Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,353
- 1,935
Unajua nimekuwa nikatafakari sana mashambulizi yetu hapa. Halafu yule mama Anne Malecela naye amenifanya nizame kwenye fikra zaidi.
Kwa kweli tumekuwa mahodari sana wa kuonesha matatizo yetu na wakati mwingine hata kupendekeza namna ya kumaliza matatizo yetu. Juzi pia wapinzani wamefungua ukurasa mpya kabisa wa siasa zetu kwa kuweza kuwakilisha sio tu bajeti mbadala kwa mara ya kwanza lakini kwa kuwakilisha bajeti yenye akili kuliko ile ya serikali ya CCM.
Hii imethibitika zaidi baada ya hata wataalamu wa kiuchumo nchini mwetu kuishauri serikali "kuiba" baadhi ya nondo zilizomo katika bajeti ya wapinzani. Of course mimi pendekezo langu lilikuwa radical zaidi; nilimshauri dada Zakia aachene na bajeti yake uchwara na badala abebe bajeti ya kaka Hamad na Zitto nzimanzima kama ilivyo. Hata hivyo najua wataendelea na bajeti yao hiyohiyo kimkandamkanda maana wanajua tutasahau na wataibua liskendo lingine la kutusaulisha hili li bajeti.
OK, where am I going? Kuzama kwangu katika fikra hizi kumenifikisha katika hitimisho hili: sote tupo katika campaign. Lakini bahati mbaya inaonekana tunafanya campaign isiyo! Campaign yeyote lazima itambue mambo manne muhimu: muathirika ni nani? adu ni nani? fursa ya kumshinda adui ni zipi? na tukishamshinda adui tunapata nini?
Kwa maoni yangu ni wazi kwamba sisi wananchi sote tu waathirika. Adui yetu mkuu ni CCM. Fursa pekee tuliyo nayo ya kumshinda huyu adui ni uchaguzi wa 2010. Wapinzani wameonesha kwamba wanaweza wakawa mbadala mzuri. Zaidi ya yote kumbe kule CCM kuna akina Anne ambao wanafikiri kama sisi. By the way tayari tunaye Mzee ES hapa; huyu kuasi sio vigumu na anaweza akatupa mikakati ya ndani ya kumtwanga adui CCM kwenye uchaguzi.
Hivyo basi kuanzia sasa tutumie muda mwingi zaidi katika namna ya kushawishi wananchi kuelewa umuhimu wa kuifukuza CCM madarakani katika uchaguzo ujao. Hili ndiyo jambo ambalo litushughulishe zaidi kuanzia sasa hadi uchaguzi ujao. Hata wenzetu wakenya waliweza kuishinda KANU baada ya kugundua kwamba KANU ndio alikuwa adui wao mkubwa kuliko kitu kingine chochote. Ndiyo hayo tunaona leo wakenya wanaanza kutembea kifua wazi na mabega juu kwa kujivunia ukenya wao.
Huu ndio wito wangu wa leo.
Kwa kweli tumekuwa mahodari sana wa kuonesha matatizo yetu na wakati mwingine hata kupendekeza namna ya kumaliza matatizo yetu. Juzi pia wapinzani wamefungua ukurasa mpya kabisa wa siasa zetu kwa kuweza kuwakilisha sio tu bajeti mbadala kwa mara ya kwanza lakini kwa kuwakilisha bajeti yenye akili kuliko ile ya serikali ya CCM.
Hii imethibitika zaidi baada ya hata wataalamu wa kiuchumo nchini mwetu kuishauri serikali "kuiba" baadhi ya nondo zilizomo katika bajeti ya wapinzani. Of course mimi pendekezo langu lilikuwa radical zaidi; nilimshauri dada Zakia aachene na bajeti yake uchwara na badala abebe bajeti ya kaka Hamad na Zitto nzimanzima kama ilivyo. Hata hivyo najua wataendelea na bajeti yao hiyohiyo kimkandamkanda maana wanajua tutasahau na wataibua liskendo lingine la kutusaulisha hili li bajeti.
OK, where am I going? Kuzama kwangu katika fikra hizi kumenifikisha katika hitimisho hili: sote tupo katika campaign. Lakini bahati mbaya inaonekana tunafanya campaign isiyo! Campaign yeyote lazima itambue mambo manne muhimu: muathirika ni nani? adu ni nani? fursa ya kumshinda adui ni zipi? na tukishamshinda adui tunapata nini?
Kwa maoni yangu ni wazi kwamba sisi wananchi sote tu waathirika. Adui yetu mkuu ni CCM. Fursa pekee tuliyo nayo ya kumshinda huyu adui ni uchaguzi wa 2010. Wapinzani wameonesha kwamba wanaweza wakawa mbadala mzuri. Zaidi ya yote kumbe kule CCM kuna akina Anne ambao wanafikiri kama sisi. By the way tayari tunaye Mzee ES hapa; huyu kuasi sio vigumu na anaweza akatupa mikakati ya ndani ya kumtwanga adui CCM kwenye uchaguzi.
Hivyo basi kuanzia sasa tutumie muda mwingi zaidi katika namna ya kushawishi wananchi kuelewa umuhimu wa kuifukuza CCM madarakani katika uchaguzo ujao. Hili ndiyo jambo ambalo litushughulishe zaidi kuanzia sasa hadi uchaguzi ujao. Hata wenzetu wakenya waliweza kuishinda KANU baada ya kugundua kwamba KANU ndio alikuwa adui wao mkubwa kuliko kitu kingine chochote. Ndiyo hayo tunaona leo wakenya wanaanza kutembea kifua wazi na mabega juu kwa kujivunia ukenya wao.
Huu ndio wito wangu wa leo.