Tanzania bado hatujapata Rais Mzalendo na Intellectual

Faizafox, hakuna mtu anayemzuia Magufuli kufanya kazi na yeye asituzuie kutoa maoni yetu ailikuwepo Nyerere akatuacha wakaja wengine wakatuacha hata huyu ataiacha Tanzania kama alivyoikuta.

Nikutoe wasiwasi tu kuwa unaongea na mkongwe wa siasa aliyeshiriki vita vya Kagera.

Wewe ni kikongwe najua unajua Tanzania lini ilianza kuteteleka kiuchumi na sababu zake ikiwepo vita ya Kagera, pamoja na uchumi kuharibika Nyerere hakuruhusu mabeberu kuchimba dhahabu yetu, kuchimba gesi na mafuta yetu, aliwaambia wayaache hayaozi hadi tutakapopata uwezo na ujuzi wa kuyachimba, lkn walioachiwa kiti ndio hawa wanayagawa kama njugu kwa kisingizio cha uzalendo bubu, Nyerere kaiacha nchi na viwanda vingi tu, kwa hilo hatuwezi kumlaumu Nyerere.

Magufuli angemrithi Nyerere leo tusingekuwa na dhahabu wala gesi wala mafuta, hana uwezo wa kulinda maliasili kwa akili.
Tanzania hatukuanza kutetereka kiuchumi sababu ya Kagera.

Umesahau Kennedy alileta msaada wa nini Tanganyika?

Tulikufa kiuchumi tulipoanza kutaifisha 1967.

Ungekuwa huruhusiwi kuongea ungekuwemo humu saa hizi?
 
"Uzalendo" (patriotism) ni hali ya mtu kuipenda, kuithamini na kujitoa kwa ajili ya nchi yake. Uzalendo unakaribiana sana na utaifa, ukizidi sana huitwa uzalendo kipofu au uzalendo bubu.

"Intellectual" (mtanisaidia kiswahili chake), is a person who engages in critical thinking, research, and reflection about society, proposes solutions, understand things especially complicated ideas.

Marais tuliowahi kuwa nao ni Nyerere tu aliyekuwa navyo angalau vyote.

Nyerere alikuwa Mzalendo na angalau alikuwa Intellectual.
Mwinyi aliipenda nchi ila hakuwa mzalendo wala hakuwa Intellectual. Tofautisha kuipenda nchi, kupenda watu wake na Uzalendo.
Mkapa alikuwa Intellectual lakini hakuwa Mzalendo.
Kikwete hakuwa Mzalendo lakini alikuwa mjanja half intellectual.
Magufuli ni Mzalendo lakini si Intellectual.

Nyerere alikuwa na uwezo wa kulinda maliasili za taifa alikuwa na uwezo wa kuwaambia wawekezaji wayaache madini hayaozi, alikuwa na mapenzi na nchi yake na watu wake alikuwa na uwezo kiakili na alikuwa haogopi challenges hata UN walitambua hilo.

Mwinyi hakuna na malengo yeyoye ya muda mrefu kwa nchi zaidi ya kusolve matatizo ya kipindi kifupi (biashara huria), hakuwa na uzalendo wala uwezo kiakili (critical thinking), alikuwa muoga wa challenges, alikuwa dhaifu kiuongozi.

Mkapa alikuwa na uwezo kiakili (critical thinker), hakuogopa challenges, lkn uwezo wake haukutumika kwa faida ya kulisaidia taifa (NBC case), alivunja misingi mingi ya kitaifa aliyoikuta, aligawa maliasili nyingi za taifa kwa wageni, hakuwa mzalendo.

Kikwete alipenda watu wake wa karibu (inner circle) lkn si nchi, half patriotism, hakupenda challenges ingawa hakuzikimbia (democracy case), hakujali sana maliasili za nchi kupotea iwe kwa kuibiwa au kwa mikataba feki, mengi alifanya kwa ajili yake na machache kwa ajili ya taifa (half intellectual).

Magufuli ni mzalendo halisi anaipenda nchi yake lakini siyo intellectual, anaogopa challenges, anataka kulinda maliasili za taifa lkn hana uwezo (hataki kujijengea uwezo) wa kugundua tricks za mabeberu, anatumia nguvu instead, (Acacia case), kwa kutambua hilo wajanja wanatumia uzalendo bubu kwa maslahi yao.

