Tangu lini Mke Ndani Ya Ndoa Akaomba Uhuru ili Kutoka Nje Ya Ndoa? Aruhusiwe?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,508
113,629
Wanabodi,
Hiki ni kisa cha kufikirika tuu lakini ni kisa cha kweli na ni cha ajabu kweli, ila ndio ukweli wenyewe kwa kitakachotokea kwenye ndoa ya wawili hawa!.

Kwa hapa Tanzania, kwa kawaida tuna aina mbili kuu za ndoa, yaani type ya ndoa, ni tuna ndoa ya mke mmoja, na ndoa za wake wengi, halafu kwenye form ya ndoa, tuna aina 4, ndoa za kidini, ndoa za kisekali, ndoa za kimila, na ndoa za dhana ya ndoa, yaani presumption of marriage, hii ni ndoa ambayo watu wamechukuana tuu na kuishi pamoja bila kufunga rasmi ndoa.

Ndoa yetu ninayoizungumza kwenye muktadha huu, ni ndoa ya watu wawili wamependana wenyewe na ridhaa zao wenyewe wakaamua kuingia kwenye mahusiano rasmi ya ndoa ya mke mmoja mume mmoja, ambao walipaswa kuishi nyumba moja, nyumba ya ndoa.

Lakini wawili hawa waliamua kufunga ndoa ya ajabu kidogo!. Walifunga ndoa ya mke mmoja mume mmoja na kuishi nyumba moja kwa mwanamume. Mke au mume utaachana na wazazi wako, utaandamana na mumeo/mkeo, mtakuwa mwili mmoja!.

Kwa ndoa hii wakaamua ni ndoa ya mke mmoja ila nyumba mbili, ndani ya nyumba ya mume, ni ndoa ya mke mmoja, mume mmoja nyumba moja. Lakini mke akapewa uhuru, kule kwao, akawa ana nyumba yake na ana uhuru wa kujiamulia mambo yake madogo madogo ya kule ndani kwake. Hivyo ndoa yetu hii ni ndoa ya mke mmoja nyumba mbili!, nyumba moja ni ndoa ya mke mbili, nyumba moja ni ndoa ya mke mmoja halafu kule upande pili ni ndoa ya mitala!.

Wakati ndoa hiyo ikiendelea mke mke akiwa nyumba kuu ni mke mwema, mke mmoka mume mmoja, nyumba moja, ila akiwa kule kwao kwenye nyumba ya pili, kwa vile kule mke anao uhuru wake, kule akaanza kuutumia vibaya uhuru huo kwa kutoka nje ndoa hiyo, mume akagundua, mkewe akiwa kwao, huwa anatoka nje ya ndoa!, lakini kwa vile anampenda sana mkewe sio tuu hata kumkanya alishindwa hata kumuuliza tuu alishindwa kwa kwa kuhofia asije akamuuliza mke akakasirika na akadai talaka yake!, mume akaona kuliko kumuuliza na kuhatarisha ndoa ni bora ajikalie kimya avumilie!.

Licha ya mume kumtimizia mkewe mahitaji yake yote ya huku na kule, ikiwemo kumpa kila kitu alichokitaka, sasa mke anataka uhuru zaidi!, ile kujiiba na kutembea nje ya ndoa bila kuulizwa, sasa anataka ihalalishwe, mke apewe uhuru rasmi wa kutembea na yeyote anayemtaka zile siku akiwa kule kwake sio kwa kujiiba iba, iwe wazi kihalali!.

Ndoa hii ni muungano wetu, ndani ya muungano kimataifa ni muungano wa union wa nchi moja ya JMT, yenye serikali moja (nyumba) ya JMT, chini ya rais mmoja wa JMT. Wanandoa Tanganyika na Zanzibar, kila mmoja amawaacha baba yake na mama yake, na kuandamana na mwenzake kuunda JMT ambayo ni nchi moja.

Lakini kitaifa, nje ya muungano, muungano wetu ni federation, wenye nchi mbili, Tanzania bara na Tanzania wisiwani, au Tanzania Zanzibar, zenye serikali mbili ya JMT na SMZ, zenye marais 2, Rais wa JMT na rais wa Zanzibar!.

Mwaka 2010 Zanzibar ilibadili katiba yake na kutoka nje ya ndoa ya JMT, ina bendera yake, wimbo wake wa taifa, sasa inataka uhuru zaidi wa kujifanyia mambo ya kimataifa kama kujiunga OIC!.

