Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,354
- 1,943
- Thread starter
- #21
Mzee Kyoma, kama kawaida maneno yako ni mazito na mshale unaochoma.
Hata hivyo nasita kukabaliana na wewe kuhusu upinzani. Wazo uliloibua ndio wazo ambalo limekuwa likiwatofautisha Shivji na Baregu. Shivji yeye haamini kabisa katika vyama vya siasa, anataka wananchi ndio washike hatamu. Na huwa ana-argue in a very intelllectually convincing way as you may know him, lakini ukimuuliza watashika hatamu vipi bila kupitia vyombo vyenye uhalali wa kisheria, hakupi jibu. Msimamo wa Baregu ni kwamba hatuna njia ingine ya kuwakomboa hawa wananchi wetu na mfumo uliopo zaidi ya kupitia katika taasisi zilizopo za kisiasa zikiongozwa na vyama vya upinzani. Mimi nakubaliana na msimamo wa Baregu.
Ninachokipata katika ujumbe wako Kyoma ni kuwa wewe unataka ideal situation, ambayo kwa kweli haipo. Ndio sote tunataka ushindi wa wananchi, lakini ushindi huu hauwezi kupatikana bila kuwa na majemedari wa mapambano. Mimi naamni katika mapambano haya ya kisiasa majemadari wetu ni vyama vya siasa vya upinzani. Labda wewe unipe mbadala, in the absence of vyama vya siasa, ni namna gani tunaweza kuwapatia hawa wananchi huo ushindi ambao tunaongelea. Tatizo linalotukumba Tanzania ni watu wengi wenye mwanga na wasomi kama wewe kukosa ujasiri wa kujiunga na vyama vya upinzani. Tumekuwa hodari wa kuhukumu tukiwa pembeni as if hivi vyama vya upinzani ni duka au shamba la mtu fulani. Inabidi tubadilike na tujue kwamba vyama vya upinzani sio mali za watu wachache, hizi ni taasisi za kijamii na vyombo mojawapo vya kuongoza mapambano katika mabadiliko tunayoyataka. Kwa mfumo wetu waa siasa na sheria tulizonazo hatuna uwanja mwingine wa mapambano nje ya vyama vya siasa. Mimi naamini kabisa kwa mujibu wa mfumo wetu wa kisiasa, kujaribu kupambana nje ya vyama vya siasa ni njia rahisi ya kukwepa mapambano!
Mwisho, naomba nitofautiane nawe sana kuhusu mafanikio ya vyama vya upinzani vilivyoshinda katika nchi zingine nchi Afrika. nafikiri umeingia katika mtego wa propaganda za CCM za kusema kwamba vyama vya upinzani vilivyoshinda katika nchi zingine havikuleta mafanikio yeyote. Hii sio kweli kwa nchi zote. Mfano wa karibu ni wa majirani zetu Kenya. Tangu KANU ifukuzwe madarakani mabadiliko mengi yamepatikana yakiwemo: kutoa elimu ya msingi bure (nasi tukawaiga), kuanzia mwakani wanaanza kutoa elimu ya sekondari bure. uchumi wao umekuwa mara mbili, wameweza kupunguza idadi ya watu maskini kwa 20%. Soma tena bajeti za Kenya na Tanzania za mwaka huu. Bajeti ya Kenya inatokana na vyanzo vya ndani kwa 95% na wanategemea misaada ya wazungu kwa 5% pekee. Sisi, tunajitegemea kwa 58% tu na tutawapigia magoti wazungu kwa 42% (note: mwaka jana ilikuwa 40%!). Kikubwa zaidi, kwa kuitoa KANU, wananchi wa Kenya walipata nguvu za ajabu; sasa wanajua kuwa wana uwezo wa kuitoa serikali madarakani kwa njia ya uchaguzi wakati wowote wakitaka. Huu kwangu ndio ushindi wa maana kuliko mwingine wowote unaoweza kuufikiria, power to people, ndiyo hayo uliyotupa mfano wa Califiornia.
Ndio NARC hawajafanikiwa kuleta mabadiliko ya katiba kama walivyoaidi. Lakini tusisahau kwamba angalau walipeleka mapendekezo ya katiba kwa wananchi na wananchi wakayakataa. Na huu ndio msingi wangu wa kusema kuwa wakenya sasa wanatembea kifua mbele. They now know they have power over their government. They know they can say no to government if they want to. Sisi je? Ni kujidanganya sana kufikiri wananchi wa Tanzania wana nguvu za kisisasa kushinda Kenya. Hakuna kitu kama hicho. Mabadiliko yaliyotokea Kenya baada ya KANU kuondoka madarakani ni makubwa mno na yanapaswa kututia moyo na wala siyo kutukatisha tamaa.
Sitaki kuingia kwa undani katika nchi zingine. Lakini fuatilia kwa makini tena ujue mabadiliko yaliyopatikana nchini Senegal baada ya Wade kushinda. Fuatilia pia Ghana baada ya Kufour,utagundua kwamba things have changed drastically for better.