Ili tuendelee Tanzania tunataka Rais awe na vyote, angalau Nyerere alionekana kuwa navyo, tunataka rais kama Putin, rais kama Kagame, Abiy Ahmed ambao ni patriotic na intellectuals.

Kwa utajiri tulionao siku Tanzania ikipata Rais mzalendo na intellectual hakuna nchi Afrika Mashariki na Kusini itakayotupata kwa maendeleo na uchumi, itakuwa nchi ya kulinganishwa na SA.

Eti Kikwete alifanya Mengi kwa ajili yake na machache kwa ajili ya Taifa, hayo ni mawazo ambayo hayawezi kuwa substantiated na data!

Mleta mada hebu weka rekodi ya pesa zoote zilizopigwa kwenye awamu ya Kikwete halafu uniambie kama idadi yake inafika Trilion 2.4 ambazo CAG hajui ziko wapi na zimetumikaje tumikaje katika awamu hii, na hiyo ni just miaka 3 ya huyu wa sasa kukaa madarakani.

Let me tell you one thing, Kikwete hakuwa mtu wa kupenda misifa, lakini Miradi aliyoifanya Kikwete nchi hii ukianza kuiorodhesha laiti ingefanywa na huyu wa sasa, hayo masifa ambayo jamaa angetaka apewe yangezidi mlima Evarest kama siyo Kilimanjaro!

Tanzania ilishuhudia Ukuaji wa Uchumi wa asilimia 8 katika awamu ya Mwisho ya Kikwete kabla ya hapo haijawahi kutokea!
Miundo mbinu aliyojenga Kikwete kuanzia Mabarabara, Madaraja, ununuzi wa Vivuko, Miradi ya maji kama ule unatokea Ruvu kupitia Bunju kuja mpaka chuo cha Ardhi, Miradi ya Umeme (Umeme ulioingzwa kwenye Gridi ya Taifa na Awamu ya Kikwete unazidi umeme wa awamu zote kuanzia Nyerere mpaka Mkapa), Vyuo vikuu kama vile UDOM, Nelson Mandela, Shule za Kata, Barabara ya Mwendokasi, Terminal 3 hapo Airport Dar, Ukarabati wa Viwanja vingine vya ndege, Mloganzila hospital, Miradi ya Nyumba za Wanajeshi nchi nzima), Demokrasia pana, maslahi ya wafanyakazi, upandishwaji madarja kwa wakati, Uhuru wa vyombo vya habari, uwezeshwaji akina mama, Ukienda huko Jeshini alinunua zana Nzito na za kisasa za kijeshi (mama Banda wa Malawi alionyeshwa zana mwaka 2014 hapo uwanja wa Taifa wa Dar akaacha kuleta kidomodomo)

Kikwete miradi mingi alikuwa hafungui yeye, alikuwa anamtuma Ghalib Bilal, na alikuwa hahitaji kuchukua TBC kumrusha Live yeye kuonyesha watu kuwa anafanya kazi, kazi zake ni landmark zinajionyesha hahitaji kiki.

Hata hivyo hii hali Kikwete aliiona, kutokana na kutokupenda kumarket kazi zake, mwishoni aliwaambia wana CCM anzeni kuwaambieni wapinzani achievement za serikali yake, hata hivyo muda wa yeye kukaa madarakani ulikuwa umeisha kwa hiyo hakubahatika makada kumtengenezea "#MATAGA yake kama huyu wa sasa amabaye hata akifungua tawi la CRDB kesho unakutana na propaganda kuuubwa ya #TUNATEKELEZA

Nakwambia hivi, Heshima ya Nyerere ni kuleta uhuru wa nchi hii na kujenga Taifa, lakini Kikwete alikuwa ni Raisi bora bora sana
 
Magufuli anachofanya ni kutukumbusha ndoto zetu siyo kutimiza doto zetu,hajui kupanga na siku zote kupanga ndiyo msingi wa kufikia malengo.Nchi hii haina uwezo wa kujenga uwanja wa ndege chato,jknyerere,chato stadium,flyovers karibia 4,SGR railway,na kujenga barabara za lami kwa wakati mmoja.

