masuala ya siasa badala ya biashara.Naungana na Dr Mwakyembe katika kuligawa shirika hili ili kuongeza ufanisi zaidi.

Haya ndiyo aina ya majibu yanayohitajika. Yanaleta mwanga name kysaidia kuuona ukweli.
Thumb up.
 
Last edited by a moderator:
While the West is uniting, Tanzania is busy splitting from her neighbors. One day, you will regret Tanzania. You can not stand by yourself.

Are you sure we cant stand on our selves?
 
Tukishavunja umoja na zambia reli itakufa kama ya kati ili wenye malori wanufaike.

Kweli hawa wafanyabiashara wa malori wana nguvu sana
 
Upumbavu zaidi ni kuilalamikia Zambia wakati TZ ndiyo iliyoshika mpini. Fursa zote za kuiburuza Zambia katika TAZARA zipo, na ni za asili. Tatizo ni kukosa mawazo yenye muelekeo huo. Wakulima wana msemo kuwa ''mtu mvivu hatawahi shambani alfajiri na mapema akisingizia uwepo wa wanyama wakali njiani" Uvivu tu kuanzia kufikiri hadi kutenda!

We have trade with care. Hoja za Zambia zipo based kwenye sheria/mikataba ya uanzishwaji wa TAZARA. Mfano agreement ilikuwa nchi ikitoa makao makuu, meneja atoke upande wa pili. Tanzania imekuwa ikijaribu kuwashawishi ili wakubali meneja mkuu aajiriwe kwa sifa na ikiwezekana hata toka nje ya nchi hizi lakini jamaa wapo stubborn kwa sababu wananufaika kwenye maamuzi. Kuna mmoja angefungwa baada ya wakili Prof Issa Shivji kuwatetea wafanyakazi wa TAZARA upande wa Tz.
Nadhani ndio maana serikali yetu inaona kama hawataki let us split the whole shit!
 
Watu hawaijui TAZARA. Ni kichefuchefu

Mtanzania ukiomba behewa kupeleka mzigo Mbeya au Makambako ni balaa.

Kwanza utatakiwa kulipa advance. Pili unapewa rate ya juu kuliko wanazopewa Wazambia. Mwishowake ilo behewa utalipata baada ya miezi sita.

Wazambia wao wanapewa rate ndogo tena kwa mkopo na behewa linapatikana ndani ya masaa 24.

Mwishowake wakopaji hawalipi wakati aliyelipa cash anasota!!!

LET US SPLIT IT
 
Kama alifanya uhaini kwenye ripoti ya Richmond kwanini asifanye vivyo hivyo kwenye kuisambaratisha TAZARA? Haya yote yanatokea kwasababu ya OMBWE la uongozi ; sintaona ajabu kuwa Vasco Dagama hajui kuwa haya ya Tazara ndio hivyo yanavyoendelea!!
 
Mkuu, watu wapumba.vu hawati kuona ukweli ulio dhahiri. Huu muundo wa Tazara umekuwa mwiba kwa Tz. Mfano mdogo ni usafiri wa mjini wa treni aka treni ya Mwakyembe. Wazambia wanapinga hata hilo.
Reli ilijengwa kimsingi kuwasaidia wao wakati ule lakini siku hizi wao ndio kikwazo kikubwa kwa sababu wana njia mbadala Afrika ya Kusini na Msumbuji.
Je Tanzania iendelee kufumba macho na kupata hasara eti ni ushirikiano?
Siku hizi lazima tuangalie maslahi ya kiuchumi zaidi si kisiasa. Tumesaidia sana watu kupata uhuru leo tunaambulia matusi.
Hakuna kitu kinafanyika tazara mpaka Zambia wakubali wakati huo huo hawana nia ya kuokoa hiyo reli. Bora tuende kivyetu na tuunganishe mikoa mingine kwenye mtandao. Mfano inaweza kutoka tunduma ikaenda sumbawanga. Njombe ikaenda ruvuma nk. Kwa mfumo wa sasa hilo gumu.

..Asante sana Mkuu....halafu si umewasikia wenyewe na Waziri wao...."we will stand on our own..." ....loud and clear......hiyo ni moja ya kauli ya Waziri.......kama alikuwa concerned na kauli alizosikia.....si angesema tu kuwa tutakutana hivi karibuni na tutalijadili hilo suala.....lakini kwa kuwa wanajua wanachokifanya.....they do not need us.....and.....they do not care!....mara moja kauli ikatolewa!.......Infact I applaud him for that boldness.....meaning they are ready to protect their interests......so should we!.....
 
Back
Top Bottom