Mshenga wa mgogoro huu wa ndoa, hiii Jaji Joseph Warioba, ameshauri uhuru huu kwa mke, utolewe!, badala ya kuendeleza ndoa ya mke mmoja, mume mmoja nyumba moja, ameshauri, kufuatia mke kuamua kwa dhati, kutaka uhuru zaidi hadi wa kutembea nje ya ndoa!, njia pekee ya kuinusuru ndoa hii, ni kumpa huyo mke uhuru zaidi, kwa kumruhusu aishi kwa uhuru zaidi, badala ya ndoa ya mke mmoja mume mmoja, nyumba moja, ndoo hii ikubaliwe kuwa ni ndoa ya mke mmoja, mume mmoja nyumba tatu!, ila kila mtu kuishi kwenye nyumba yake kwa uhuru, ila pia iwepo nyumba ya tatu ya ndoa ambayo mke na mume, watakutania hamu, ile siku watakapo hitaji kutimiza hitaji la ndoa!.

Jee ungekuwa wewe, ungekubali?!.

Kama unaamini kwenye ndoa ya mke mmoja mume mmoja nyumba moja!, pigania serikali moja!.

Kama unaamini kwenye ndoa ya mke mmoja mume mmoja nyumba mbili kama hivyi ilivyo sasa kwa kila mtu na haki zake kwa nyumba ya watu wawili, pigania serikali mbili!.

Lakini kama unakubali na ndoa ya mke mmoja, mume mmoja nyumba tatu ili kila mmoja awe huru, na mke awe na uhuru wa kutembea nje ya ndoa!, unga mkono serikali tatu!.

Baada ya kumsikia Jaji Warioba leo, akitoa sababu za Tume yake kupendekeza serikali tatu!, kumbe nia ni ili kumpa uhuru zaidi mke, afanye anachotaka, hadi kutembea nje, bila kuivunja ndoa!.

Mungu Ibariki Tanzania!.

Muungano Milele na utalindwa kwa gharama yoyote!.

Paskali
 
mimi naona ni kama ndoa ya mke mmoja mume mmoja kila mtu na chumba chake,lakini kuna chumba cha tatu cha makutanio ya hao mke na mume kwa mambo maalum!na kila chumba kina sheria na katiba yake! haya maisha wapo pia watu wanaishi siku hizi ktk ndoa za namna hii ,na siku zinasonga mbele!
 
mimi naona ni kama ndoa ya mke mmoja mume mmoja kila mtu na chumba chake,lakini kuna chumba cha tatu cha makutanio ya hao mke na mume kwa mambo maalum!na kila chumba kina sheria na katiba yake! haya maisha wapo pia watu wanaishi siku hizi ktk ndoa za namna hii ,na siku zinasonga mbele!
Ukumbuke mwanzo mke alitoka nje ya ndoa ndipo akaomba uhuru zaidi ili aendelee kutoka, na ataingia chumba cha kukutania siku atakapo jisikia yeye!. Huku kwake akiendelea kupokea wageni!. Utaweza kuvumilia?!.
Paskali
 
Ndugu pasco,hebu tuambie hiyo ndoa ilifungishwa wapi kanisani au msikitini?ndoa bila ya sheria za ndoa inakuwa c ndoa,kama unakiri mkeo anatoka nje ya ndoa je upo tayari kufa kwa ukimwi kisa unampenda mke?utakuwa mtu wa ajabu kufurahia mkeo madume wengine wanampandia halafu wewe unaonesha mijino tu,mume bw-e-ge!wasiwasi wangu wakati mkeo kaenda kwa dume jengine basi nawewe unatumia nafasi hiyo kuingiza dume jengne likupumulie kichogoni.
 