Tutakubaliana kwamba magufl ana nia ya kutufikisha uchumi mkubwa ila uwezo hana maana hajui kupanga,kuchagua wala kutekeleza kwa usahihi na hajui kuchagua wa kumsaidia kuendeleleza nchi,ukishindwa kuwasikiliza wengine umechagua kufa bila taarifa.
 
Ukiwa genius hutumii nguvu kukariri mkuu.
Vitu ukiviangalia mara moja tu count inanasa kichwani.
Wala usifikir anakesha usiku na kutumia miguvu kukariri.
Nguvu anayotumia ni Kama ambayo unaitumia ww kwenda kazini na kurud lkn output yake inakuwa kubwa kuliko yako.

Nadhani bado ujajua maana ya mtu kuwa intellectual, kama unaweza sema jiwe ni intellectual basi you are real far away from understanding what the term intellectual means. Anyway haya ni waoni yako na yanaweza kuwa yamemezwa na mahaba pia, but mkuu no offense intended, uwe na asubuhi njema mkuu
 
hao unaowasema walikuwa na roho ngumu na bado wengine ni wagumu haswa na ndo maana unaona maendeleo, tatizo leo hii mtu akifanya jambo kwa maslahi ya taifa tunakuwa na midomo sana na tunalia haswa, miaka ya nyuma watu walipotea sana na haikuwahi julikana walipotelea wapi na kutokana na uhaba wa vyombo vya porojo habari hazikuenea ka hivi leo, yani ni ka vile kupotea kwa alibino miaka ile,

Mtu ka kagame si mtu wa mchezo mchezo bana anafanya lolote ilimradi nchi yake iwe vizuri, je tuko tayari kuwapa ushirikiano iwapo watakuwa ka hao viongovi ulowataja?
watu hawa wanasema tu hawamjui Putin wala kagame. hata nukta hawawajui. wale ni zaidi ya dictators
 
Ukiwa mtu wa kulalamika lalamika bila hoja za msingi, hata uwezo wako wa kufikiri unakuwa mdogo.

Tuwaulize Chadema, Patriotic & Intellectuals wapo kwenye chama chao?
Tundu Lissu ~msomi mtoto wa wazungu, anayeunga mkono democrasia hadi kuoana kwa uhuru~shoga
 
Mkuu Quinine naona unayemuongelea ni rais wa Tanzania ya kwenye play station na sio ile Tanzania halisi.

Hayupo mtu mwenye kufanan na huyo aliyeko kichwani mwako, upungufu wa mtu ndio sifa yake kuu ya kiuongozi.

Hata Marekani na Russia huwa wanakubaliana na wanachokipata kwa maana ya sifa za rais. Wamarekani husema "a lesser devil" wakimaanisha shetani mwenye afadhali kulinganisha na mwenzake anayegombea naye.


Ridhika na ukipatacho, huyo rais mwenye uzalendo na weledi mkubwa yupo ndotoni zaidi kulinganisha na uhalisia wa maishani.
Hoviyooooooo👹👹👷👷👷😆
 
Haya maandiko ya nani? "yeye asituzuie kutoa maoni yetu".

Kama umesahau yameandikwa na nani nenda post namba 139.
Ulisema tumwache rais afanyekazi, nikakujibu, "hakuna mtu anayemzuia Magufuli kufanya kazi na yeye asituzuie kutoa maoni yetu", kuna tatizo hapo.
 
Ulisema tumwache rais afanyekazi, nikakujibu, "hakuna mtu anayemzuia Magufuli kufanya kazi na yeye asituzuie kutoa maoni yetu", kuna tatizo hapo.
Malizia nikakujibu nini? Mbona humalizii? Mwiba wa koo?
 
Jiwe sio mzalendo, sio intellectual, na wala hakuwa na sifa ya kukalia kiti kile.
Hao wanaosema bwana mkubwa ni mzalendo ni waliozaliwa majuzi au ni wakale lakini wanajivesha usahaulifu
IMG_20190726_112639.jpeg
IMG_20190726_112712.jpeg
 
Back
Top Bottom