Tangazo muhimu kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT mujibu wa sheria 2016

Naisoma360

JF-Expert Member
Jan 23, 2015
820
491
180681_158735330845567_2210285_n.jpg




TANGAZO


MABADILIKO YA TAREHE YA KURIPOTI KATIKA MAKAMBI YA JKT KWA VIJANA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT KWA MUJIBU WA SHERIA MWAKA 2016.


Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) linautangazia umma mabadiliko ya tarehe ya kuripoti makambini vijana wote waliohitimu kidato cha sita mwaka 2016 na kuchaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2016.


Taarifa ya awali kwa vyombo vya habari nchini ilianisha tarehe ya kuripoti kuwa ni tarehe 01 June hadi tarehe 05 Juni 2016. Tarehe hiyo imeafanyiwa mabadiliko badala yake vijana hao wanatakiwa kuripoti katika makambi ya JKT waliyopangiwa kuanzia tarehe 07 June hadi tarehe 10 June 2016 bila kukosa.


Atakayesikia tangazo hili amtaarifu na mwezie.



Imetolewa na:

Kurugenzi ya Habari na Uhusiano

Makao Makuu ya JKT

Tarehe 31 Mei 2016
 
Haya sawa kuna kijana mwenzangu hapa ntampa taarifa maana yeye si mfuatiliaji wa vyombo vya habari anaweza akaenda kuripoti kesho.
 
Back
Top Bottom