Baada tu ya mke kutembea nje ya ndoa, na hata baada ya kuonywa na hakubali, tayari ndoa hiyo ilikuwa imevunjika! Kuendelea nayo na mke huyu hajakubali kuacha, ni unafiki tu. Tulikuwa na nchi moja yenye serikali mbili. Kulikuwa na kero lakini zilikuwa zinashughulikiwa hata zilishaundiwa Wizara kabisa. Lakini Zanzbar ilibadili katiba yake na kutamka wazi kuwa wao ni nchi kamili. Wana bendera yao, hata juzijuzi ilikamatwa ikipeperushwa na meli za Iran zilizowekewa vikwazo, wana wimbo wao wa taifa, Raisi wao ni Mkuu wa vikosi vyao vya ulinzi na anapigiwa mizinga 21 kama amirijeshi mkuu, mambo yanayopitishwa na bunge la Muungano si halali hadi yajadiliwe na baraza la wawakilishi kule Zenj, na mambo mengi yanayoonesha kuwa tayari wamejitoa kwenye muungano hata kama hawajatamka hilo. Tayari kuna tatizo. Zanzbar kama nchi kamili sasa imejiunga na nchi gani ili kutengeneza muungano? Sisi sio nchi moja yenye serikali 2 tena. Sasa ni Nchi ya Zanzbar ambayo haikuwepo tangu 1964 hadi hivi karibuni walipobadili katiba yao, na nchi ya...Tanganyika??? ah! nchi ya muungano?.. ah! au nchi gani sasa? Sio Tanzania kwani Tanzania ilikuwa muungano wa nchi mbili kuwa moja. Lazima Tanganyika iwepo sasa. Nchi moja ya Tanzania ilishavunjika sasa ni nchi mbili. Moja ni Zanzbar na moja ni nini? Hapa lazima hata na mfumo wa Muungano ubadilike. Haiwezekani kuweka viraka tena.Aidha Zanzbar ibadili katiba yake tena na kurudi tuwe nchi moja ya Tanzania au Tanganyika nayi iibuliwe upya, na mfumo wa Muungano ubadilike kabisa. Vinginevyo ni unafiki na wanafiki wote hawataenda peponi kulingana na misahafu ya dini zote.
 
Wanabodi,
Hiki ni kisa cha ajabu kidogo ila ndio ukweli wenyewe kwa kitakachotokea kwenye ndoa ya wawili hawa!.

Watu wawili wamependana na ridhaa zao wenyewe wakaamua kuingia kwenye ndoa ya mke mmoja mume mmoja, jumla wawili!.

Wakati ndoa hiyo ikiendelea mke akaanza kutoka nje ndoa hiyo, mume akajua lakini kwa vile anampenda sana mkewe sio tuu hata kumkanya alishindwa hata kumuuliza ulishindwa kwa kumhofia mkewe asije muuliza mke akakasirika na kudai talaka yake!, mume akaona kuliko kuvunja ndoa bora avumilie!.

Licha ya mume kumtimizia mkewe kila kitu, sasa mke anataka uhuru zaidi!, ile kujiiba na kutembea nje ya ndoa sasa ihalalishwe, mke apewe uhuru rasmi wa kutembea na yeyote anayemtaka!.

Mshenga wa mgogoro huu wa ndoa, Jaji,Joseph Warioba, ameshauri uhuru huu kwa mke, utolewe!,, badala ya kuendeleza ndoa ya mke mmoja, mume mmoja, ameshauri, kufuatia mke kuamua kwa dhati, kutembea nje ya ndoa, njia pekee ya kuinusuru ndoa hii, ni kumpa huyo mke uhuru zaidi, kwa kumruhusu aishi kwa uhuru zaidi, badala ya ndoa ya mke mmoja mume mmoja, ndo ikubaliwe kuwe ya mke mmoja, mume mmoja ila kila mtu kuishi kwenye nyumba yake kwa uhuru, ila pia iwepo nyumba ya tatu ya ndoa mbayo mke na mume, watakutania hapo, siku watakapo hitaji kutimiza ndoa!.

Jee ungekuwa wewe, ungekubali?!.

Kama unaamini ndoa ya mke mmoja mume mmoja nyumba moja!, pigania serikali moja!.
Kama unakubali ndoa ya mke mmoja mume mmoja hivyo kila mtu na haki zake kwa nyumba ya watu wawili, pigania serikali mbili!.

Lakini kama unakubali na ndoa ya mke mmoja, mume mmoja ila mke awe na uhuru wa kutembea nje ya ndoa!, unga mkono serikali tatu!.

Baada ya kumsikia Jaji Warioba leo, akitoa sababu za Tume yake kupendekeza serikali tatu!, kumbe nni ili kumpa uhuru mke, afanye anachotaka, hadi kutembea nje, bila kuivunja ndoa!.

Mungu Ibariki Tanzania!.

