Nenda sehemu zenye migodi midogo midogo kama pande za katoro, lwamugasa, nyarugusu, mgusu, huko mkoani geita au kakola, nyakagwe mkoani shinyanga.
Huko kote mimi nimepita, nimepiga kazi za kutwa kwa elfu8 hadi kumi ila siku hizi migodi mingi ukiingia asubuhi saa moja unatoka kesho yake asubuhi saa moja unalipwa kati ya 20k hadi 30k.
Kazi kubwa ni kupakia mawe saizi ya kawaida saana na sio mchaka mchaka kivile kupumzika a.k.a KULA TANO kupo sana tu.
Misosi ipo mala mbili hadi tatu kutegemeana na mda wako wa kazi.
Kama huwezi kuingia duarani bado kuna kazi za juu kifupi kazi ni nyingi hadi kwenye plants za kuozesha marudio. Yaani madogo huku, kina mama kina baba wapo plants wanapiga kaz hawakosi 450k had 600k kwa mwezi.
Bei ya dhahabu inapanda na migodi inaongezeka so ajira pia zinaongezeka.
Hiyo 50k ya kufuga kuku!!!!???? Kuku mmoja jogoo ni 50k au we uko kijijini sana? Halafu kuanza na kuku wawili utatoka lini br??