Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,106
Nani anaweza kutueleza tangu Makonda aanze kudhalilisha watendaji wa umma na wananchi kwa mlango wakusikiliza kero ametatua kero ngapi?
Kuna maeneo ameelekeza watu watengeneze madawati ya kusikiliza kero, alipoondoka kwenye wilaya wakurugenzi wakarudi kwenye basics
Kuna Sehemu mfano Rukwa amekwenda kutatua kero kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa, ameondoka kila mtu kutawanyika kwenye kazi zake za kila siku.
Hakuna Sehemu yoyote alipopita akaacha maelekezo yake yanafanyiwa kazi. Watendaji wanampuuza.
Na hapa atakuwa amekasirika, atakacho kwenda kufanya ni kupendekeza watumbuliwe au wahamishwe kuonekana kama yeye ana nguvu
Swali kubwa, je atasikilizwa na wakubwa zake? Wakimsikiliza yeye fukuto ndani ya chama na serikali litakuwaje?
Tunanufaika vipi kama wananchi na siasa hizi? Lakini mbona kote anakopita hakuna Sehemu anapouliza mbunge wa jimbo husika yupo wapi? Wabunge wanaowakilisha wananchi kama kweli hizi ndizo kero za wananchi wao wanazosemea wapi?
Ni wapi tumemsikia akimtuhumu waziri kwamba hakuna huduma za afya na shule? Katavi kuna shida kubwa ila hajasema kwa sababu msimamo wa chama nikusema tumejenga.....je amejionea vilivyojengwa?
Kuna maeneo ameelekeza watu watengeneze madawati ya kusikiliza kero, alipoondoka kwenye wilaya wakurugenzi wakarudi kwenye basics
Kuna Sehemu mfano Rukwa amekwenda kutatua kero kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa, ameondoka kila mtu kutawanyika kwenye kazi zake za kila siku.
Hakuna Sehemu yoyote alipopita akaacha maelekezo yake yanafanyiwa kazi. Watendaji wanampuuza.
Na hapa atakuwa amekasirika, atakacho kwenda kufanya ni kupendekeza watumbuliwe au wahamishwe kuonekana kama yeye ana nguvu
Swali kubwa, je atasikilizwa na wakubwa zake? Wakimsikiliza yeye fukuto ndani ya chama na serikali litakuwaje?
Tunanufaika vipi kama wananchi na siasa hizi? Lakini mbona kote anakopita hakuna Sehemu anapouliza mbunge wa jimbo husika yupo wapi? Wabunge wanaowakilisha wananchi kama kweli hizi ndizo kero za wananchi wao wanazosemea wapi?
Ni wapi tumemsikia akimtuhumu waziri kwamba hakuna huduma za afya na shule? Katavi kuna shida kubwa ila hajasema kwa sababu msimamo wa chama nikusema tumejenga.....je amejionea vilivyojengwa?