Muungano Milele!.

Pasco.
Tulio soma sheria tuna amini kuwa
1. Ndoa ni issue ambayo inatakiwa kuwa treated unique na wala si kulinganisha na nchi
2. Kama unalinganisha na Muungano je nani kamuoa mwenzake kwa maana ya kwamba nani mwanaume
3. Na kama mwanaume ni Tanganyika basi hana hadhi ya kuendelea na ndoa yaani anamuacha Mke wake anazini ovyo tu nje ya ndoa halafu yeye anaridhika
3. The purpose of marriage is to maintain stability of the family na kunapo kuwa na migogoro basi serikali huingilia kati ili kulinda hadhi ya ndoa hata muungano imebidi serikali kupitia kwa Warioba imeamua kuingilia kati ili kumaintain Stability kwa maana ya kuondoa kero. Kama mimi ni jaji kwa kuzingatia principle ya ndoa ya "best interest of the child " kuwa kuna wakati nitaangalia maslahi ya wananchi lakini sia ya vyama
 
Ndugu pasco,hebu tuambie hiyo ndoa ilifungishwa wapi kanisani au msikitini?ndoa bila ya sheria za ndoa inakuwa c ndoa,kama unakiri mkeo anatoka nje ya ndoa je upo tayari kufa kwa ukimwi kisa unampenda mke?utakuwa mtu wa ajabu kufurahia mkeo madume wengine wanampandia halafu wewe unaonesha mijino tu,mume -----!
Mkuu Bobwe, ndoa ni ya mkeka!, mwanzo mume alimbaka tuu mke, ila mke akajituliza tuli, mwaka 1984 akataka kutoka nje ya ndoa, tukamuadabisha yule kuwadi alokuwa akiwatongo..a mabwana wa nje!, ndipo akaanza kutembea nje!, 2010 akajitambulisha kuwa yupo kivyake vyake!, sasa anaomba ruhusa huo uhuru wa kuwa kivyake vyake ukubaliwe na mumewe!, kama ungekuwa wewe, na mke bado unampenda!, utakubali?!.
Paskali
 
Futa hii post pasco!wewe mume una matatizo mkeo akitoka unaingiza bwana wako anekukamatisha ukuta na ndio maana unafurahia mkeo akitoka nje.
 
Naona huu mfano ni irrelevant kwa issue iliyoko mezani. Ni lini Tanganyika iliioa Zanzibar. Na ni nani alohalalisha Zanzibar ni mke (apangiwe taratibu za kuishi) na Tanganyika ni mume ampangie Zanzibar jinsi ya kuishi.
 
Kila muungano unapofananishwa na ndoa, basi Zanzibar inapewa nafasi ya mke! Kwa nini? Pasco
 
Last edited by a moderator:
Kila muungano unapofananishwa na ndoa, basi Zanzibar inane wa nafasi ya mke! Kwa nini? Pasco
Anyegharimia uendeshaji wa nyumba ndie mume!, kikawaida mwenye umbo dogo ndie mke!, na kama hujui yupi ni mke na yupi ni mume, fuatilia, anyedai kupewa talaka ndie mke!, mumu haombi talaka, huwa anaacha tuu!.
Pasco
 
Mkuu Bobwe, ndoa ni ya mkeka!, mwanzo mume alimbaka tuu mke, ila mke akajituliza tuli, mwaka 1984 akataka kutoka nje ya ndoa, tukamuadabisha yule kuwadi alokuwa akiwatongo..a mabwana wa nje!, ndipo akaanza kutembea nje!, 2010 akajitambulisha kuwa yupo kivyake vyake!, sasa anaomba ruhusa huo uhuru wa kuwa kivyake vyake ukubaliwe na mumewe!, kama ungekuwa wewe, na mke bado unampenda!, utakubali?!.
Pasco

Kumbe ulibaka?
 
Wanabodi,
Hiki ni kisa cha ajabu kidogo ila ndio ukweli wenyewe kwa kitakachotokea kwenye ndoa ya wawili hawa!.

Watu wawili wamependana na ridhaa zao wenyewe wakaamua kuingia kwenye ndoa ya mke mmoja mume mmoja, jumla wawili!.