Hata hivyo nasita kukabaliana na wewe kuhusu upinzani. Wazo uliloibua ndio wazo ambalo limekuwa likiwatofautisha Shivji na Baregu. Shivji yeye haamini kabisa katika vyama vya siasa, anataka wananchi ndio washike hatamu. Na huwa ana-argue in a very intelllectually convincing way as you may know him, lakini ukimuuliza watashika hatamu vipi bila kupitia vyombo vyenye uhalali wa kisheria, hakupi jibu. Msimamo wa Baregu ni kwamba hatuna njia ingine ya kuwakomboa hawa wananchi wetu na mfumo uliopo zaidi ya kupitia katika taasisi zilizopo za kisiasa zikiongozwa na vyama vya upinzani. Mimi nakubaliana na msimamo wa Baregu.
Ninachokipata katika ujumbe wako Kyoma ni kuwa wewe unataka ideal situation, ambayo kwa kweli haipo. Ndio sote tunataka ushindi wa wananchi, lakini ushindi huu hauwezi kupatikana bila kuwa na majemedari wa mapambano. Mimi naamni katika mapambano haya ya kisiasa majemadari wetu ni vyama vya siasa vya upinzani. Labda wewe unipe mbadala, in the absence of vyama vya siasa, ni namna gani tunaweza kuwapatia hawa wananchi huo ushindi ambao tunaongelea. Tatizo linalotukumba Tanzania ni watu wengi wenye mwanga na wasomi kama wewe kukosa ujasiri wa kujiunga na vyama vya upinzani. Tumekuwa hodari wa kuhukumu tukiwa pembeni as if hivi vyama vya upinzani ni duka au shamba la mtu fulani. Inabidi tubadilike na tujue kwamba vyama vya upinzani sio mali za watu wachache, hizi ni taasisi za kijamii na vyombo mojawapo vya kuongoza mapambano katika mabadiliko tunayoyataka. Kwa mfumo wetu waa siasa na sheria tulizonazo hatuna uwanja mwingine wa mapambano nje ya vyama vya siasa. Mimi naamini kabisa kwa mujibu wa mfumo wetu wa kisiasa, kujaribu kupambana nje ya vyama vya siasa ni njia rahisi ya kukwepa mapambano!
Mwisho, naomba nitofautiane nawe sana kuhusu mafanikio ya vyama vya upinzani vilivyoshinda katika nchi zingine nchi Afrika. nafikiri umeingia katika mtego wa propaganda za CCM za kusema kwamba vyama vya upinzani vilivyoshinda katika nchi zingine havikuleta mafanikio yeyote. Hii sio kweli kwa nchi zote. Mfano wa karibu ni wa majirani zetu Kenya. Tangu KANU ifukuzwe madarakani mabadiliko mengi yamepatikana yakiwemo: kutoa elimu ya msingi bure (nasi tukawaiga), kuanzia mwakani wanaanza kutoa elimu ya sekondari bure. uchumi wao umekuwa mara mbili, wameweza kupunguza idadi ya watu maskini kwa 20%. Soma tena bajeti za Kenya na Tanzania za mwaka huu. Bajeti ya Kenya inatokana na vyanzo vya ndani kwa 95% na wanategemea misaada ya wazungu kwa 5% pekee. Sisi, tunajitegemea kwa 58% tu na tutawapigia magoti wazungu kwa 42% (note: mwaka jana ilikuwa 40%!). Kikubwa zaidi, kwa kuitoa KANU, wananchi wa Kenya walipata nguvu za ajabu; sasa wanajua kuwa wana uwezo wa kuitoa serikali madarakani kwa njia ya uchaguzi wakati wowote wakitaka. Huu kwangu ndio ushindi wa maana kuliko mwingine wowote unaoweza kuufikiria, power to people, ndiyo hayo uliyotupa mfano wa Califiornia.
Ndio NARC hawajafanikiwa kuleta mabadiliko ya katiba kama walivyoaidi. Lakini tusisahau kwamba angalau walipeleka mapendekezo ya katiba kwa wananchi na wananchi wakayakataa. Na huu ndio msingi wangu wa kusema kuwa wakenya sasa wanatembea kifua mbele. They now know they have power over their government. They know they can say no to government if they want to. Sisi je? Ni kujidanganya sana kufikiri wananchi wa Tanzania wana nguvu za kisisasa kushinda Kenya. Hakuna kitu kama hicho. Mabadiliko yaliyotokea Kenya baada ya KANU kuondoka madarakani ni makubwa mno na yanapaswa kututia moyo na wala siyo kutukatisha tamaa.
Sitaki kuingia kwa undani katika nchi zingine. Lakini fuatilia kwa makini tena ujue mabadiliko yaliyopatikana nchini Senegal baada ya Wade kushinda. Fuatilia pia Ghana baada ya Kufour,utagundua kwamba things have changed drastically for better.