Wakati ndoa hiyo ikiendelea mke akaanza kutoka nje ndoa hiyo, mume akajua lakini kwa vile anampenda sana mkewe sio tuu hata kumkanya alishindwa hata kumuuliza ulishindwa kwa kumhofia mkewe asije muuliza mke akakasirika na kudai talaka yake!, mume akaona kuliko kuvunja ndoa bora avumilie!.

Licha ya mume kumtimizia mkewe kila kitu, sasa mke anataka uhuru zaidi!, ile kujiiba na kutembea nje ya ndoa sasa ihalalishwe, mke apewe uhuru rasmi wa kutembea na yeyote anayemtaka!.

Mshenga wa mgogoro huu wa ndoa, Jaji,Joseph Warioba, ameshauri uhuru huu kwa mke, utolewe!,, badala ya kuendeleza ndoa ya mke mmoja, mume mmoja, ameshauri, kufuatia mke kuamua kwa dhati, kutembea nje ya ndoa, njia pekee ya kuinusuru ndoa hii, ni kumpa huyo mke uhuru zaidi, kwa kumruhusu aishi kwa uhuru zaidi, badala ya ndoa ya mke mmoja mume mmoja, ndo ikubaliwe kuwe ya mke mmoja, mume mmoja ila kila mtu kuishi kwenye nyumba yake kwa uhuru, ila pia iwepo nyumba ya tatu ya ndoa mbayo mke na mume, watakutania hapo, siku watakapo hitaji kutimiza ndoa!.

Jee ungekuwa wewe, ungekubali?!.

Kama unaamini ndoa ya mke mmoja mume mmoja nyumba moja!, pigania serikali moja!.
Kama unakubali ndoa ya mke mmoja mume mmoja hivyo kila mtu na haki zake kwa nyumba ya watu wawili, pigania serikali mbili!.

Lakini kama unakubali na ndoa ya mke mmoja, mume mmoja ila mke awe na uhuru wa kutembea nje ya ndoa!, unga mkono serikali tatu!.

Baada ya kumsikia Jaji Warioba leo, akitoa sababu za Tume yake kupendekeza serikali tatu!, kumbe nni ili kumpa uhuru mke, afanye anachotaka, hadi kutembea nje, bila kuivunja ndoa!.

Mungu Ibariki Tanzania!.

Muungano Milele!.

Pasco.

Team lumumba njooni huku mwenzenu anasema jk na shein wananini vile, njooni mtwambie sisi umeshindwa kumuelewa! au ndo mambo ya Cameroon
 
Pasco wish kama ungekua mwalimu wa hadithi au kutunga stori kama akina Shigongo ungeuza sana.

Back to the topic unapotumia neno mke na mume unatuwekea limit ya kuchangia ila tambua kua Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikosewa katika vipengele vya kiutendaji na mkataba ulisahiniwa haraka haraka bila kufikiria mara mbili hii ni kutokana na hali ilivyokua kipindi hicho huko visiwani, waarabu na maadui wengne walikua wanaimezea mate Zanzibar .

Makosa gani walifanya Karume na Nyerere !
Kosa ambalo walifanya ni kutofanya Unguja na Pemba kuwa mkoa na si nchi ilo ndilo kosa kubwa waliofanya viongozi hao kipindi hicho, je nini madhara ya Zanzibar kuwa nchi na siyo mkoa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tz ? Madhara ni kwamba Zanzibar wanaona kwamba nchi yao ni inamezwa na Tanzania bila kutazama mbele na kuhoji je Serikali ya Tanganyika ipo wapi ? Kwa Watanzania bara na wao wanaona ni kejeli kwa eneo ndogo kuliko ata mkoa wa Mbeya unakua na mamlaka yake kamili huku kila siku wakilalamika kuonewa na Watanganyika sasa wabara nao wanataka Tanganyika yao.

NINI SULUHISHO:
Suluhisho ni serikali moja yenye nia moja kua Zanzibar iwe kama mkoa au jimbo na si nchi ila kwa hili tushachelewa sn.
Solution nyingne ni serikali tatu ambayo najua aitodumu kwa mda mrefu na mifano tunazo kutoka nchi kadhaa walio adopt system km hili. Mf Scotland watapga kura ya kuwa autonomous state baadae kutoka Uingereza. Ni hayo tu.
 
Last edited by a moderator:
Zanzibar sijajua faida yake kwa Tanganyika,anayejua tafadhali anisaidie maana tunaing'ang'nia sana. Hopeless kabisa.
 
Back
Top Bottom